
hapana shaka umeshasikia kizaazaa cha taasisi isiyo ya kiserikali ya hakielimu pamoja na ujumbe wake mzito kuhusu bongo na wabongo, ila ulisahau kujiuliza ni nani anayetengeneza matangazo hayo ambayo yamegusa hisia hadi za serikali kwa ukali wake. basi kwa taarifa yako mbunifu ama prodyusa wa matangazo yote ya hakielimu ni huyu david kyungu niliegongana nae leo, mbongo alierejea nyumbani kufanya vitu vyake miaka minne ilopita baada ya kuishi ujeremani kwa takriban miaka 15. hivi sasa anaandaa jingo zingine zenye ujumbe mzito wa hakielimu na pcb. kaeni mkao wa kula kwani ameahidi maajabu makubwa zaidi...anapatikana www.matatizo.net ama matatizo@raha.com ama info@matatizo.net
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...