MWANDISHI Mwandamizi na Mratibu waHabari na Matukio wa televisheni yaITV na Radio One, John Mndolwa (46),amefariki dunia leo alfajiri majira ya saa 10 baada ya kuugua kwa muda mfupi.

Kwa mujibu wa habari zilizotolewa naMkurugenzi Mtendaji wa ITV na Radio One, Joyce Mhaville, marehemu Mndolwa alilazwa hospitali ya Kairuki kwa wiki moja. Kifo chake kimesababishwa na shinikizo la damu.
Mndolwa ambaye alizaliwa Novemba9,1962 mkoani Tanga alianza kazi za uandishi mwaka 1980 katika Idara ya Habari ya Radio Tanzania (RTD) na aliajiriwa na ITV na Radio One Julai 1994.

Mipango ya mazishi inaendelea kufanyika. soma zaidi habari hii ya kuhuzunisha kwa kwenda lukwangule.blogspot.com


Mungu ailaze mahala pema roho ya marehemu - AMINA


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 12 mpaka sasa

  1. Michuzi shukrani kwa kututaarifu hili, hii imenistua sana.Mungu aiweke roho yake mapumzikoni na aipe nguvu familia yake.

    ReplyDelete
  2. Du!RIP Mndolwa....Mungu awape nguvu familia yako.

    ReplyDelete
  3. Bwana ametoa na Bwana ametwaa.
    poleni sana Ndugu wafiwa tupo pamoja katika kipindi hiki kigumu kwenu kwa kuondokewa na mpendwa wenu nyie mlimpenda Mungu kampenda zaidi

    katochi

    ReplyDelete
  4. R.I.P. Brother.

    SteveD.

    ReplyDelete
  5. Duh!!mungu amlaze pema peponi marehumu,, alinisaidia sana katika maswala ya uandishi

    ReplyDelete
  6. RIP John,

    Faraja ya Mungu iwe pamoja na wote walioguswa na msiba huu.

    Patrick Kamera.

    ReplyDelete
  7. RIP
    Mungu amlaze roho yake peponi

    Na kama alizaliwa Nov 62 atakua na miaka 45...au ni mimi sijui kucount

    ReplyDelete
  8. Poleni sana wafiwa mimi namkumbuka sana john halikuwa lafiki sana wa kaka yangu mwandishi wa gaziti la michopo mashaka mapunda naye alisha tutangulia.

    ReplyDelete
  9. Mungu ashukuriwe,Pole kwa familia,ndugu na jamaa wa Marehemu.Nilimfahamu Marehemu nimeikitishwa na taarifa za kifo chake, tumuommbee ndg yetu.AMEN.
    Asante Michuzi.

    ReplyDelete
  10. Poleni sana wafiwa namkumbuka sana John enzi za Chakuwajali (chama cha kuwasaidia waliopatwa na hajali tz)alitoa mchango mkubwa sana katika chama yeye na waandishi wengine kina Khlid Mika..
    Mungu akuweka mahali pema peponi Amina

    ReplyDelete
  11. Poleni sana wafiwa nimesikitika kupata habahari hizi. namfahami John miaka mingi sana

    ReplyDelete
  12. RIP John.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...