jengo la justice kahwa lugakingira ambalo lina ofisi za haki za binaadamu na msaada wa sheria ni mojawapo ya majengo yanayovutia sana dar. lipo nyuma ya jengo la sayansi na teknolojia kijitonyama maji machafu

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 14, 2007

    Hapa pananoga sasa Michuzi, huyu jaji Rugakingira alikuwa haangalii sura. Maamuzi yake yalikuwa makini. Sikijua kama walimuenzi kwa kumpa memorial "institute". Nakumbuka wakati ule akitumia gari J2 kule Mwanza. Watoto wake nao pia wana akili, kina Kaitaba. Aliamua Mtikila awe mgombea huria bila chama cha siasa huyu jaji. RIP (nilisikia hivyo, i am not sure, mtanisamehe kama haikuwa vile)

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 15, 2007

    ni kweli baba wa watu amefarki,RIP.nasikia aliwahi kumlamba mvua tano nduguye wa karibu kisha jioni yake na yeye akaenda kwenye kikao cha ukoo kuungana kwenye masikitiko,yeye alikuwa anaangalia sheria tu,period.

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 16, 2007

    Jengo ni zuri sana, tunaomba short history ya huyu baba, na uchapa kazi wake kwani tulishaangaa kuona jina hilo tuelezeni kidogo habari zake. gwantusa

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 16, 2007

    Hivi huyo Marehemu Jaji hilo ni jumba lake binafsi au limepewa tu jina hilo kwa kumuenzi?
    Naomba hilo jibu kwanza, halafu ndo nitoe koments zangu.
    Nawasilisha

    ReplyDelete
  5. Anon wa July 16, 2007 12:20:00 PM EAT ni hivi; Jaji Kahwa Lugakingira likuwa ni jaji wa mahakamu kuu ya Tanzania na enzi za uhai wake alikuwa ni mwanaharakati bora akbisa wa haki za binadamu nchini Tanzania. Hilo jengo si jengo lake binafsi na wala hana hisa ya kipesa kwenye jengo hilo isipokuwa Kituo cha Sheria Haki sa Binadamu ambao ndio wamiliki wa jengo hilo wametumia jina la Marehemu jaji Kahwa Lugakingira ili kumuenzi yeye binafsi kutokana na mchango wake katika eneo la hki za binadamu nchini Tanzania.

    Hilo jengo ndio makao makuu ya Kituo cha Sheria na Haki Za Binadamu ambapo kituo hicho kina ofisi nyingine mkoani Dar es Salaam, Kituo cha Msaada wa sehria Magomeni na Kituo cha Msaada wa Sheria Buguruni na pia kuna fisi nyingine ambayo ipo mkoani Arusha.

    Wasslaam

    Volunteer - LHRC
    Kituo cha Msaada wa Sheria Magomeni

    ReplyDelete
  6. AnonymousJuly 17, 2007

    Nashukuru kaka "Kaka Pori" kwa kunielewesha. Basi kama sio jengo lake binafsi, basi sina koments

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...