JK akiwa katika mazungumzo na marais yoweri museveni wa uganda na joseph kabila wa jamhuri ya kidemokrasia ya kongo, ikulu, dar jana ambapo JK aliweza kuwapatanisha viongozi hao ambao nchi zao zilikuwa zimewekeana bifu kwa muda mrefu. pamoja na mambo mengine viongozi hao wamezungumzia ufunguzi wa ofisi za kibalozi katika nchi zao habari kamili bofya hapa

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 17 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 12, 2008

    I think its time JK kumpatanisha Maalim Seif na Karume. CCM need to stop political spin.

    Mpasuko wa kisiasa ndani ya Zanzibar ni out of touch, wakati nyinyi wakazi wa bara mnaendelea kugonga glass za mivinyo, watoto kadhaa Pemba wanaaga dunia sababu serikali ya Karume inawaadhibu wapiga kura wa Pemba.

    Blaza michuzi, nakupa challange moja tuu, nayo ni wewe kufanya safari kwenda pemba na kupiga picha mitaa ya pemba kisha uje uweke kwenye hii blog, i will contribute travel expenses if necessary. Ni muda muwafaka kuwaonyesha watanzania kwamba Pemba inafanana vipi, wakati JK and CCM play political gatcha game, another child in Pemba is dropping school kusaidia wazazi kufika siku ya pili.

    I feel so sad, sababu majority ya sisi wabara hatuna idea ya Pemba. We think mambo yanakuwa exaggerated kwenye media. Michuzi hiyo ndio challange niliyokupa, plz nenda Pemba na kisha uje uonyeshe wadau dunia nzima wajue Pemba inafanana vipi. I bet next day watanzania tulio nje na walio nyumbani Tanzania tutaomba fund rise kupitia website kuwasaida watoto wa Pemba.

    I challange all Tanzania popote tulipo kuchukua muda kuwaombea watoto wa Pemba. Kama unauwezo wowote wa kusaidia chochote then take action plz.

    Michuzi wasiliana na mimi kupitia mtanganyika01@yahoo.com
    Michuzi kama kuna non profit organization ya kuaminika ndani ya Pemba plz naomba ni fowardie info zake.

    Mdau wa US Tawi #1

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 12, 2008

    Ni jambo la busara sana ulilofanya Rais wa Tanzania kuwapatanisha hao watu Mungu akupe afya tele na maisha marefu.
    Sweet,
    Arusha.

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 12, 2008

    Mganga Hajigangi...!

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 12, 2008

    Nyani kuyaona ya wenzie, yake hayaoni

    ReplyDelete
  5. AnonymousMay 12, 2008

    Issue ya Zanzibar kafikia wapi mpaka sasa? Aache kutufanya sisi watanzania kwamba ni wapumbavu.

    ReplyDelete
  6. AnonymousMay 12, 2008

    Hapo hakuna kupatana, hakuna chochote! Ni pesa ya 'waafrika inatafunwa' tu! We' utasikia siku chache tu zijazo wamegombana tena. Ni tabu kubwa sana kwa sababu viongozi wengi wa nchi za afrika 'wanawekeza' kwenye migogoro. Migogoro ndiyo 'kula' yao! Kamwe hawafurahi kuona watu wa nchi wanazoziongoza wanafurahia kuwa binaadamu kama wao wanavyofurahia. Wahenga walisema 'Wagombanao ndiyo wapatanao'...siyo 'ndiyo wapatanishwao' Kama ni mapatano ya kweli wangepatana wao wenyewe huko huko kwao wakamuacha Kikwete ahangaike na ya kwake.

    ....Afrika,

    ReplyDelete
  7. AnonymousMay 12, 2008

    KWA KWELI HUYU RAIS WETU NINAMSHANGAA SANA YANI KWA WENGINE YUKO KIMBELEMBELE LAKINI MGOGORO UNAONUKIA KATIKA VISIWA VYA ZANZIBAR YEYE HASAIDII HILI SISI HALITUINGII AKILINI JAMANI KAMA KWELI ANAPEENDA AMANI YA KWELI BASI ASULUHISHE WAZANZIBAR KATI YAA UNGUJA NA PEMBA LA SIVYO ATAENDELEA KUSULUHISHA KW MJIRNI HUKU KWKE NYUMBA INAUNGU KUWA NA AAKILI WEWE JK..............CHA MZAHA WWA KUCHZEA SHILINGI CHOONI HATUTAAKI VITA..TUNASEMA HTUTAKI VITA

    BY GEBO ARAJIGA
    ARUSHA-TANZANIA

    ReplyDelete
  8. AnonymousMay 12, 2008

    Wewe unayesema Michuzi apige picha Pemba watu waone hali ya maisha ilivyo mbaya Pemba kwenye hii blog hujui usemacho.

    Kwa taarifa yako vijiji vingi tu vya tanzania bara vina hali mbaya kuliko huko Pemba.Kwa nini akapige picha za Pemba aache za Vijiji vya Tanzania bara?

    Hali ngumu ya maisha iko Tanzania nzima na si Pemba tu! Hata kijijini kwa Michuzi na Kwa Kikwete wana hali mbaya kuliko Pemba sasa unasemaje nao waende umoja wa mataifa wadai vijiji vyao vijitenge na Tanzania? viwe kama visiwa vya Comoro na Anjuani? Au picha zao zipelekwe umoja wa mataifa kama za Pemba mnazotaka zipelekwe?

    ReplyDelete
  9. AnonymousMay 12, 2008

    Ama kweli wahenga walisema "Jivuli la mvule, hufunika walombali" Haiyumkiniki, Kikwete ayaone ya Museven na Kabila, lakini hayaoni ya Maalim Seif na Amani! Duh au ndo "Nyani haoni..."
    Lakini waswahili wanasema "Mzarau biu, hubiuka yeye"

    ReplyDelete
  10. AnonymousMay 12, 2008

    KAMA KIKWETE,KAGAME NA KABILA A.K.A (KKK)

    ReplyDelete
  11. AnonymousMay 13, 2008

    KIKWETE, KAGAME, KABILA, KAGUTA AND KURUNZIZA (KKKK)

    ReplyDelete
  12. AnonymousMay 13, 2008

    KIKWETE, KABILA, KURUNZIZA, KAGAME, KAGUTA, KIBAKI, KARUME

    ReplyDelete
  13. AnonymousMay 13, 2008

    MKAPA,MWANAWASA,MOI,MULUZI,MUTHARIKA,MUSEVENI,MREMA,MFISADI ETC

    ReplyDelete
  14. AnonymousMay 14, 2008

    We anony unaeandika Kikwete sijui Kabila and so so so ...

    Acha kutuchekesha . Unamaanisha nini hapo?

    Tehe tehe tehe tehe tehee

    ReplyDelete
  15. AnonymousMay 14, 2008

    Anony unayetaja majina ya maraisi acha kutuvunja mbavu

    Ala wewe Joti nini? au Masanja Mkandamizaji?

    ReplyDelete
  16. AnonymousMay 14, 2008

    MAKAMBA, MAGUFULI, MWANDOSYA, MWAKYEMBE, MASHISHANGA, MPOROGOMYI, MIZENGO, MAGHEMBE,

    ReplyDelete
  17. AnonymousMay 18, 2008

    Kambarage , Karume, Kenyata , Kaunda , Kamuzu , Kwame , Kwetu ( Masire Botwasna)Kukung'wendo (Mobutu)

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...