Kwa wanachama wote wa F.C.BONGO,
Ningependa kuwataarifu kuwa mazoezi rasmi ya kujiandaa kwa mashindano ya Prevention Cup 2008 yataanza siku ya jumamosi tarehe 3.5.2008 saa kumi na moja jioni katika uwanja wetu wa kawaida wa Väinämöisenkenttä a.k.a (Vumbi Stadium) Hietsu.
Kabla ya mshindano tutakuwa na mechi za kirafiki na baada ya mashindano pia tutakuwa na mechi zingine za kirafiki ambazo moja wapo ni ya safari ya Tampere na ingine ni safari ya Stockholm Sweden.
Majadiliano na maoni kutoka kwa wanachama wote yatajadiliwa baada ya mazoezi katika wiki tatu za kwanza.
Wanachama wote mnakaribishwa kuchangia mawazo yenu ili kufanikisha mafanikio ya mwaka huu wa 2008. Kwani tumepania mwaka huu kuchukua lile kombe.
Mazoezi ya winter yameenda vizuri sana, wachezaji wengi wamehudhuria na tunategemea tukianza Vumbi stadium wengi zaidi watahudhuria.
Hapo juu ndiyo ratiba kamili ya msimu huu wa summer.
Unaweza kudownload attachement kwa ajili ya kuprint.
Regards:
Ezza


Bongo FC..yaani safari mje kabisa na kagunia kakubebea magoli.
ReplyDeleteIla jina la uwanja wenu wa mazoezi linamvuto..uwanja wa vumbi...aa aaalol..
pamoja watu..jipangeni sisi tunawasubiri
Sawa Edwin, lakini kumbuka mwaka jana tuliwanywisha manane nyumbani kwenu, na safari hii tunakuja na mtindo wa SEX FOOTBALL sio sexy football.
ReplyDeleteBongo FC muwe makini sana na Kilimanjaro ya sweden, wanaloga mno. Mdau -Adam-
ReplyDeleteKaka Ezza, siku hizi umekuwa manager wa Timu badala ya U-Dj??? Nawatakia kila la heri mlibebe kombe hilo. Nisalimie akina, Mzee Mataluma, Mzee Bonanza, Kijana Shaaban Bakari, Moddy Bakari, Dj Erick, Na Smart Boy Erick. Mimi
ReplyDeleteWewe ndaki kwani umesahau mwaka jana mvua ya magoli ilivyo wanyeshea nyumbani ?
ReplyDeleteSiku hazigandi..muda si mfupi tutatundika matokeo ya game letu na la kwenu.
ReplyDeleteKwanza tumefanya usajili wa kufa mtu safari hii.
Time will tell...chwaaap