ni saa saba ya usiku na jamaa hapa ndio mwanzo wanafungua maduka. hiki ni kitongoji cha deira. naomba niwafahamishe kwamba dumila. kuna dubai na deria ambako ndiko kwa wenyeji. dubai ni kama mji mpya, uko kama feri na kigamboni, bahari katikati. kwa hiyo ukija huku lazima ujue unaenda deira ama dubai

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 8 mpaka sasa

  1. Michuzi,
    Asante kwa taarifa hizi za kuelimisha. Ebu jaribu kutafiti juu ya nishati. Wenzetu hao wanatumia nishati gani zaidi kwenye mapishi, maana kuna taarifa kuwa wanapenda sana kuchoma nyama kwa kutumia mkaa wetu, hivyo basi , kuwepo kwa biashara haramu ya mkaa kutoka pwani yetu hadi Dubai.
    Vinginevyo, miye nimetia timu Mzizima, Jiji la Lawama!

    ReplyDelete
  2. Mzee michuzi mpaka saa 7 usiku ulikuwa hujalala? Kunani?

    All in all, mzee wengine tumeshakuwa adicted na glob yako. Kwa hiyo ujue kila siku una deni kwetu, ingawa sisi hatuna cha kukulipa. Hapo Dumila kulala Gest kama zile za buguruni bei gani?

    OC-Sinza, DSM.

    ReplyDelete
  3. Michuzi unafanya kitu kikubwa sana ambacho sijui kama unafahamu unafanya au la kwakweli binafsi nafurahishwa sana sana sana sina tu cha kukulipa lakini mara nikifika tz nitakutafuta nikupe shukrani hizo kubwa ahsante.

    ReplyDelete
  4. saa 7 usiku gani michu mbona saa hapo ukutani inaonyesha ni 9:26 au saa imekosea ndugu ?

    ReplyDelete
  5. We Issa, usitufunge kamba bwana duh, au saa nayo inasomeka kiarabu?!. Mbona saa inaonyesha saa 3.25 hivi usiku.

    ReplyDelete
  6. Michuzi mi nina ombi moja naomba unijulishe visa ya Dubai ni bei gani ukiichukulia Dar,Halafu nataka kuagiza BIG SCREEN,Toka DUBAI Lakini hayo maduka naomba utupe web site zao kwani nataka kuorder online,Nitashukuru nijibu humu kwenye blog yako.

    ReplyDelete
  7. Michuzi ni msanii ukienda kichwa kichwa anakuingiza mjini..saa inasema saa tatu yeye anadai saa saba!!

    ReplyDelete
  8. UAE has 7 emirates,Dubai being one of it. Deira is the old part of Dubai and the other famous part is Bur Dubai.But you can not divide Dubai into Deira and Dubai its like saying Dar and Mwenge.There are places like Rashidya were a majority of people are of Zanzibar descent and Swahili is highly spoken although some pretend not to know it.I belive you must have had some lunch at The Zanzibar Restaurant when you were here.Deira is like the Manzese or Kariakoo (in business sense) of Dar and yes it is busy till the earlier morning hours.Places like Jumeirah,the marinas etc are high class residential areas(the masaki of Dar).
    If you do visit Dubai, send us an email at darresident@yahoo.com and we would sure you around and let you get intouch even with the locals who you did not meet as per your pictures. But keep up the good work we really appreciate your effort in uniting us.Ever thought running for a seat ;)
    Some sights and sound of Dubai
    http://www.thepalm.ae/
    http://www.burjdubai.com/
    http://www.theworld.ae/
    http://www.dubaiinternetcity.com/
    http://www.malloftheemirates.com/photoGallery.asp

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...