Hii ni taarifa ya kifo cha Mtanzania mwenzetu ambaye katupwa pembeni ya barabara.


Inaaminika kifo chake kimetokana na vifurushi vya unga ambavyo kakutwa navyo tumboni kwa kua hakuwa na majerui mwilini ya aina yoyote.
Mdau Coventry


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 48 mpaka sasa

  1. tunashuru kwa taarifa yako marehemu hakua na majeruhi wala majeraha sasa wewe ulijuaje kama unga ndio uliompasukia ata kabla wahusika na wataalamu wakazi zao awajatangaza sababu ya kifo.

    ReplyDelete
  2. Poleni sana wafiwa sasa inaelekea ameuwawa au vilimzidia wenzie wakamtupa mapumziko mema

    ReplyDelete
  3. MICHUZI UJUMBE KWA TANZANIA DIASPORA

    Another missteps, It is SAD, your wife and family will miss you intensely.

    He should have stayed doing a box Job, invest at home, invest at home, invest at home and last not least for those who happen to have offspring, the parents should make sure that their kids have access to EDUCATION, and help them to achieve their goals for themselves and future GENERATION, in helping themselves and Tanzanians back home in GENERAL. Education is the key to everything, and thats the theme of most wabeba mabox, and I must say for Majority of them, they had done a remarkably well at home in investment, in providing assistance to their poor family whether on Education or well being.

    It is painful long process and it is the only legitimate process for those of us who are less educated and not coherent enough to get to well paid UK and US Job market.

    I urge for those who are hard working citizens to stay the course, and never being tempted to get on this illegal trade of any manifest either car theft business or drugs business, or whichever may result you in spending those precious hours, years of life in Jail.

    This IS A SAD day for the family of this young man and that of Mr. Malakasuka and Tanzanians Diaspora in general. I know there is a huge contrast between the two but all terms to greedy and manipulation. I hope we all take this hard learned lessons.

    May GOD forgive your sins and REST IN PEACE.

    May GOD Give us courage and determination to go ON. for the good of Tanzania and Tanzanians at large.

    AMEN

    By Mchangiaji

    ReplyDelete
  4. Poleni kwa msiba wa mtanzania mwwenzetu. Mtoa taarifa sijamuelewa kidogo pale aliposema kauwawa na katupwa barabarni, then huenda issue za unga ndiyo chanzo kwa sababu hakukutwa na jeraha. Sasa huyu aliuwawa au vipaki vya unga vilipasuka? au waliomua na kumtupa barabarani ndiyo hao waliompasua na kutoa huo unga? au jamaa waliombebesha huo mzigo ndiyo waliomua ili wafute ushahidi?.
    Poleni sana wafiwa

    ReplyDelete
  5. Raj Patel amerudi nini? huyo mchangiaji hapo juu anasound just like him.Poleni sana wafiwa katika kipindi hiki kigumu mungu atawasidia.Mlaze pema peponi.

    ReplyDelete
  6. napenda kuchukuwa fusa hii kuwapa pole ndugu ya wafiwa pamoja na Watanzania na wadau waishio huko

    ReplyDelete
  7. poleni jamani sasa uko coventry hamna watanzania, kumsaidia poleni wafiwa.

