Kama wewe ni mfuatiliaji wa maendeleo na mapinduzi mbalimbali katika zana za habari na mawasiliano ya umma,yawezekana umeshawahi kujiuliza maswali kadha wa kadha kuhusu mitandao kama Wikipedia.


Wikipedia hivi leo ni mojawapo ya mitandao ambayo ina watembeleaji na wachangiaji lukuki kila siku. Bahati nzuri au mbaya ni kwamba Wikipedia inaendelezwa na watu kama mimi na wewe.Kuna uzuri wake na kuna ubaya wake. Ukweli huo ndio pengine unaufanya mtandao wa Wikipedia kuvutia wachunguzi na watafiti mbalimbali wa zana mpya za mawasiliano ya umma.


Hivi karibuni kituo kimoja cha televisheni cha nchini Uholanzi,
VPRO Backlight, wameandaa documentary waliyoipa jina la The Truth According to Wikipedia.Miongoni mwa watu ambao wamehojiwa katika documentary hiyo ni Ndesanjo Macha(pichani) ambaye wengi hivi leo tunamfahamu kama “Mfalme wa Blog za Kitanzania”. Ndesanjo ndiye chachu ya kuanzishwa kwa blog nyingi za watanzania kama tunavyoziona na kuzitembelea hivi leo.

Tunakusihi uitazame documentary hiyo hapo chini kwani tuna uhakika utajifunza mengi na pia kupata majibu mengi ya maswali ambayo pengine umekuwa nayo kuhusu Wikipedia. Baada ya hapo(kama utaona yafaa) usisite kujiunga na
Wikipedia katika lugha ya Kiswahili ili nawe uwe mmoja miongoni mwa mamilioni ya wanajumuia(kutoka lugha na mataifa mbalimbali ulimwenguni) walio mstari wa mbele katika kupashana habari, kubadilishana maarifa, kuhifadhi historia mtandaoni nk nk.

Ukitaka kusoma mahojiano tuliyowahi kufanya na Ndesanjo Macha siku za nyuma bonyeza hapa.


Blog ya Ndesanjo unaweza kuitembelea kwa kubonyeza hapa.


Mtazame Ndesanjo kupitia documentary hii
ukweli-kwa-mujibu-wa-wikipedia/

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. Ndio King!kazi always inalipa keep up the good work!

    ReplyDelete
  2. aISEE MICHUZI, NILIKUWA SIJUI KABISA KUWA WIKIPEDIA IKO KWA LUGHA YA KISWAHILI TENA SAFI,

    mmoja anisaidie hivi huwa wanalipwa na nani, au wanapataje faida? sijui nauliza, mtu asinitukane tafadhali, maana kufanya kazi hiyo si mchezo.

    Hongereni jamani kazi nzuri.

    ReplyDelete
  3. We are getting on an age, where people and web activists, moving the activism's onto the new level. "Whichever the mass believe it is true and then that become the TRUTH". Internet has become shared ideology on a massive scale.

    We now have blog tv, heading to more interactive web shares, where people create own web television and discuss and talked live about the issues from personal life experience to political issues through mass sharing, and that it is GREAT!.

    Question, The trend is expanding, but who then will be controlling it, it is just out of curiosity, there is definitely a temptation to do just that, by the so called expertise, then ideological believe will take a center stage, it will be tuned to fit the ideological values of the powerful, WIKIPEDIA isn't an exception ?

    By Mchangiaji

    ReplyDelete
  4. Nadhani umefika wakati sasa kwa wa TZ kujua opportunities za kutumia concept ijulikanayo kama Open Content.

    wikipedia inafanya kwazi kwa kutumia dhana ya Open Content ambapo makala/taarifa zinazowekwa humo huwekwa na wachangiaji waliotapakaa ktk kijiji chetu cha dunia via wwww. hii ndio tofauti kubwa kati ya wikipedia na site kama hii ya misupu. hapa kwa misupu yeye ndio anacontrol kubwa ya nini kiende hewani na nini kisione mwanga wa jua (hii 'kauli' yako misupu nimeipenda).

    Nimejaribu kutembelea page kuhusu Tanzania ktk wikipedia ya kiswahili na ile ya kiingereza. nimegundua kwamba ile ya lugha ya Kiingereza, imesheheni taarifa nzuri na makini ukilinganisha na ile ya 'kimatumbi'. ni dhahiri kwamba page ya kiswahili imekosa wachangiaji na imejikuta inakuwa inapwaya

    Michuzi / Ndesa,
    naomba niwape hii challenge ili twende mbele.
    Nyie wawili mmeasha hamasa ya watu kublog. tusiishie hapa tusonge mbele na kuwafundisha wa TZ namna ya kushea 'Vijisenti' vyao vya taarifa mbali mbali kwa kutumia dhana ya Open content.

    naomba nitoe mchango wangu wa vijisenti

    Kubwa la Ma-Annony

    ReplyDelete
  5. Ndesanjo shimboni mmeku. Ke njiwia mboni tza ifo huye bana. njikundi na inyi icha sanja meso. Otherwise big up man coz unatuwakilisha vizuri sana mkuu.

    Mdau wa kwenye sky

    ReplyDelete
  6. AnonymousMay 25, 2008

    Anoni mmoja ameuliza hapo juu:
    mmoja anisaidie hivi huwa wanalipwa na nani, au wanapataje faida? sijui nauliza, mtu asinitukane tafadhali, maana kufanya kazi hiyo si mchezo.

    Jibu: Hakuna mtu anayelipwa kuchangia Wikipedia. Ni kazi ya kujitolea kutengeneza kisima cha maarifa kwa ajili ya wanadamu.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...