Mkurugenzi Bodi ya Utalii Tanzania (TTB),Peter Mwenguo(Kulia)akikabidhi bendera ya Tanzania kwa Miss Universe Tanzania 2008,Amanda ole Sululu jijini Dar es Salaam kabla ya kuondoka kwenda Vietnam kushiriki mashindano ya Miss Universe,katika nchi mbalimbali duniani. Mashindano hayo yanatarajiwa kufanyika Julai 14 mwaka huu katika mji wa Nhatrang nchini humo. katikati ni mwandaaji wa mashindano,Maria Sarungi. mtembelee lukwangule kwa habari motomto na mapicha kama haya kwa kubofya hapa

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 7 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 17, 2008

    Mtoto mzuri

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 17, 2008

    AAHH! BONGO NAO MMEZIDI SASA NAONA HAKUNA CHA MAANA CHA KUFANYA MIAKA HII, KILA SABABU ITATAFUTWA YA UMISS FULANI, UMISS FULANI. WAJAMENI KWANINI MSIWE KAMA ZAMANI KUWA NA UMISS TANZANIA TU. AMBAYE ATAKWENDA KUWAKILISHA KWENYE UMISS WORLD?

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 17, 2008

    Tumechoka na mambo ya u miss. Michuzi mbona habari nyeti huto humu, kama zilizotolewa magazetini CHENGE na KATIBU wamekutwa wakifanya mambo ya UCHAWI bungeni. Na kesi ipo POLICE?

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 17, 2008

    pamoja na umiss-bongo na ushirikina wa mzee vijisenti, lakini tusisahau kuwa Mkapa hajajibu maswali yetu, husasan kuhusu ukwapuaji wa mali ya umma ya kiwira. Huu umiss na vikolombwezo vyake visitusahulishe masuala ya msingi ya maendeleo.

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 17, 2008

    atarudi kama richa adhia,na kukazania kusema walikua racists kama basila mwanukuzi. mi nipo hapa nasubiria

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 18, 2008

    Amanda huitwi Ole Sululu bali wewe waitwa Amanda Ene Ole Sululu.Wamasai wenzangu hapo mpo?

    ReplyDelete
  7. AnonymousJune 18, 2008

    NENDA KATALII DADA URUDI NA ZAWADI..ASHE NALE

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...