waziri wa habarti, utamaduni na michezo mh. muhhamed seif khatib akipokea kombe la hisani la jkm toka kwa keith masters rais wa tanzania youth sports charity organisation (tysco) ofisini kwake. kulia ni makamu wa rais wa tysco ulaya david palmer nyuma ya waziri ni mkurugenzi mkuu wa tysco allan kalinga shoto ni mratibu wa tysco vicent kinyange akifuatuwa na afisa mipango wa tysco victor mgoya. tayari yanga na simba wameshakubali kucheza na timu ya middlesex wanderers toka uingereza mwezi wa sita mwanzoni kwa mualiko wa tysco ambayo imeamua kufungua vituo 24 vya kuandaa vijana kucheza kabumbu nchi nzima pamoja na ungua na pemba. kombe hilo litashindaniwa kama charity shield ya fa na mapato yataenda kusaidia maendeleo ya soka la vijana nchini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. kombe jepesiiiiii

    ReplyDelete
  2. Kama mpango huu tutaushikilia kwa makini wabongo basi soka yetu itapanda sana, bongo kuna vipaji vya soka lakini huwa tunakumbuka kuvishikia vinapokuwa above miaka 25 hilo ni tatizo kwa kweli eheh

    ReplyDelete
  3. ah afadhali mmeturudishia umiseta .kila la kheri

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...