Pastor Abisalom Nasuwa,wa Dallas Texas anapenda kutangaza kifo cha baba mzazi wa mke wake Esther Abisalom Nasuwa kilichotokea katika hospitali ya KCMC Mkoani Kilimanjaro juzi siku ya jumatatu saa tatu usiku.
Mipango ya mazishi inaendelea kupangwa huko Moshi.

Kwa kuwa kutokana na sababu mbali mbali pastor Abisalom na mke wake hawataweza kusafiri kwenda nyumbani kwa mazishi,kutakuwa na ibada nyumbani kwao siku ya ijumaa jioni kuanzia saa moja kamili.
Tunapenda kumkaribisha kila mwanajumua aliyeko hapa Dallas na sehemu mbali mbali ambao wataweza kuungana na familia hii wakati huu mgumu wanaopitia.
Anuani ya nyumbani ni;

7311 Otomi Street,
Dallas Texas 75236.

Kwa watakaopenda kuwapigia simu na
kuwafariji namba zao ni hizi;

Pastor Abisalom Nasuwa 214 554 7381
Esther Nasuwa (Mrs) 972 896 6228
Res; 972 780 2668.

Karibuni sana na Mungu atubariki sote.
Mdau

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 11 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 12, 2008

    Dah hii wadau haijatulia "...anapenda kutangaza kifo.." ninavyoelewa anatakiwa aseme ...ANASIKITIKA KUTANGAZA KIFO etc etc.
    Anyway poleni wafiwa

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 12, 2008

    Poleni kwa msiba. Ila kwenye msiba watu hawasemi ANAPENDA KUTANGAZA KIFO, bali tunasema ANASIKITIKA KUTANGAZA KIFO. Msiba si furaha. Nawakilisha.

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 12, 2008

    Pole sana kwa wafiwa wote. Mungu ailaze roho ya merehemu mahali pema peponi.

    Bro Michuzi,swali la kizushi kwako: Pastor Abisalom anapenda kutangaza kifo au anasikitika kutangaza kifo?

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 12, 2008

    Pole Esther, na family.
    rafiki Zanaki and Msange JKT!
    Kumbe ile dili ya jeshi ilifaa hadi ikawa endelevu. Hongera sana.

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 12, 2008

    poleni
    inatakiwa kuwa MNASIKITIKA KUTANGAZA KIFO
    Please rekebisha tangazo

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 12, 2008

    Mchuzi yeye kapewa abandike, kazi yake sio ku edit matangazo, mpeni break kaka wa watu!

    ReplyDelete
  7. AnonymousJune 12, 2008

    baba mzazi "ESTHER"?? kidogo nimekwazika na jina au ni mama mzazi? pleni na msiba anyaway!

    ReplyDelete
  8. AnonymousJune 12, 2008

    Poleni sana wafiwa lakini hata mimi tangazo limeniumiza kichwa kuelewa nilishngaa huyo mkwe aliyefariki ana jina kama lake? Yaani yeye akioa anabadilisha jina anafuta la mkewe? Sikuelewa kabisa "kutangaza kifo cha baba mzazi wa mke wake Esther Abisalom Nasuwa wakati mtangazaji mwenyewew anaitwa the same name...

    Poleni ni wakati mgumu huu lakini naamini Mungu atawapatia nguvu

    ReplyDelete
  9. AnonymousJune 13, 2008

    JAMANI MIE SIONI CHA AJABU AKISEMA ANAPENDA KUTANGAZA KIFO!!MAANA ALIYEKUFA MUNGU ANAMPENDA SANA NDIO MAANA KAMCHUKUA!!NDIO MAANA YA KUSEMA ANAPENDA KUTANGAZA..MAANA MUNGU NI MKUBWA KWA KUMCHUKUA HUYO MZEE WAO...HAINA HAJA YA KUBADILI TANGAZO MEELIELEWA ACHENI KUOSHA VINYWA...POLENI SANA WAFIWA

    ReplyDelete
  10. AnonymousJune 14, 2008

    Poleni sana. Lakini Jamani wabongo tunazamia mpaka tunashindwa kurudi nyumbani kuzika wazee. Hii mbaya sana. Michuzi toa hii comment yangu usi ibanie. Tumezidi.

    ReplyDelete
  11. AnonymousJune 17, 2008

    wasamehe bure kutorudi kuzika nikwamba wameoza wakitoka tu kurudi labda mihujiza ishuke na bingu iteremmuke, unajua hawa watu wa majuu wameoza almost wote hawajuhi kuwa mambo yote bongo!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...