    ReplyDelete
  8. POLENI SANA WAFIWA

    HABARI ZA LEO KAKA MICHUZI NA WADAU KWA UJAMLA
    nakuomba usinibania comment kaka michuzi :-
    Ni masikitiko makubwa ambayo ndugu zetu wa Tanzania waishio maeneo mfano haya:- Northampton,Coventry,London,Milton keynes na Leicester,Birmigham,Reading,Slough na mengine mengi lakini haya ndio vitovu vikubwa vya mahafaa.nitatoa mfano hai kuna rafiki yangu(jina kapuni) alikuwa akiishi hapo Cv westmidlands wakati mimi naishi northampton yeye alikuwa anajiusisha na biashara za haramu na group la wenzie London(majina kapuni)kwa bahati mbaya au nzuri siku ya siku wazee walimdaka na kumtia mbaroni ninavyoongea mpaka sasa hivi, huu ni mwaka watatu bado yupo ndani.nilikuwa nikimshauri sana achana na biashara hizi zina mwisho wake hakutaka kusikia na miaka ya nyuma alikuwa mchapakazi kweli kweli mbeba box maarufu sasa unajua tena ukishaanza kupata hizi hela za haraka haraka uwezi kurudi kwenye hili li baridi la warehouse.masikini kabla hajafanikiwa vizuri mzigo wapili mbaroni alifanikiwa kununua gari la kifahari moja masikini.ameacha mke na mtoto mmoja ambao wanaangaika uraiani na unajua nchi hii kumkuza mtoto kama mzazi pekee bila msaada wa kupokezana ni ngumu na wale rafiki zake waliyomsababisha kama vile hawamjui mama watu kumjulia Khali halafu tabu ya nini ukisikia wazee unaanza kujificha ficha.Kwa umri ni mtu mzima sasa kwa mtazamo wangu mimi naona amepoteza muda wake sana ambao awezi kurudisha nyuma mimi binafsi namshukuru ALLAH wangu maisha yangu sio haba naweza kutunza familia yangu hapa na nyumbani Tanzania.
    USHAURI KWA WATANZANIA WENZANGU KWA UJUMLA NYEMBE,MADAWA,UWIZI WA MALI ZA WATU YANAMWISHO HIVI MNAFIKIRI KUNAMTU ANAPENDA KUWA MASIKINI JAMANI BASI NJIA HIZI ZINGEKUWA RAHISI WOTE TUNGEKUWA MATAJIRI.
    MAPUMZIKO MEMA KAKA
    As-sa-laa-mu `a-lai-kum ah-lad di-yaa-ri mi-nal mu'-mi-nee-na wal-mus-li-mee-na wa innaa in-shaa-al laa-hu bi-kum la-laa-hi-qoon. Nas-a-lul laa-ha la-naa wa la-ku-mul `aa fiyah.

    Wajina
    Othuman

    ReplyDelete
  9. POLENI AWAFIWA: ALIKUWA ANATAFUTA MAISHA BORA

    ReplyDelete
  10. Poleni sana ndugu waislam kwa msiba huu mzito.nasikitika sana huyo jamaa hapo juu aliyesema huyu ndugu yetu alikuwa anatafuta maisha sio kweli uwezi kutafuta maisha kwa kuwauwa watoto wa wenzio yaani huo unga ni kitu haramu sawa halafu wewe unasema kutafuta maisha kumpoteza ndugu yetu ndio inatia uchungu ila sio kitendo binadamu tupende kuwa wa wazi bila kuficha jambo lenye ukweli ndani yake samahani kama niktakuwa nimekosea

    malik
    london

    ReplyDelete
  11. anon March 30, 2008 12:50:00 PM UMECHANGIA VIZURI SANA POINT YAKO WATU WENGI WANGEKUWA NA MTAZAMO HUO WANGEKUWA MBALI NIKIFIRIA WEWE RAFIKI YAKO ALIKUWA ANAJIUSISHA NA VITU HARAMU LAKINI WEWE ULIKAA PEMBENI ULIJIEPUSHA NI KITU KIKUBWA SANA UZIDISHIWE

    ReplyDelete
  12. NIMEINGIA NDANI YA HIYO BLOG YA WATANZANIA HUKO MJI ALIPOFIA HUYU BWANA http://wemsas.blogspot.com/ EHEE BWANA JAMANI WATU WAMECHOKA ILE MBAYA NI BOX AU EBU TAFUTENI HELA NJOONI TUWAONYESHE BIASHARA BONGO

