benchi la ufundi la tsn media group wakati wa fainali za kombe la nssf leo klabu ya sigara chang'ombe ambapo timu ya kampuni hii ambayo ni wachapishaji wa magazeti ya daily news, sunday news, habarileo na sportscene iliibamiza uhuru na mzalendo 1-0 kutwaa ubingwa na kitita cha 2m/- pamoja na kombe. vyombo vyote vya habari vilishiriki ambapo tsn ilikuwa ikishiriki kwa mara ya kwanza iliweka rekodi ya michuano hii ya kila mwaka kwa kuibenjua tvt bao 11-0 katika mechi ya ufunguzi na kutopoteza mchezo hata mmoja kati ya minne ilocheza

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. Wee Michuzi unashangilia timu za ndani unavaa jersey ya timu za ulaya mbona huna uzalendo?Mimi ni simba damu na zaidi ya hapo WAYA MKALI ya A.City

    ReplyDelete
  2. du ! siku nyingi zimepita, siagara pakekua na miti hivyo?! itabidi nije nitembelee washkaji .

    ReplyDelete
  3. Dr Dau wa NSSF haachi tuunazi wake wa kushabikia SIMBA
    kwani hizo jezi lazima ziwe NYEKUNDU?

    nssf acheni hizo

    ReplyDelete
  4. michuzi kumbe chamalenu linatisha yaani mliwatandika tvt bao 11.0 inamanisha hadi kipa wenu alifunga goli? kwamaana goli hizo ni idadi ya wachezaji.

    ReplyDelete
  5. Sasa wewe Unamlaumu Misupu Kuvaa Jezi Toufauti Hujui Kua Yeye Ni Kamati Ya Ufundi!! Vipi Misupu Tanga Au Sumbawanga Mikoba Hio???

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...