salamu za shukrani toka makunduchi zimeingia sasa hivi

Bwana Michuzi,


Tunakushukuru kwa jitihada zako za kuwaelimisha Watanzania wenzetu. Kujitokeza kwa wadau wengi kutoa maoni yao juu ya ule mjadala wa 'amarula, na ndovu ni dalili kuwa ujumbe wetu umefika. Tunawashukuru Watanzania wote waliotoa maoni yao. Hii ni dalili njema ya kupevuka kwa demokrasia nchini. Hatuna nia ya kuanzisha mjadala mwengine lakini tunategemea Watanzania walio wengi watakuwa pamoja nasi. Mwisho tunawakaribisha Watanzania wote katika Sherehe yetu ya jadi ya kusherehekea 'Mwaka Kogwa' yaani mwaka mpya wa kiswahili huko Makunduchi itakayofanyika mwezi wa Julai 22.


Mwenye kutaka habari zaidi kuhusu mwakakogwa afungue mtandao wetu wa kijiji http://www.mzuri-kaja.or.tz/
Ahsante sana

Muombwa

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 11 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 20, 2007

    Watu wa Makunduchi siwawezi .... kumbe longo longo lote lile ilkuwa ni "Nitoke vipi?"

    Haya bwana mmeshapata "attention" yetu.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 20, 2007

    Tunaogopa kuja huko: POPOBAWA!!

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 20, 2007

    Waungwana umefika wakati wa kuziacha mila nyengine zisizo na value added kwa jamii .hayo mambo ya mwaka kogwa kwa kweli si mazuri kwa kipindi hichi kilichoshamiri hili janga la ukimwi, kwani nikichocheo kikubwa cha maambukizi ya ukimwi.kwa kweli watu hufurika kufanya ufuska tu.ukimwai utatumaliza tukiendelea kukumbatia mila potofu.

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 20, 2007

    sijabahatika kufika kisiwa cha pemba,sijui hapo makunduchi au mwanakwereke ndo mjini kabisa? au nje ya mji,
    hongereni kwa mwaka mpya wa kiswahili,japo sijaelewa mnamaanisha nini?na hepi bethdei zenu zinafata mwaka huo? au?
    Kamtu-Chui/Paris

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 20, 2007

    hahahhah! Haya tena Muombwa kaja na mamabo ya mzuri kajaaaaa huyu jamaa kweli kibokoo pwanii full maneno yake yantia wlakini wadau tusijekuwa tumeingiliwa na popo bawa kweny blog yetu Michuzi angalia hii mammbo.

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 20, 2007

    Web yenu kaandaa mzungu "The local traditional medicine man call it "Mkuu hapingwa", literally meaning "the leader is not opposed"" au HAPINGWA ndo HAPINGWI kwa ki makundu chi

    ReplyDelete
  7. AnonymousJune 20, 2007

    DUH..MICHUZI HUYO JAMAA ALIYEKUPA PICHA AMENIKUMBUSHA MBALI SAANA.
    HUU NDIYO MBUYU NILIYOCHEZWA NGOMA YANGU YA JANDO BAADA YA KUTAHIRIWA.
    HIVI BADO UPO MPAKA LEO. MIAKA AROBAINI SASA SIJAFIKA ZENJI LAKINI HAPA SIJAPASAHAU KWANI NILIKUWA NIKIPITA KILA SIKU. BRAVOOOOOO JAMAAAA

    ReplyDelete
  8. AnonymousJune 20, 2007

    Vipi mzee msosi, na wewe unafika huko makundu uchi?

    ReplyDelete
  9. AnonymousJune 20, 2007

    Michuzi hii website ya mzuri kaja...Nimeipeda sana!!! Ina touch maisha ya mwananchi wa kawaida!

    Best,

    ReplyDelete
  10. AnonymousJune 21, 2007

    Gina la village linafurahi "Mzuri kaja"
    Culture celebration yao iko so rich nafikiri hizi ndio sehemu bali Tanzania still zina keep original traditions.

    ReplyDelete
  11. AnonymousJune 21, 2007

    nakupitisha michuzi, hizi culture ni muhimu kutunzwa. Huwa nafikiria kwa nini Ukanda wa Pwani usijaribu kutunza traditional swahili. Kuna weza kuwa na Traditional swahili na modern swahili kama ilivyo ktk Chinese. Sijui kwa nini sisi hatuna hamu ya kuhifadhi historia yetu, wakenya wataendelea kudai kiswahili kimeazia kwao kwa vili sisi hatuthamini hata historia na utamaduni watu.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...