msanii ambwene yesaya a.k.a ay amerejea toka nairobi ambako alikwenda kufanya shoo. habari kutoka huko zinasema ay alitesa vilivyo na pia wasanii wa bongo sio tu wanakubalika bali pia wanaheshimika sana kwa watani wetu wa jadi kuliko nyumbani...msikilize ay kwa kubofya hapa

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 10 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 15, 2007

    Hello Pageant Fans!

    Pageant Almanac's Miss Universe 2007 Pageant Playoffs Top 20 has finally
    been chosen!

    In alphabetical order:
    Angola - Micaela Reis
    Brazil - Natália Guimarães
    Curacao - Naemi Monte
    Denmark - Zaklina Sojic
    Dominican Republic - Massiel Taveras
    Greece - Doukissa Nomikou
    India - Puja Gupta
    Italy - Valentina Massi
    Japan - Riyo Mori
    Korea - Honey Lee
    Mexico - Rosa Maria Ojeda Cuen
    Norway - Kirby Ann Basken
    Peru - Jimena Elias
    Philippines - Anna Theresa Licaros
    Russia - Tatiana Kotova
    South Africa - Megan Coleman
    Spain - Natalia Zabala Arroyo
    Tanzania - Flaviana Matata
    USA - Rachel Smith
    Venezuela - Ly Jonaitis

    Stay tuned for an email that will give you the chance to vote in Round 3
    of the Pageant Playoffs. Round 3 will cut the Top 20 to the Top 15.

    --- Pageant Almanac
    MICHUZI ILI UWEZE KUPIGA KURA LAZIMA UWE MEMBER WA ALMANAC.WADAU WABONGO INGIA KWENYE SITE NA JIANDIKIKISHE ILI UWE MWANACHANA HATIMAYE UPIGE KURA. WATANZANIA HIMA HIMA HIMA.

    SAMBAZA UJUMBE SI VIRUSI

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 15, 2007

    si unajua tena nabii hawiki nyumbani, au inawezekana huyu jamaa anatengeneza muziki kwa ajili ya soko la Kenya ndio maana anakubalika huko.

    Lakini mbona amevaa kishamba sana hapa?

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 15, 2007

    Usemalo ni kweli bwn Michu, sisi wabongo tunatabia ya kudharau chetu na kuthamini vya wengine. Jamani tujifunze kuthamini wasanii wetu!

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 15, 2007

    Watani wetu wa jadi na muziki wapi na wapi!? Nenda mahusiano usikilize vitu vilivyopangwa na kupangika. Hamna matusi bali nyimbo ambazo zinakupa msisimko mkubwa kila unapozisikiliza pamoja na kuwa nyingi ni za miaka 20, 30 au hata 40 iliyopita. Mie hao wasanii wapya hata hawanigusi kabisaaaa!!!. Kuna wachache wanaojitahidi (majina kapuni) lakini bado wana safari ndefu sana. Michu mbona umeminya maoni yangu kuhusu mkorogo? Acha hivyo!!!!

    Mchango wangu wa senti kumi huo

    ReplyDelete
  5. AnonymousMay 15, 2007

    Kamua mwana, ila sifa zisizidi uwezo na kipaji chako, ila nasikia uliwekwa selo Kenya baada ya kutompandisha Matonya jukwaani wakati umeshapokea hela, ni kweli?
    Kuwa makini, utapoteza mashabiki.
    Ni kweli umevaa kishamba, ukiwa kama model inatakiwa upangilie mavazi.

    ReplyDelete
  6. AnonymousMay 15, 2007

    Unajua wasanii wa kibongo wanatesa nchi jirani kwa sababu ya kuwepo kwingi wa vituo vya TV na radio station nchini Tanzania.Ukiwa na dishi na LNB poa TV station za bongo zinaonekana mpaka Gabarone, Botswana (at least TVT), na ITV, Star, EATV etc zote zinaonekana in east and central Afrika. Madishi na LNB nyingi hazishiki TV za nchi jirani(ingawa LNB yangu inashika a Mozambique channel)

    Kuna jamaa kaniambia Juba, southern Sudan, wanashika na vilevile Oman and/or somewhere in the Persian Gulf wanawapata fresh EATV

    Vilevile, kuwepo kwa recording studio nyingi in TZ pia kunasaidia sana wasanii wa kibongo wapendwe kwani wakwao wanakuja huku kurekodi.

    ReplyDelete
  7. AnonymousMay 15, 2007

    AY ni mwanamuziki makini sana, ila shida yake ni moja tu, kundi alilo nalo. Kundi la East Coast limejaa watu wasio makini, ndio maana hata nyimbo zao nyingi ni za majogambo na kuponda watu. Unafikiri kwa nini Mwana FA kajitoa? Kachoka! Nasikia hata AY yuko mbioni kujiengua katika kundi hilo.

    ReplyDelete
  8. AnonymousMay 15, 2007

    kaka michuzi muangalie dada yako nancy katika video ya mkali wa hiphop mtoni

    sio vibaya ukaipost mbele ili wa tz tujivunie nae

    http://www.youtube.com/watch?v=icyw2VuOAHs&mode=related&search=
    wazee wa Licoln, Uk

    ReplyDelete
  9. AnonymousMay 16, 2007

    Ni kweli wanamuziki wa bongo wanawika zaidi nje kama X plastaz kuna wabongo humu ambao hawawajui bt sikilizia wanavowika ughaibuni!! Ila nawapongeza wabongo kwa kuthamini vya wenyewe atleast kwa wakazi wa tmk wanaozimikia sana hip hop kuliko wakazi wengine wowote kati ya watu 10 9 wana tape za bongo fleva. nchi kama kenya duuuh inakuwa ngumu!! AY KIP IT UP!!!

    ReplyDelete
  10. AnonymousMay 16, 2007

    MICHUZI we need habari za hawa watu maana wamepotea sana:
    1.SYLVIA BAHAME
    2.MANDOJO na DOMOKAYA
    3.RAH P
    4.MWISHO MWAMPAMBA
    5.OTHMAN NJAIDI
    6.IRENE KIWIA
    7.LIL TK(TEDI KALONGA)
    alafu naskia eti loon alivokuja aliwashalawena sana TK na nacy sumari mpaka wakawa na bef ivi ni kweli au??tudodose.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...