Kaka Michuzi,
Nakupongeza kwa mafanikio makubwa sana ya gulobu yako hii ambayo hata huku kijijini tarime tunaipata.
Kaka yangu Magabe Kibiti amekula nondozz ya masters ya economics kutoka St Cloud State University huko Marekani. Naomba sana uweke picha hizi kwenye gulobu yako ili kumpongeza kwa kumaliza shule.
Ujumbe ni kuwa familia ya mzee Kibiti inamuombea Magabe ili aendelee na kumaliza Phd ya economics. Ombi ni kumtaka arudi nyumbani akimaliza masomo yake ili afundishe wadogo zake hapa Tarime. Mwisho nakutakia wewe na wanagulobu wote mwaka mpya mwema wenye mafanikio.
Asante.
Mariam

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 9 mpaka sasa

  1. Hongera kaka!!!! heri ya mwaka mpya pia!

    ReplyDelete
  2. Mariam, wewe umemwandikia mtu ambae kapata digrii kubwa kiasi hicho, halafu unakosea, sijui bahati mbaya, hujui au nini. Hii ni BLOG na sio GLOBU. Badilika mwanamke, jifunze!

    ReplyDelete
  3. Siyo gulobu tafadhali, ni BLOG, sawa mama? Rudia tena, tena, tena, enheeee swadakta bila shaka hutakosea tena.

    ReplyDelete
  4. Jamani jamani,
    Hongera sana kaka Kibiti. Yaani nimekuwa excited ajabu kuona habari zako hapa mtandaoni. Dada Mariam ubarikiwe sana. Yaani huyu kaka tumemiss sana hapa kanisa la chuo kikuu mlimani. Imenikumbusha ulivyokuwa unaimbuisha ile kwaya yetu ya kanisa.

    Naomba ninukuu sehemu ya wimbe aliokuwa anaupenda sana na alituimbisha kwa furaha yote:
    Sing sing Halellujah to the Lord Almighty, .......
    Unakumbuka enzi hizo kaka Magabe?
    Yaani tunakumiss sana na tumefurahi sana kwa hatua uliyoipiga kimasomo. Kweli Mungu hujibu maombi tumwombapo.
    Dada Mariam naomba unipe email yake ili nimwandikie ananifahamu sana nikimwandikia na ninadhani atafurahi pia kusikia habari za chuo Kikuu mlimani.Naomba unitumie kupitia salumayu@yahoo.co.uk.
    Ubarikiwe kwa hatua hii.
    Ninakutakia pia mafanikio tele hapo Tarime, uende mbali lakini usipotee.

    ReplyDelete
  5. Hongera Mr Petroliii, You will understand what I mean bse I still remember how we went through tough times together as DARUSO leaders in the October 2000 strike/extended meeting.

    ReplyDelete
  6. ohhh Jamani,

    hongera sana magabe kwa mafanikio haya. maliza shule urudi nyumbani usizamie huko kwa wazungu mzee

    umenikumbusha sana maisha ya mlimani na DARUSO.

    Hongera

    ReplyDelete
  7. mkitaka majina ya utani marekani sio tarime,marekani paiteni tabora kwani ni kwa wanyamwezi.mdau wa kwa gulity.

    ReplyDelete
  8. Hongera Magabe! Amang'ana. I am very proud of you. Yeah tunaitaka hiyo PHD ipelekwe Tarime, Keep it up. Mwirege wa Wisconsin

    ReplyDelete
  9. Keep it up Mr.Maasa. You are ma' hero......I will always adore you...Hongera sana....Men!!!You deserved it....Goodluck and have a merry x-mass.........

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...