askari wa kikosi maalumu cha kuzuia ujambazi wakikusanya magamba ya risasi yalokutwa leo sehemu ya kurasini mivinjeni jijini dar baada ya greda linalofanya kazi ya upanuzi na ujenzi wa barabara ya kilwa rodi kuyafukua. polisi bado hawajatoa taarifa rasmi ya kukutwa kwa magamba hayo wala idadi yake na sababu ziliopelekea kuwepo kwake hapo mahali. ujenzi na upanuzi wa barabara hii ya urefu wa kilometa 11 na ushee na ambayo ikiisha itakuwa ya njia mbili kuanzia mbagala umezinduliwa majuzi na jk na inaghalimiwa na serikali ya japan

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. Michuzi kuna kamchezo hapo maana kuna matukio mengi sana yanafanyika na ushahidi unapotea i mean maganda yanaokotwa watu wanatamabaa na hayo maeneo ya Mivinjeni ndio kwao hao wanaokota maganda sasa watuambie yanawahusu ama?

    ReplyDelete
  2. Hii issue inanichekesha, mi nilidhani wameokota risasi kumbe maganda!!!, Hayo bwana kuna mtu aliyabeba kutoka maeneo wanayolengea Shabaha kama Kunduchi vile akidhani dili miaka hiyo, akaona uchafu akaya damp hapo sasa leo hii imekuwa uchunguzi, uchunguzi gani hapo hebu waendelee na uchunguzi wa kesi za wafungwa wasipoteze muda buree

    ReplyDelete
  3. Hawa wachunguzi njaa kweli. ndio maana kesi nyingi hazina ufumbuzi. Iweje risasi zinazoshukiwa ama kitu chochote cha mashaka kuokotwa kama njugu na mikono wazi bila kuwa na glove. Sasa utabainije alama za vidole za wahusika wakati askari kanzu wenyewe walishachafua na vijikono vyao!! Bongo kazi kweli!

    ReplyDelete
  4. Hizo sio risasi ni maganda ya risasi wanachofanya hao ni kuyazoa wakayatupe dampo ili jamaa waendelee na ujenzi wa bara bara

    ReplyDelete
  5. hapo kesi atambambikiziwa mlevi aletoka baa usiku kazidiwa kazima karibu hilo eneo mpaka kesho yake, au mtu yeyote tu mwenye ugomvi nao lazima apewe kesi uchunguzi umekamilika

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...