hapa ngoja nimwage ung'eng'e labda nitaeleweka. mai dog! hivi ze pipo of mipango miji ofu dar iz wea jamanizzzz...

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. suala zima sio mipango miji, hii ni sera mbaya ya chama cha mapinduzi. wataalamu wapo lakini hawapewi nafasi ya kuonyesha utaalamu wao. hatuwezi kusema UCLAS haitoi wataalamu. hiyo itakuwa siyo sahihi. nadhani hao wazee ni muda wao kuachia ngazi. wataka kumaintain status quo. hakuna analolifanya lakini hataki kuachia ngazi.

    halimashauri za miji zenye majukumu hayo zimelala. badala ya kufanya kazi wao wanajiingiza kwenye siasa. hapo undhani kuna kitu kitakachofanyika. angalia miji yote, ni kichekesho. bado nashangaa madaraka waliyopewa madiwani, wakati tunajua kabisa kuwa hawana uwezo kielimu. hao hao ukileta programe za kupanga mji wanagoma kwa sababu ya ueelewa mdogo. nadhani huu ni muda muafaka wa kubadili policy.

    tatizo si wataalamu, ni siasa ambayo imeingia kila pahala

    ReplyDelete
  2. Michuzi huna lolote. Nimekustukia.
    Swali hili kwani si ulishatuuliza jana!?!
    Nia yako ni kutuonyesha tu kuwa na we ulipanda ndege kwenda Zenji na sio Boti.
    Haya, tumeshakufaham. Hongera!

    ReplyDelete
  3. dawa yao ni kuwageuza ngazi then wote tunawapanda halafu kwa jeuri hatushuki mwezi mzima!

    ReplyDelete
  4. wewe anoy wa kwanza kabisa nakupa five kabisa bila hata ya kukufichia hata kidole kimoja!hiki chama kimechoka kabisa jaribu hata kuangalia upembuzi yakinifu wa uchaguzi wao uliokwisha alioutoa Prof Harub Othaman ya kwamba hakuna jipya pale kwenye ule uchaguzi ni sawa na kuweka mvinyo mpya kwenye chupa ya zamani!Hawa Madiwani ni chanzo cha kuzorota kwa hizi halmashauri za miji,wapo pale kwa ajili ya kujipendekeza kwa watu flani flani tu na kusubiria posho za vikao.
    Tusipokuwa makini 2030 hii nchi haitakuwa na mji hata mmoja wentye mpangilio wa kimiji.Ebu jaribu kuangalia hata Dar ambako ndo uso wa nchi hakuna hata utaratibu wa kipi tufanyie wapi na kile tufanyie huku.Ebu angalia Ubungo bus terminal nje kulivyo jaa biashara za ajabu ajabu alafu wale watu hata vyoo pale nje hawana matokeo yake mifereji pale imejaa vinyesi na harufu za mikojo.Mtu anaanza kujenga nyuma mbele ya choo cha jirani kule Manzese,Mburahati na sehemu nyingi tu hakuana anaekata asifanye hivyo!Angalia pale Bonde la Jangwani tunajua fika maji hujaa pale kila mwaka lakini kuna nyumba zimejengwa watu wanaishi ama kweli MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA AU NDO BORA MAISHA KWA KILA MTANZANIA?

    ReplyDelete
  5. Ze pipo of mipango miji iz vimbisharingi vitambizz baaaas!Nasingi duingi!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...