    ReplyDelete
  13. Nyie msianze kuuliza maswali ya kijinga hiyo taarifa ina link ya coventry telegraph,sababu za kifo ni unga uliokutwa tumboni,wenzie wameamua kumtupa baada ya kugundua mwenzao kafa.Nakubaliana na Othuman hapo juu, watanzania tulikuja nchi za watu maisha yetu yalikua low key lakini siku hizi ujambazi wa aina zote sisi ndio ajira zetu,yote tunataka plasma 100",gari za kifahari, sherehe za kifahari kwa kuibia watu huu ni mfano mzuri na wengi yatawakuta, na sio kwamaba ni jinsia moja tu ni wanawake kwa wanaume,mwaka jana tumezika mmoja Northampton.Hivyo vijiji vyote vilivyo tajwa na Othuman ndio vinaongoza kwa wakazi waki zanzibari kwa ujumla(don't hate me I'm just telling the truth)na ndio kazi zao hizo majority(bisha basi).
    Na wewe unae sema alikua anatafuta maisha hujui thamani ya uhai kama alikua anatafuta maisha vipi kapoteza maisha na hao aliokua akiamini ni rafiki zake wakamkimbia nakumuacha aokotwe na wasafisha mji(you know who you are that will be in your conscience for the rest of your lives).
    USINIBANIE LAZIMA WAPEWE VIDONGE VYAO.

    ReplyDelete
  14. Jamaa hapo juu kaongea Point kuhusu watanzania tuwache tamaa na ziki, za kuchanja kuchukuwa mikopo wakati unajuwa huwezi kulipa, masikini unaweza kuwa hapa akhera mungu akakupa jitahidi kumuomba mungu, kunywa pombe si ndio kutoa fikra kumuomba mungu ndio kutoa matatizo, ishini maisha ya halali japo magumu ila siku ya mwisho mungu atakupa wacheni majungu, kokote kule mungu kasema unaweza kuishi ndomana binadamu tuko rangi tofauti kwa uwezo wa mungu katuchanganya wote japo kila mtu anatoka bara lake. inshallah mungu atatusaidia, Allah amuweka mahali pema peponi tujifunze kwam ambo kama haya jamani hasa tuliokuwa nchi sio zetu utajiri wa haraka haufai someni kama hamuwezi kusema jitahidini kazi kazi hata kuuza nyanya uweze tu kuitizama familia yako. tafuteni pesa nchi yoyote ila sio kimagendo.

    ReplyDelete
  15. wewe anonymous wa kwanza wacha upuuzi au ni mtoto mdogo sana? kabla ya kuleta comments zako kwa nini husomi taarifa yote? umewekewa link hapo chini ukiisoma utagundua ni polisi ambao wamethibitisha hayo alosema mleta habari.
    Mola amlaze pema marehemu na amsamehe makosa yake amin

    ReplyDelete
  16. He deserves what he got,no mercy to merchants of death!!!

    ReplyDelete
  17. Huko Uingereza hamna dogo. Pamoja na yote hayo, matawi ya CCM yanaota kama uyoga. Ni hao hao wanaofurika CCM au ni wengine? Hata hivi, namsikitikia marehemu na familia yake. Namwomba Mungu awateremshie baraka zake.

    ReplyDelete
  18. No symphathy...to those who prey on society's most vulnerable and feed addiction.Let him rot in hell...

    ReplyDelete
  19. acheni hizo angefanikiwa mngemsifia,mbona wengine huko mnatumia njanjaa bila vitambulisho halali kwani hilo sio kosa na dhambi.Mbona kuomba visa mtu anadanganya kwani hiyo si dhambi ,maisha ni ujanja angalia wenzetu wa nigeria walivyoendelea kwa sababu ya ujanja.

    ReplyDelete
  20. Kila mtu huvuna anachopanda, haya ndio matokeo ya utajiri wa harakaharaka.

    ReplyDelete
  21. Poleni wafiwa.

    Ndugu zangu wabeba mabox msidanganyike wala kurubunika kupata pesa ya haraka haraka. Na mkisha pata kumbukeni ku invest nyumbani.

    ReplyDelete
  22. Poleni sana wafiwa na jamaa wote wa marehemu.
    Vijana wenzangu jihadharini sana na biashara hii haramu. Sio kutafuta maisha bora bali ni kuangamiza jamii nzima.

