nguli wa utunzi na uimbaji kamarade ali choki 'mzee wa farasi' akiwa na mashabiki wake hivi karibuni katika klabu ya tcc chang'ombe. hivi sasa amehama twanga pepeta na kwenda endeleza libene katika kundi la tanzania one threatre (toto) kwa kepteni john komba

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 15 mpaka sasa

  1. WE ALI CHOKI MBONA UNATANGATANGA SANA, HUTULII SEHEMU MOJA?? HUKO TOT NDIO WANAKWENDA KUKUMALIZA KABISA KIMUZIKI. SHAURI YAKO KAKA, TAMAA MBAYA MKUBWA!!!!

    ReplyDelete
  2. Ni kweli watu tuna uhuru wa kufanya yote kwa matashi yetu binafsi bila ya kumbugudhi mwingine.. poa kabisa.. !! Lakini huyu jamaa mimi kwa kweli nimeshindwa kabisa kumuelewa na hii hama hama yake.. anatafuta nini huyu??? Haya nyie wana Sebene mkae macho na huyu bwana maana hajiamini na haaminiki huyu!!! Si tamaa bali sasa ni balaa.. (dRU)

    ReplyDelete
  3. hao jamaaa mapacha

    ReplyDelete
  4. Ana kazi kubwa huko maana tangu Banza atoke huko TOT imekua haina lolote.
    Je ataweza?

    ReplyDelete
  5. kaka michuzi hao jamaa ni mapacha wananitesa kweli nikiwaangalia naweza pata contact zao natumaini ndio wale wa tanga naowafahamu. na vipi hawajaoa namtaka mmoja wao no matter what

    ReplyDelete
  6. Kina kaka mapacha wazuri nyie
    loh !!!!
    mngeweka contact basi kina dada tuwatafute
    nimechoka na hawa watu huku ughaibuni
    mmmmhhhhh

    ReplyDelete
  7. Ili kupunguza kutuchanganganya sisi wapenzi wa muziki naomba Bunge litunge sheria ya kuruhusu wanamuziki kuhama mara tano tu kutoka bendi moja kwenda nyingine...na kama mwanamuziki kama Ally choki, Banza na Muumini watataka kuhama zaidi ya hizo mara tano basi waende likizo isiyopungua miaka mitano kwanza wakirudi wanapewa tena ruksa ya kuhama mara nyingine tano..wadau mnasemaje?? Hiyo itapunguza sana confusion..
    Naomba kuwasilisha

    ReplyDelete
  8. wee nawe ovyoooo yaani ktk karne ya 21 bado unataka tuishi kama enzi za miaka ya 80 sasa sheria ya kuwazuia wanamuziki zina maana gani

    ReplyDelete
  9. Ali Choki ni HANDSOME kwelikweli.....jamani...mnyonge mnyongeni ila haki yake mpeni.

    ReplyDelete
  10. Mwaka, M. Mimi nakubaliana na wewe na mikono na miguu yote. Maana hawa wajinga hawajui watakacho bora wakienda likizo watapata muda wa kutafakari

    ReplyDelete
  11. Jamani huyu Alichoki amezidi huko alikoenda ndio kabisa kapoteza mwelekeo jamani ngoja ataanza kuimba taarabu na kwaya ndipo atakapo lijua jiji yaani yaliwashinda wenzie yeye kaona ndio ataweza anyway may be kafwata maslahi lakini sio kuendeleza kipaji mwe! hzi njaa jamani kazi kweli kweli alikosa nini kwa mama Asha Baraka? Na hapo alipoenda atulie coz atahangaika weee then atarudi tena twanga kwani pale ndipo kisima cha burudani na hao waliompokea wawe makini coz hatabiriki yule hakawi kupokea za mwezi mmoja then akala kona hana dogo huyo ati da! kijana hatuliii kutwa kuchwa anahama band hafiki jamani mweeeee!

    ReplyDelete
  12. HAO WATOTO NI MAPACHA WANAFANYA KAZI CONTAINER TERMINAL (TICTS) NI WATOTO WA MZIRAY WA BANDARI. BADO VIDOGO MTAVIBAKA TU JAMANI, ILA VINA SAUTI NZITO TAYARI KWA HIYO VINAWEZA KUGAWA MBEGU ZA WATOTO...

    ReplyDelete
  13. hapo sasa ndiyo alichoki amefika finally,hamtomsikia tena!ali choki kwisha kabisa!

    ReplyDelete
  14. Nampa Hongera aliyewazaa hao twins! Vijana wamesimama.

    ReplyDelete
  15. anatafuta maslahi mwacheni atafanya kazi wote mtashangaa sasa ndio kajiunga na bendi itakayomtoa hapo alipo na kumfanya awe mkali zaidi tunaangalia umri hivi sasa umri wa choki umefikia mahala si pa kupigia bendi za kihuni kama hiyo ya twanga na kupepeta sasa hivi anatakiwa kupigia bendi kama tot plus na kuanza kujitangaza na kugombea ubunge kibaha picha ya ndege kwani vipi komba ccm hata ukiwa chizi utapata kura tu mshikaji ili mradi una mtaji na choki mtaji wake ni domo lake na utunzi vipi Hadija Kopa

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...