Mpira ulianza taratiib kila timu ikijaribu kusomamchezo wa mwenzake. Walikuwa DC ndio waliotangulia kupata bao mbili za haraka haraka.
Kabla ya mapumziko vijana wa ATL walifanikiwa kuchomoa goli moja. DC ikiundwa na vijana wadogo ambao ni hazina yaTaifa hapo baadae waliipeleka puta ATL timu iliyoundwa na wakongwe mbali mbali ambao waliwahi kuwika huko nyumbani.
Habari tulizopokea muda si mrefuzimethibitisha kuwa Jumapili ijayo Vijana wa kwa baba Moi "Harambee Stars watapambana na timu kabambe ya TANZATL jijini Atlanta. Pambano ambalo limekuwa gumzo kubwa katika kilakona ya Wabongo na Wakenya hapa ATL.
Kuhusu mapicha na matokeo please stay tuned!
Juu ni timu ya Wabongo DC (blue) na ATL (yellow).


Na mwandishi Mark!

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 11 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 20, 2007

    What i don't understand is how this ATL kid get time do this. Few weeks ago i heard they were in houston, now DC... Goodluck guy, i hope no eviction notce will be awarded to neither of the player

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 20, 2007

    michezo hudumisha undugu na urafiki katika jamii yoyote, na hii ni kawaida yetu Watza bado mnaonesha moyo huohuo wa kirafiki hata mkiwa ugeneni kwa kuonesha ushirikiano. big up sana, ombi langu tu jezi zinazotumika naomba zioneshe uzalendo na Utanzania halisi kwa kuandikwa TANZANIA hata kama kiwango chetu cha soka kiko chini lakini hata wasioijua Tza kimchezo watajua na sisi watanzania huu mchezo hatuko nyuma, na ndipo mtakapo pata mechi nyingi zaidi za mialiko mbalimbali: mechi njema ila mturushie mapema matokeo ya mechi hiyo.

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 20, 2007

    Sasa Hio Timu Ya Juu Inaimbiwa Nyimbo Ya Taifa Lipi Ona Walivokakamaa...Punguzeni Vitambi

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 20, 2007

    Hao waliovaa blue kipa wao(jezi nyeusi) ni DJ wa zamani Luke Joe wa DSM? maana ni siku nyingi Luke Joe alikuwa kipa wetu O'bay watoto wa kaole Masaki DSM.

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 20, 2007

    Wahusika muwe mnatoa majina ya safu nzima ya wachezaji, ingependeza zaidi

    ReplyDelete
  6. AnonymousJuly 20, 2007

    ""Anonymous said...
    What i don't understand is how this ATL kid get time do this. Few weeks ago i heard they were in houston, now DC... Goodluck guy, i hope no eviction notce will be awarded to neither of the player""

    WEWE NDIO HUNA AKILI KABISA. NO SUBSTANCE IN YOUR TALK AT ALL. I FEEL SORRY FOR PEOPLE LIKE YOU.

    ReplyDelete
  7. AnonymousJuly 20, 2007

    Ni jambo zuri sana lakini hizi timu kwenye state yangu zimewafanya watu kadhaa ndoa zao zimekuwa mushikeni au zimeharibika.

    Wengi wa wachezaji wa timu yetu wakijisahau na kufanya mazoezi sana na kusahau kusaidia nyumbani. Wakitoka kazini moja kwa moja kwenye mazoezi. Wamesahau huku hamna msaidizi wa nyumbani. Mke ndio atoke kazini, akachukue watoto kwa day care, aje a make sure watoto wamekula. Ikawa hivyo kila siku mwanamke mmoja namfahamu alisurrender sas hivi wameachana na huyo jamaa.

    Nawaomba na nyie msije mkasahau kusaidia familia zenu kwa ushabiki wa mpira.

    ReplyDelete
  8. AnonymousJuly 20, 2007

    watu wengine hata hawajui wanataka kusema nini. Untasemaje wamekakamaa kisha wawe wana vitambi.
    Vitambi na ukakamavu wapi na wapi ?????

    ReplyDelete
  9. AnonymousJuly 23, 2007

    WATU WAMEMKANDIA SANA YULE MZAIRE ALIYEJITISHWA NGUO ZA BENDERA YA UK NA US.
    LAKINI HAO HAO WABONGO NDIYO TUNAOWAONA HAPA WAKIVALIA JEZI ZENYE JINA LA BRAZIL. DUH KWELI NYANI HAONI KUNDULEEEEE.

    ReplyDelete
  10. AnonymousJuly 23, 2007

    Sponsor wa safari yao labda ni kutoka brazil yule sponsor wake ni US au UK I doubt. Kupand a private jet lazima inakuja na masharti yake

    ReplyDelete
  11. AnonymousJuly 24, 2007

    Jamaa minaona ni wazalendo tosha kwani hiyo staili ya kuweka mikono kifuani yote ni kujaribu kuziba neno brazil. Tuwape pongezi kidogo jamani!! Pwa! Pwa! Pwa!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...