
Hi Uncle Michuzi,
Shikamoo,
Mimi mdau wako Faith Octavian Barnabas leo ndio nimetimiza mwaka mmoja toka nizaliwe, mdingi kanifanyia birthday ya kiushkaji na rafiki zangu, tumefurahi sana. Nakupongeza kwa kuifanya Blog hii hata sisi watoto iwe yetuuuu!Usinibanie, weka hiyo picha yangu.
Faith Oc, Sinza-Dsm
Asante sana kwa salamu nami nakuimbia Hepi Besdei Tu Yuuuuuu na kukutakia maisha mema na marefu. Mwambie dedi kwamba nondozzz muhimu huko mbeleni hivyo asifanye ajizi kukupeleka skuli bab'kubwa uzibebe. Ila nalalamika kwa kuninyima mwaliko wa kupata biskuti hizo na bila shaka na keki... acha hizo Faith!
Michuzi
happy birthday Faith, umependeza kweli baby,kila la heri mimi ni wajina wako eheee. mwaaa! mwaaa!
ReplyDeleteAwww what a cutie. Happy 1st birthday babygirl. N I hope u live to see 100 more ( I noe she only one but hey!). She is a cutie one.
ReplyDeletehappy birthday cutie Faith and God bless you. Sie tunajaribu kupigania haki taifa la kesho msiteseke kama sie wazazi wenu.
ReplyDeleteHappy bday Faith
ReplyDeletelkn wewe upo kwenye mbolea Faith,so huwakilishi hata kidogo asilimia 99 ya watoto wa tz ambao hata kunywa soda kwao ni jambo la anasa
wewe umefanyiwa party,umekula keki na wazazi wako wanaonyesha wanakupenda wewe kama inavyostahili
Kua uyaone mrembo Faith,kuna wenzako kwa umri kama huu wako,wazazi wao wamekwisha sahahu hata walizaliwa lini kwa sababu ya taabu za kuwalea,wakati wewe unafanyiwa party,mtoto kama wewe kijijini Kashozi kadumaa kwa kukosa lishe bora dada Faith!
Bytheway,hongera sana faith na mungu akupe maisha marefu,wewe huna kosa na hukuomba uzaliwe sehemu ya"mbolea",ilaumiwe system mbovu ya tz
Happy birthday Faith! Nimefurahi sana kukuona jinsi ulivyokua na umependeza sana, Mungu akutangulie katika maisha yako.
ReplyDeleteEhh Faith, happy birthday Faith! Nimefurahi kusikia umetimiza mwaka mmoja, nakutakia maisha mema katika ukuaji wako na mungu akubariki.OC, anza maandalizi ya Elimu kwa mwanao, asome kama ww ulivyosoma na tena iwe zaidi yako.Michu usinibanie
ReplyDeletewee bibi wa Uk, yaani umekua bibi bado unabeba mabox tuu, rudi bongo ulee mjukuu,any way, happy birthday Faith.
ReplyDeleteweeeeeee Anonymous wa November 20, 2007 2:10:00 AM EAT, unafikiri kila mtu akikaa huku ughaibuni ni kubeba box, inaonekana una mapungufu kwenye kichwa chako, kwa sababu hujui na hutakaa hujue kamwe.
ReplyDelete