    ReplyDelete
  23. WE ANON WA KWANZAN NIMESHAKUFAHAM
    WEWE PIA UTAKUWA MBEBAJI MZURI WA AWALI
    ILA NI ISSUE YA TIME TU.MWAMBIE
    JAMAA YAKO AMBAYE HUWA UNAFIKIA
    AACHANE NA KAZI HIYO NA YEYE MUDA
    SI MREFU TUTAMLENGESHA KWA WAZEE
    NA WEWE UNAWEZA JUMUISHWA UKAKOSA
    KUISHI TENA HAPO KWA MALKIA.USHAURI
    WA BURE KAKA.
    NDUGUYO LEICESTER

    ReplyDelete
  24. Nyinyi watz mlioko UK mchangieni sasa mrudishe mwili uzikwe kama tunavyosoma kila vinapotokea vifo vingine.... Au mnatumia vigezo gani kwa mtu kuchangiwa na kurudishwa home... muwe wazi kwani kuna kila aina ya watz huko.

    ReplyDelete
  25. Kuna limk ya local paper inayoonesha masuala ya unga. Toxicology lazima ifanywe kwa sababu inasemekana tests za awali hazikuwa conclusive. Hili ni jmbo la kawaida kiutendaji unahitajika usahihi wa ngazi fulani kuweza kusema kama kaua na toxocology ya namna gani kwani hivyo vifuko 71 vyaweza kuwa ni sambusa 71 alizokula labda akawa na indigestion na hazikusagika.

    Sala langu kwa mchangiaji ni kama kawasiliana na Polisi wa kuzuia ualifu au wapelelezi endapo alimjua marehemu.

    ReplyDelete
  26. MUNGU AMLAZE MAHALA PEMA PEPONI, AMINA. NA WEWE "MCHANGIAJI" ACHA UJINGA WAKATI WATU WAMAFIWA HAPA. HICHO KINGEREZA CHAKO UNACHOANDIKA HAPA KUWAAMBIA WATU WASOME KINAKUAIBISHA, KWASABABU SI CHA MTU ALIYESOMA! ACHA HIZO.

    ReplyDelete
  27. Mdau Othman.. Asante kwa dua ya kuzuru makaburi... lakini hapa sio mahala pake. unatakiwa kusema hiyo dua unapotembelea makaburi tu.. Kama unataka kumuombea marehemu dua unasema Inna lilah wa inna ailaihi raajiuun.. (Hakika sisi ni wa Allah na hakika kwa Allah tuta/narudi)..na dua nyingine nyingi tu.. kama Allahuma ighfir lahu wa Arhamhu..

    ReplyDelete
  28. haya wadau wa uk msijirushe sana muwe mnakumbuka wenzenu wakati wa shida pia, kuanzia hapo coventry watanzania mpunguze chuki na majungu, msaidiane nje ya nchi.

    ReplyDelete
  29. Ndugu watanzania wenzangu, hayo ndiyo maisha waishio vijana wengi walio ughaibuni hasa wale wanaotaka maisha mazuri kwa haraka haraka. yeye sio wa kwanza. Wengi wa wabongo wanazikwa na councils/governments huko UK. Ndio ile unasikia mtu fulani kaenda ulaya siku nyingi hana communication wala nini. Ndugu zangu, maisha mazuri hayataki haraka.....lazima ufanye kazi ndio upate vitu vizuri.
    Wale watu wa London, nina uhakika mnamkumbuka Beka mzee wa katesa sana spain kisha akatupwa barabarani kama huyu, na kesi yake bado iko London. Uongo kweli? Wengi mnajua na mshakula pesa zake sana.
    Wabongo wenzangu, msidanganyike na watu hawa wa ulaya, maisha yao ndio kama hayo ya kubahatisha na kuishi kwa kufukuzana na polisi. Ni wachache sana wanaoishi wakiwa wanafuata sheria na kutafuta pesa kwa haki. Na ubaya zaidi wengi hata nyumbani hawakumbuki.
    Hata mungu hapendi kuuza unga, unategemea kupata baraka kwa mateso ya watoto wa watu?

