mdau anatutambulisha kitabu chake kipya cha 'watanzania kuelekea kwenye nchi ya ahadi - Tanzaniana to the Promised Land' ambacho kinachambua uongozi wa siasa wa bongo kwa awamu zote tatu zilizopita, na kinatathmini pia kasi mpya, nguvu mpya, na ari mpya ya awamu ya nne. ukitaka nakala kutoka 'TANZANIA PUBLISHING HOUSE" kwa wale walio hapa nchini au wale walioko nje ya nchi kupitia www.lulu.com/ijwerrema au watembelee http://www.ijwerrema.info/ ama tuma email kwa mwandishi author@ijwerrema.info

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 14 mpaka sasa

  1. Ni hatua nzuri, manaake vitabu vipya Tanzania vimepungua sana. Siku hizi waandishi sijui wamechoka? Najua najua wengi watasema kuwa hakuna soko, lakini mwandishi mzuri anatakiwa kufanya utafiti kwanza soko linapenda mambo gani then aandike kuhusu hayo mambo. na internet adevrtising kwa Tanzania bado uwanja ni mpana sana saaana. Kwa kuwa Wabongo wengi hawana credit cards yaani bado hawajajikita kabisa katika internet advertising

    ReplyDelete
  2. ana nini jipya humo,au ndo usual bla bla tu ?

    ReplyDelete
  3. TANZANIA TO THE PROMISED LAND? man not in a million years!

    ReplyDelete
  4. To the promised land ! my a--e!!!!

    ReplyDelete
  5. Ah mijitu mingine bwana eti,"To the promised land ! my a--e!!!!".

    Yaani miwazo hasi tu na chuki zisizo na msingi. Yaani hata sijui nani kafanya makosa kukupa computer. Mtu kama wewe inatakiwa ufungiwe stoo uwe unabeba maboksi maisha yako yote.

    ReplyDelete
  6. Kazi njema hii ingawa wanasema tusihukumu kitabu kwa kusoma mai hedingi au mai kava yake.

    Nyakatakule

    ReplyDelete
  7. SIYO (AHADI) NI MATARAJIO.. KENYA NA UGANDA WATATUCHEKA...WATATULETEA HATA WAKARIMANI.samahani sawahili yangu mbofumbofu.

    ReplyDelete
  8. Hongera Ndugu Mwandishi JAPO SIKUJUI NA WALA SIJASOMA HICHI KITABU LAKINI NI HATUA NZURI

    ReplyDelete
  9. Mimi nilibahatika kupata kopi ya kitabu hiki hapo TPH. Kwa kweli mtunzi amejitahidi sana kutoa mawazo yake kwa uwazi na bila woga. Anaonekana sio ana mtazamo tofauti kidogo.

    DOLE MTUNZI

    ReplyDelete
  10. Nyie wote wenye kulaumu, tuonyesheni vitabu vyenu mlivyoandika!

    Kazi kulaumu tu na hali hamuwezi hata kuandika kurasa kumi zikasomeka!

    Ni heri zaidi mkaenda maktaba, kama hicho kitabu kimeishawekwa, mkisome vizuri na kutuandikia, angalau, "review" yake!

    Kumbukeni, na liwajae akilini mwenu: One Tanzania, many voices!
    Sio lazima Tanzania yetu ipimwe na mawazo yenu tu, ambayo pengine mkiyaandika yasomwe na wengine, watayakuta ni pumba tupu!

    Yaelekea mwandishi anawaona Watanzania wanavyopiga hatua kufikia "promised land". Sisi amabo hatujakisoma kitabu hicho hatujui mwandishi katamati namna gani!

    Hata kama kitabu hicho kimeandikwa "one-sided" kupendelea uongozi wa CCM, kisomeni mkikosoe kwa kutoa upnde wenu manaofikiria kutufikisha kwenye "promised land"!

    ReplyDelete
  11. hii tittle mimi wala haijanipendeza. Anafanya kumdhalilisha baba yetu wa taifa mwl Nyerere. Yaani ina maana the more we have new leaders the more we are walking towards the promised land. Kama sio kinyume chake?

    ReplyDelete
  12. Mimi naomba tu kumuuliza Michuzi kama tunaweza kupata japo uchambuzi tu wa sehemu ya kitabu hiki. Maana watu wanasema tu bila hata kujua kitabu kinasema nini. Lakini inaelekea kuna amabao wameishakipata kama mtoa maoni mmoja hapo juu ambaye yeye anasema anavutiwa na mwandishi.

    ReplyDelete
  13. Jamani mbona, hizo rangi za bendera zimekosewa?? Au kipo apsaididauni!!

    ReplyDelete
  14. JAMANI HIYO BENDERA MBONA IKO APSAIDIDAUNI?? AU NDIO YALIYOMO HUMO NDANI FEST IMPRESHENI MUHIMU.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...