Familia ya Victor V. Mujwauzi Karugaba wa Arusha inawashukuru wote walioshiriki kwa hali na mali katika kumuuguza, kumsafirisha hadi kumzika kaka mpendwa marehemu Valery Valentine Karugaba aliyefariki tarehe 29 April 2008 katika hospitali ya St. Elizabeth Arusha kutokana na "Low Blood Pressure" na kuzikwa tarehe 1 Mei 2008 Dar es Salaam.


Shukrani za pekee ziwaendee madaktari na wauguzi wa hospitali ya St. Elizabeth Arusha, Wafanyakazi na uongozi wa Impala Hotel, wafanyakazi wa University of Dar es Salaam Computing Centre-Arusha branch, majirani, marafiki na ndugu na jamaa wote. Ni vigumu kushukuru kila mtu zaidi tunaomba Mungu awazidishie.


Mpaka mauti inamchukua marehemu alikuwa mfanyakazi wa Impala/Ngurdoto Hotel upande wa mapishi ya kichina. Marehemu pia amewahi kufanya kazi katika Hotel mbalimbali ikiwemo Kilimanjaro Hotel, Hotel Karibu, Walk Guard Hotel n.k.


Marehemu atakumbukwa sana kwa ucheshi na upendo wake hasa kwa wale waliosoma naye Mlimani primary school na sehemu nyingine mbalimbali.Marehemu ameacha mjane na watoto watatu."sisi tulimpenda lakini Mungu alimpenda zaidi"


Misa ya shukrani tarehe 10/5/2008 katika kanisa Kuu la Mt. Theresia wa mtoto Yesu- Arusha saa 1.00 asubuhi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 08, 2008

    Professeur Karugaba,

    Je l'écris avec les condoléances les plus profondes pour la mort de votre fils. Dieu donne et emporte. Peut Dieu endurer pour toujours. Je prierai pour vous et votre famille

    Est Rose

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 08, 2008

    Poleni sana wafiwa,kazi ya mungu haina makosa,marehem ninamkumbuka sana wakati tunaishi pale Ubungo Kibangu,alikua mtu wa karibu yangu sana,Pole sana Victor kwa kumpoteza Brother wako pekee.RIP.Mdau London.

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 09, 2008

    Hi Victor,

    Poleni sana na msiba, nimestuka sana kusoma habari hizi.
    LUZANGO-PTRETORIA.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...