    ReplyDelete
  30. haraka haraka haina baraka so kulikuwa na wachanjaji(wezi wa credit card)wamekwisha,unga ukawa deal sasa mmoja mmoja maana huyu ni wa pili sasa mwingine alifia london huko miaka miwili iliyopita,na sasa wameingia kwenye wizi wa magari ya kifahari na wameshaanza kukamatwa maana expensive cars zote huwa hazikosi traker so mwendo ni ule ule,kuweni na maisha ya kawaida tu,tatizo watanzania ni copy cut wakiona kitu tu wanataka bila kujua gharama zake na mtu alikipataje.

    ReplyDelete
  31. sio mateso ya watoto wa watu wale wazazi,ndugu na jamaa wa waathirika wa madawa ya kulevya ndio wa kusikitikiwa na yote haya kiini chake ni watu kama hawa wanafanya hatutali kuogopa uwizi na mambo mengine

    ReplyDelete
  32. Michuzi mara nyingi naweka comments hauziweki naomba hii iingie katika comments.

    Mwenyezi mungu ametoa na ametwaa jina lake lihimidiwe. Poleni sana wafiwa na tunaomba roho mtakatifu awatie nguvu katika hiki kipindi kigumu. MAY HIS SOUL REST IN PEACE: Amen.

    Kwa kweli walio wengi tunataka maisha ya haraka na yenye ufahari bila hata kujali unamuumiza nani. Deal za unga ni sawa na jambazi anavovamia nyumba luiba kisha akaua waliomo. UNGA nao unaua watoto na ndugu zeu hiyo yote sababu ya maisha ya haraka haraka.

    Wadau mnaojihusisha na hii biashara ACHENI JAMANI... sio ughaibuni peke yake ila na nyumbani someni fanyeni kazi kihalali na unachopata ndio haki yako. Kuna msemo unasema VIDOLE HAVILINGANI hivo sio kila mtu anaweza kuwa na maisha kama mwenzie. Cha kufanya ni kuhangaika na kupata kipato halali...

    Biashara hii SIYO tafuteni kingine cha kufanya. Ushauri wa bure kwa wale ndugu zetu wanaoendelea na hii biashara.

    ReplyDelete
  33. Marehemu hayuko peke yake wako wengi sana, tena siku hizi utasikia wengi wao wakidao wanafanyakazi scotland, unga mtupu, kwa nijuavyo mimi dini zote zinakataza uuzaji wa vitu haramu iweje ndugu zetu mmfanye hivyo? kwanini mnateketeza maisha ya vijana wengi kwa lengo la kupata utajiri wa haraka haraka na kuishi maisha ya kifahari? SHAME ON YOU DRUG DEALERS 'JAHANNAM' IS WAITING FOR YOU INSHAALLAH. Simuonei huruma marehemu hata kidogo hayo ni malipo ya M'mungu kwa watu wote aliowateketeza kwa uuzaji wa madawa yake. MALIPO NI DUNIANI AKHERA HUENDA HESABU.

    ReplyDelete
  34. MMESAHAU CHEQUE FAKE WATU WANATABIA YA KUTUMIA BANKS TO DEPOSIT CHEQUE FAKE MWISHO WAKE MTAUONA KUNA MAJAMAA HAPA LONDON TENA WANAUMRI MKUBWA NADHANI KAMA 50 HIVI NDIO TABIA YAKE KIONGOZI BISHOO HIVI ALIKUWA MAARUFU SANA TANZANIA YETU MACHO

    ReplyDelete
  35. RIP

    Lakini this is so sad news....Jina la TANZANIA linapamba moto na kuja juu kishenzi kwa mabaya mengi sana tu siku hizi....Ukiangalia news ni UK magari ya uizi ...ring leader....mtanzania....Mara huyu katupwa tena njiani ....mtanzania...mara waizi wa bank...mtanzania....wengine waizi wa vifaa vya computer...mtanzania....mara hapa kazini CNN news sasa hivi asubuhi BREAKING NEWS .... mara mtanzania amehukumiwa kwa 1998 bombing.....kila mtu ananitupia macho...wow!!! talibans in your country too????.....yaani inasikitisha...soon watatuona kama wanigeria...

