Mama wa kwanza Salma Kikwete akiwa pamoja na majenerali wanawake waliopandishwa vyeo hivi karibuni.Wa kwanza kushoto ni Mkuu wa tawi la mgambo jeshini Meja Jenerali Zawadi Madawili,Watatu kushoto ni mkurugenzi wa Masuala ya Wanawake Jeshini Brigedia Jenerali Grace Mwakipunda na kulia kabisa ni mkurugenzi wa utumishi jeshini Brigedia Jenerali Lilian Kingazi. Hafla ya kuwapongeza maafisa hao wa ngaziu za juu jeshini ilifanyika katika ukumbi wa JKT Mgulani hivi karibuni

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 10 mpaka sasa

  1. du, hapo wakina mama mmenimaliza. Hongereni sana kwa kuweza kupanda ngazi kufikia hapo. Mnatia raha sana na tunajivunia hilo. Chukueni mpaka ukuu wa Majeshi na Mungu awasaidie sana.

    ReplyDelete
  2. Wanawake wa nguvu sana nyie. Mungu awabariki. Inatia moyo sana kuona wanawake wanapitia kwenye heka heka za Kijeshi mpaka kufikia hapo walipo. Mubarikiwe sana sana.

    ReplyDelete
  3. Hongereni wanawake washoka, kwa kupanda vyeo. Ha hapo mmependeza kweli.

    Hii inaonyesha kuwa hakuna kitu kinachoweza mshinda mwanamke. Yale mambo ya wanawake hawawezi yamepitwa na wakati. Kinamama Oyeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee!

    ReplyDelete
  4. Hivi kweli walipigana vita gani vile?

    ReplyDelete
  5. walipigana vita ya jinsia hao kupambana na mfumo dume mpaka wameshinda .. hahahahaaa

    ReplyDelete
  6. jeshi gani jamani...la wakovu???

    ReplyDelete
  7. Michuzi, inabidi sana Tanzania itilie mkazo wa kuelemisha vijana wake.

    Mimi nikiona hiyo picha, na kumwona Brigedia Jenerali Lilian Kingazi, yanirudisha mwaka 1970 hapo Kibosho Sekondary School.

    Mwaka huo nilianza kazi ya kufundisha baada ya kuhitimu Mlimani na kupelekwa Moshi Technical Sec. School kufundisha.

    Kwa bahati nilipelekwa hapo Kibosho Sec. School kuwa
    "Invigilator" wa tihani wa kumaliza kidato cha nne.

    Kwa kuwataja wachache tu, watahiniwa walikuwa akina Esta Maro, Rose Rusimbi, Irene Temu na huyo Lilian Kingazi.

    Mara ya mwisho kumwona Lilian Kingazi ilikuwa mwaka 1975 akiwa Second Lieutennant baada ya kumaliza mafunzo hapo Mugulani.

    Hongera, Brigedia Jenerali Lilian Kingazi na maafisa wenzako wa kike, kulingana na "women empowerment and gender equality"!
    ,

    ReplyDelete
  8. Its about time; even though this comes late as it does. Hongera akina mama. Na shukrani nyingi kwa jemadari mkuu rais Kikwete. Furaha yao yetu sote hata sisi wanaume.

    ReplyDelete
  9. Mheshimiwa Raisi najua unasoma hii blog ya michuzi, ningependa kuona siku moja tunapata Mkuu wa majeshi ya ulinzi mwanamama....yes why not...

    ReplyDelete
  10. MH. Rais, kama ni kweli unasoma hii blogu ya supu nakushukuru pia kwa uchaguzi huu nan pia nakuung mkono kwa kuoa mwanamke mzuri. Huyu ndiye first lady anayefaa.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...