mwanamke hina, babu... au vipi wadau?

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 19 mpaka sasa

  1. Uchafu mtupu

    ReplyDelete
  2. Tatoo(Temporary) za kikwetu.halafu mnasema kila kitu kinaanzia ughaibuni.

    ReplyDelete
  3. Unayesema hina uchafu mtupu, kweli hujui maana ya hina. Kabla hujaikandia na kuisagia uliza ueleweshwe, na ukishaipata hiyo sidhani kama utathubutu tena kusema uchafu mtupu.

    Wewe mtu wa bara eeeh! Basi tena hiyo bara ni bara kweli kweli, manake zamani hina ilikuwa kwa waswahili wa pwani na waswahili wa bara. Lakini siku hizi hina watu wameshaijua maana yake na utamu wake kila mtu anapaka.
    Zamani hina ilikuwa kwa maharusi n wa kiswahili au wakiislam lakini siku hizi hata bi harusi ambao sio waislam wanapaka na wanapendeza.
    Hina haina dini kusema ni ya waislam au si ya waislam inaendana na utamaduni wa kiafrika. Watu wakisikia hina wanaihusisha moja kwa moja na pwani, lakini hina inapakwa nchi nyingi za kiafrika na kiarabu na Asia hasa huko uhindini ndio imeota mizizi.
    Kwa uchache ukienda Sudan, Somalia, Kenya, Ethiopia, Eritrea, Mali, Senegal, Gambia, huko utaikuta hina.Hiyo ni kwa uchache tu.

    Labda kwa kukumegea tu zamani nilipokuwa mdogo (enzi hizoo miaka ya 70)nilikuwa nakatazwa na bibi na mama yangu kupaka hina ya mapambo, yaani hina niliyokuwa naruhusiwa kupaka ni ile ya kusiliba mkono na miguu yote bila kuweka maua. Bibi yangu aliniambia hina ya mapambo ina wakati wake, na hapa pia sio mahala pake kukwambia maana yake.

    Ukiondoa hayo mambo ya mapambo, hina pia inatumika kama dawa, wanaofanya shughuli za salon wanajua kazi ya hina kama dawa ya nywele. Vile vile wapo wanoitumia kama dawa ya miguu (sio hiyo piko ni hina yenyewe.

    Kwa kifupi tu usidharau tamaduni za wenzio kwa sababu hujui maana yake uliza uambiwe. Nitafute nikupe maana ya hina halafu kama utarudia tena kusema uchafu mtupu!

    Mswahili.

    ReplyDelete
  4. YUK........

    ReplyDelete
  5. HINA IMETULIA ,SIO UCHAFU KAMA JAMAA ANAVYOPAKA HAPO JUU ISHU NI KWAMBA DEMU HANA MGUU ULIOTULIA YAANI WA CHUPA YA BIA MGUU UMENYOOKA KAMA MLINGOTI DUUUUUUUU!

    ReplyDelete
  6. MICHUZI HUYO NI MY WIFE WAKO ISHA KALILI MIGUU.

    ReplyDelete
  7. Mambo ya pwani hayo...kwa sisi tunaojua raha yake wacha tucongee!!! dah..nimemic nyumbani kinoma...

    ReplyDelete
  8. Huu ni ujinga tu wa kuiga waarabu. Kuna uzuri gani mtu kupaka uchafu mwilini wakati unaenda kuolewa? Yaani uvae vizuri kisha unajipaka miuchafu mwilini, kuna furaha gani hapa?

    ReplyDelete
  9. kwa kweli michu kwa mimi naona uchafu mtupu!sijui labda huyu kapaka vibaya au na hilo ligagulo halijampendeza ila imeonekana kichefchef tu!

    ReplyDelete
  10. Michuzi,
    asiyefahamu uzuri na utamu wa hina na mikato yake ataona uchafu ila mweleze kuwa uchafu kwake harufu ya shombo na siyo samaki mwenyewe.
    Hina uipate ilee ya mkato wa lamu na mama mwajuma siyo mary akupake utaona sifa zavyomiminika tele.
    Mdau North Carolina.USA

    ReplyDelete
  11. Dah mimi nilifikiri vidonda vya kuungua!(1st degree burn) Dah! thats too much

    ReplyDelete
  12. Waswahili bwana kwa kudharau vyao, ingekuwa mzungu na matatoo hapo ungesikia wanavyoyasifia lakini kwa kuwa ni hina basi uchafu.

    Wazungu wenyewe wakifika Zenji wanapaka hina ya kwenda kuonesha kwao siku wanapoondoka, nyie mwaona uchafu eeh!!