    Mbona wahindi wako so many kila kona ya dunia lakini maasi yao hayasikiki kwa nguvu hivi? Sisi wala hatuko wengi nchi za nje lakini hao wachache tulioko kazi mbona ipo.....!!!!!!

    Eeee Mola utuengezee rehema na busara!!!!!!

    ReplyDelete
  36. Mbona sioni sehemu yoyote ya hii link inayosema kama huyu jamaa ni Mtanzania???????????????

    ReplyDelete
  37. Watanzania kwa wizi sasa hivi wa_nigeria wamesingiziwa.

    ReplyDelete
  38. Drugs courier theory in A45 body find
    Mar 31 2008 By Michael Corley

    THE man whose body was discovered on the verge of the A45 in Warwickshire was a Coventry father who was carrying a huge quantity of drugs in his body.

    Said Othman, aged 38, from the Foleshill area, had swallowed 71 large packets of what is believed to be cocaine.

    Police are working on the theory that the father of two was a drugs courier.

    Swallowing drugs sealed in condoms is a well-known technique for smuggling substances into the country.

    Mr Othman's body was found by council workers who were picking up litter next to the Coventry-bound carriageway, between the Little Chef and the War Memorial roundabout, near Stretton, on Tuesday at about 9am.

    Toxicology tests are still being carried out to determine the cause of death, after a postmortem proved inconclusive.

    A Warwickshire Police spokesman said: "The presence of these packets indicates that Mr Othman was involved in the illegal importation of drugs into the country and officers are working with points of entry into the UK including ports and airports to establish his route of travel."

    Mr Othman, who came to the UK in 2002 from Somalia and worked as a kitchen hand, was last seen by his wife at their Coventry home on Monday, March 17.

    The family were said to be too upset to comment.

    Police are still appealing for anyone who knows where he has been since he went missing.

    Officers are also keen to hear from anyone who noticed any suspicious activity on the A45 northbound between the Thurlaston and Stretton roundabouts during the 24 hours leading up to the discovery of the body.

    Mr Othman was wearing faded blue jeans, sandy-coloured laced boots, a white polo T-shirt with horizontal orange, white and brown stripes, and a Swatch watch.

    Anyone with information should call officers on 01788 853787 or Crimestoppers, anonymously, on 0800 555 111.

    * SIX years ago, and just six miles from the spot where Mr Othman's body was discovered, the body of a woman, aged about 60, and of Jamaican descent, was discovered on a grass bank next to the M45, by a workman.

    She had swallowed 10 small packets of cocaine. It was believed she was acting as a courier and was dumped after dying of poisoning.

    No one was ever caught in connection with the incident and she was never identified

    ReplyDelete
  39. Wewe Anony "Sunday, March 30, 2008 1:49:00 PM EAT (Malik-London)" sikupendezwa na maoni yako. Pole itolewe kwa watu wa makabila au dini yoyote-sisi sote ni watanzania. Inaelekea una udini sana!!

    ReplyDelete
  40. THE GUY IS SOMALIAN and not Tanzanian. according the police report.

    ReplyDelete
  41. 'GET RICH OR DIE TRYING'

    ReplyDelete
  42. huyu jaamani ni MDEBWEDO alijilipua kwenye vurungu za uchaguzi TANZANIA na kujifanya MSOMALI.Nakushangaa wewe unaye mtetea kusema ni msomali hujui maisha ya ulaya?

