mdau kaachwa na pantoni...

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 8 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 24, 2007

    HAYA MAMBO YA MTU NA PANTONI YASINGEKUWEPO KAMA SERIKALI INGEJIDHATITI NA KUJENGA DARAJA AMBALO LINGEVUSHA MAGARI NA WAPITAO KWA MIGUU.
    NASHANGAA (HARAMBEE)MCHANGO WA USHINDI WA TAIFA STARS ULIIBUKA NA ZAIDI YA SH.MILIONI 300 TENA KWA SIKU MOJA.
    KIVUKO KIMEANZA UKUSANYAJI WA HELA TANGU ENZI YA NYERERE HADI LEO NA HAKUNA DALILI YA KUTATUA TATIZO HILO.
    ILIBAKI NI WABUNGE KUJINEEMESHA NA MASHANGINGI NA MA-BENZ AU BMW YA KIFAHARI BADALA YA KUJALI WANANCHI WANAOWAPIGIA KURA.
    HIVI MAJUZI NILISIKIA KUNA BONGE LA UGOMVI NUSURA WATU WAFE KISA; WALIKUWA WANAGOMBEA USAIFIRI WA KUWAPELEKA MJINI KUTAFUTA MAISHA.
    LEO HII TUNAAMBIWA JK ATAFUTIWE HELIKOPTA ETI KUPUNGUZA MSONGAMANO WA MAGARI MJINI. ELIMU KWELI INA WAKWAO.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 24, 2007

    Maskini mtu wa watu... unaweza kukuta kuwa hiyo ilikuwa pantoni ya mwisho siku hiyo...

    Kweli kabisa anon wa 6:23:00 PM unayoyasema hapo juu ni ya maana. Wewe waache wanunue hilo helcopter... siombei itokee, lakini ninavyo yajua mimi,lita ishia tu kuua viongozi kwenye ajali, ndiyo watakapojua kuwa hayafai kabisa kama njia ya kupunguza msongangamano, hali wananchi wakiwa wanapeta kwa miguu au kupata karaha kwenye misongamano mabarabarani.

    SteveD.

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 24, 2007

    mchango wa kivuko ni jukumu la wananchi wa eneo husika, pale ndo mjini,matajiri kibao.
    Michango ya Taifa Stars inatolewa wapenda michezo popote walipo.

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 25, 2007

    serikali imejaa wajinga tuu na wala rushwa....yaani usumbufu wote wanaopata wa foleni wangeweza kupunguza hiyo load kwa kujenga daraja la kigamboni ,lakini wanachofikiria ni kusaidia mtu mmoja kwa kununua helicopter mbovu ...rushwa na ujinga vikichanganyika basi mnachopata ni hard life,poleni sana

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 25, 2007

    Wewe mbwegelembwegele,
    Barabara unayotumia umejenga kwa hela yako? Serikali inakusanya kodi kutoka kwa raia na ikikopa na kukujengea barabara ni watanzania wote wanalipa. Iweje useme daraja la kigamboni lijengwe na wanakigamboni?! na je watakotumia lakini hawakai kigamboni walipishwe hela? Ukweli ni kwamba hapo pangejengwa daraja zuri kungeweza hata kukuza uchumi. Kigamboni ingejengwa saana maana ni karibu na mji na watu hata wangeweka kwenye biashara ya kucruise huku wakiangalia view ya pande zote mbili (kigamboni na mjini). Serikali inatakiwa ilishughulikie swala la daraja sasa kigamboni.

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 25, 2007

    Jamani anatia huruma sasa tuseme anavyoikimbilia ndio ataifikia au. makubwa.It's realy sad. Pole sana kaka yangu ndio maisha hayo

    ReplyDelete
  7. AnonymousJune 25, 2007

    kwa kweli nakubaliana kabisa kwa yale yaliyosemwa juu hasa kwa serikali kuwekea umaanani swala la maendeleo ya wananchi na sio vigogo peke yao. Kwa nini hatuigi nchi tu jirani hapo RWANDA hakuna Rushwa moja mbili rais wao alipiga bei mashangingi yote na sasa wanatumia magari ya kawaida tu mpaka ubalozi wao uliopo hapa wanatumia tu Baloon ya kawaida mno na maendeleo yanaendelea kupatikana tena kwa kasi ya ajabu sasa hivi hata thamani ya pesa yao ipo juu kuliko hata sisi na uchumi haoooo wanasonga mbele na wanapenda maendeleo sisi tunachojua ni kusafiri kushinda kwenye ndege kama ma air hostess bwana na pia kufanya matumizi tu ya ajabu bunge letu mawaziri balaza kubwa saa ngapi tutasave hiyo shilingi tutengeneze hizo barabara kwa kweli inabidi tubadilike natamani kama michuzi haya maoni unge print siku moja ukawapelekea hao wakubwa kwa sababu sidhani kama wanapata hiyo fursa ya kuyasoma.. wamekalia kujineemesha wao kwa ufupi viongozi wetu ni ma selfish wanataka wafaidike wao tu hata ukitoa wazo la kitu chenye manufaa kwa nchi wakigundua hakitawanufaisha mifuko yao moja kwa moja wapo radhi hicho kitu kisifanyike hapa nchini wanakasirisha kwa kweli. tubadilike jamani tukianza na viongozi wakuu.
    NAWAKILISHA

    ReplyDelete
  8. AnonymousJune 25, 2007

    Michuzi mbona unaingiza watu machaka?? Yaani kuna wengine wameamini kuwa kweli huyo jamaa anafukuzia pantoni !!! Jamani tuwe siriasi huyo jamaa anafanya kitu kingine tu hapo, michuzi kawachomekea tu

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...