    EMANCIPATE YOURSELVES FROM MENTAL SLAVERY NONE BUT YOURSELVES CAN FREE YOUR MIND!(Bob Marley sio mimi niliyesema msinile nyama bure!)

    Michuzi lete picha ya mzungu hapa kapaka hina au tatoo upate kuona mambo!!!!!!

    ReplyDelete
  13. Nyinyi mnaosema uchafu, vipi kuhusu wamasai ambao wanajipaka sijui tope au mavi ya ng'ombe na wanakuwa na harufu sio nzuri, lakini mnafagilia kuwa ndio utamaduni wa mwafrika na mnajivunia, kwa kuwaonyesha kila kona duniani. Lakini waungwana wa pwani wakifurahikia utamaduni wao, watu wapuuzi ni kukandia tuu.

    I smell some bias among Tanzanians, whenever an issue involves Muslims or Islam, I can tell by negative comments posted.

    Hey, if we still prefer peace let respect each other.

    I'm out.
    Mdau.

    ReplyDelete
  14. Nyie mnaotoa comment oza-oza ngoja niwaulize...kwa akili yenu nyie mnaweza kupaka mavi na matope mwilini kwenda kutafuta kazi? Hayo ni masuala ya wamasai huko kwao vijijini na ndio maana hata wale wanaofanya kazi mijini hawaendi kazini huku wamejipaka mavi na matope mwilini kwani si jadi yetu watz na si asili yetu pia, ila for the maasai's that's normal. Mind you, hii sio mila ya waafrika, wamasai ni kabila na hali-represent the whole afrika, mpo hapo?

    Kwa mzungu kupaka hina zenji si ajabu, kwani mzungu ni mtu anayependa ku-try vitu vya ajabu ambavyo pengine wewe, mimi, hata pia Michuzi hawezi kujaribu kufanya, mfano kufanya mapenzi masikioni (kwenye tundu la sikio). Ila kwa kuwa kajaribu kitu kama hicho yeye mzugu anaona ujiko na kujitambia kwa wenziwe, na watamshupalia.

    Mzungu ataenda kuishi na wabarbeigi na atakaa uchi nao, wewe utaweza? Hivyo acha kutumia mzungu katika mfano huu, hina ni uchafu na ujinga mtupu ni sawa tu na tatoo...Tatoo ina uzuri gani mwilini?

    ReplyDelete
  15. Ushamba ndio unaokufanya uone tamaduni za wengine ni uchafu, kwani wanaopaka hina ni waafrika pia hata kama hawatoki Tanzania sababu Tanzania siyo inayocover Africa peke yake. Sie kwenu hina hatujaiga utamaduni wa mtu ipo watu wanapanda na kupaka. Ni sawa na wabantu wengine kupaka mdaa mdomoni au kupaka zingifuli kama unaijua na kujipamba kwa maua.

    Hapo hakuna kuiga tamaduni ya mtu.
    Mzarau kwao mtumwa wahenga walishasema. Unaona hina uchafu lakini lipstick yenye lead unaona ni safi!!

    Acheni hizo amkeni kumekucha ukijidharau na watu watakudharau, lakini sishangai ustaarabu ulianzia pwani!!

    ReplyDelete
  16. wewe anon nov 27 5:01 am ea
    koma kabisa
    nani kakuambia wamasai wanapaka mavi mwilini?
    watu wengine bwana if your not sure keep your mouth shut.
    mfyoooo ( yes nakufyonza )
    do something !!!!
    shika adabu yako
    wamasai hawapaki hivyo vitu - being one of them I know better.

    ni mimi,
    mmasai namba 1 duniani

    ReplyDelete
  17. Hina ni sawa na kujichonga matatoo mwilini siku unayokwenda kuolewa, in short ni uchafu. Binafsi nilimkataza mke wangu na wapambe wake wasije na matatoo ya kiafrika (hina) kwenye harusi yetu. Hina haileti uzuri wowote kwa mwanamke bali kujichafua tu mwili.

    ReplyDelete
  18. ANON 28,NOV 11:58 Ehee shekhee na ugomvi umooo? eeeh! mbona wenzio washashi, wehehe hutulizana tuu wanapoletewa vijimambo kama hivyooo, ohooo!tempaa tempaa. madongo kuliko hayo tunampiga bro michu na kumchanganya na my wife wake wala hajacharuka hata siku moja kwani ye hana nyongo? tujifunze kwa big nchi yetu watani wapo au....? we mmasai bwana luga mbofumbofu m-badooo!

    ReplyDelete
  19. wanaosema hina uchagu mtupu ni washamba, wewe una usafi gani hapo ulipo kama si kujishaua. get life woman!!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...