    ReplyDelete
  43. Naona Anonymous wa Monday, March 31, 2008 11:06:00 PM EAT hajui style za watanzania wanaoishi ulaya hasa Uingereza. Kule kuna aina tatu za watanzania. Kwanza, wale halali wenye passport za kijani za Tanzania ambao wengi wanakuwa kule kwenye shughuli za masomo/matembezi na ambao hata likizo Tanzania utawaona wakija na hata wakimaliza masomo wanarudi nyumbani kujenga taifa; ya pili ni 'waliooza' ambao walikuwa na passport za kitanzania lakini kwa makusudi na tamaa mbaya wakaamua kutofuata sheria za uhamiaji za UK na kuamua kuzamia kinyemela bila kurenew visa zao (hawa huwa hawajagi likizo kabisaaaa hata wafiwe na baba mzazi kwa sababu hawana travel documents) na aina ya tatu na al-maarufu kwa vijana wapenda maisha rahisi/wasio na mipangilio/wenye tamaa ni 'milipuko' au 'waliojiwasha', hawa ndio asilimia kubwa sana na ndio kama huyu mwenzetu ambaye police wanasema ni msomali. watanzania wengi huwa wanajilipua (kubadilisha status na kudai wao ni wakimbizi) kisomali au kirundi au kinyarwanda. NAWASIHI WATANZANIA TULIO NYUMBANI HAWA WATU WANAOKUJA HUKU NA PASSPORT ZAO ZA MILIPUKO WASIWABABAISHE MAANA WENGI NI WABEBA MABOKSI ULAYA.....AU KUISHI EITHER KWA KUPOKEA BENEFIT AU KWA KUUZA UNGA KAMA HUYU. WAAZAZI PIA WAOMBEENI WATOTO WENU SANA MAANA WENGI MNADANGANYWA NA PICHA WAZAZOPIGA ULAYA ILI KHALI HAWANA JIPYA WANALOFANYA..........AKINA CHRISTINA ALPHONSE MFANO......WENGI MNAWAJUA.......FAINALI UZEENI. BEBENI WAZEE SIJUI NYIE MKIZEEKA ATAWABEBA NANI? MAISHA YAKO BONGO BWANA ASIKWAMBIE MTU AKILI KU MKICHWA LAKINI UKIJIPANGA VIZURI AHHA...HULALI NJAA NA HATA HUPATI STRESS ZA AJABU AJABU. WABONGO KUMBUKENI KWENU JAMANI......NA LA MUHIMU MUOMBE MUNGU WAKO AKUONGOZE....AMISHA YA KUBEBA BOKSI MPAKA LINI? HUO NI UTUMWA JAMANI. TENGENEZENI MITAJI MRUDI HOME....KUNA OPPORTUNITIES KIBAO...PESA YAKO TU! UKWELI LAZIMA TUUSEME, WENGI MNABANGAIZA NA KUISHIA PABAYA KAMA HUYU JAMAA.

    ReplyDelete
  44. ndio sasa cha ajab nin mara kujlipua mara nin jaman acheni wivu mbona wao walikuja kwetu na stail tofauti "waeneza dini na kadhalika" na maisha popote kaka hata hapa watu wenye akili wanafanya mambo yao lakin mi nakwambia sie wabongo tunapenda sana staarehe na tamaa tumeweka mbele tofauti na wenzetu waasia kwa mfano jamaa kama kweli ni mbongo na ina maana anaa status tayar angeweza kusoma kama mzawa kwa hela ndogo kuliko kulipa karibu 10,000pounds kwa international student kwa mwaka,ambayo hiyo elimu ingemsaidia sana ok anyway tuachie sie twenye milipuko tuwamalize hawa na mikoba yetu mekundu

    ReplyDelete
  45. jaman acheni wivu mara kujilipua mara nini we kaa na viza ya student uongeze muda kila siku na masomo yako yasiyoisha tuachie sie na tule vyetu kila kitu kwa bibi hapa hakuna nini wala nini akili kichwani wajanja tunapiga bao kilaiiin........aaah wao pia si walijifanya wamisionari sasa tunakamua wenye nywele sory "maaakil"

    ReplyDelete
  46. Huyu jamaa wamemwandika ni MSOMALI! Kwanini nyie Watanzania mnataka kudandia watu wa mataifa mengine kuwa wa kwenu?? Au imekuwa ni "deal" ya kuchangishana tena?

    ReplyDelete
  47. Location is actually among the most vital aspects of an ideal TV film location. The area must be easy to get to and near urban areas. https://gabhandymancoventry.co.uk/

    ReplyDelete
  48. During World War II Coventry had the dubious honour of being the UKs third most bombed city after London and Plymouth. Sadly that industrial production base has virtually disappeared leaving only a few truly industrial scale companies within the city. more info

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...