GLOBU HII YA JAMII INAUNGANA NA WANAHARAKATI WOTE WANAOLAANI NA KUPINGA WALE WOTE WENYE UKATILI NA FIKRA POTOFU WANAODHURU NDUGU ZETU MAALBINO KWA IMANI YA KISHIRIKINA.
MWITO UNATOLEWA KWA WADAU WOTE KUWAFUCHUA WAOVU HAO ILI WASHUGHULIKIWE KISHERIA. HII NI AIBU KWA TAIFA KWANI LINAPAKA MATOPE JINA ZURI LA TANZANIA. WADAU MNA MAONI GANI JUU YA HILI NA NI HATUA GANI ZICHUKULIWE KUKOMESHA KUFURU HII?
HEBU SOMA LINK HIYO HAPO CHINI UONE TUNAVYOJIPAKAZIA HUKO NJE

http://www.nytimes.com/2008/06/08/world/africa/08albino.html?bl&ex=1213070400&en=751c11f3322c497f&ei=5087%0A

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 11 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 11, 2008

    kWA KWELI HAWA WATU WANAOSHIRIKI VITENDO VYA KUWADHURU MAALBINO HAWANA LOLOTE LA MSINGI ZAIDI YA SABABU ZA KISHIRIKINA TU!NAWALAANI SANA WATU HAWA.HAKUNA JINA LINALO WAFAA ZAODI YA KUITWA WAUAJI!HIVYO BASI SHERIA INAYO KABILIANA NA WAUAJI NADHANI INAELEWEKA!1NI "DEATH PENALTY" MAANA NAAMINI KABISA HAKUNA HATA MMOJA KATI YA WATU HAWA"WAUAJI"ANAYEFANYA JAMBO HILO BILA YA KUKUSUDIA!WOTE WNA MAKUSUDI MAZIMA NA WANAJUA FIKA KAMA WANACHO KATILI PALE NI ROHO YA MTU!BINADAMU MWENYE KILA HAKI YA MSINGI YA KUISHI KAMA YEYE!NAWA LAANI VIKALI WATU HAWA!NASHAURI IKIBIDI IANZISHWE KAMPENI KALI YA KUTOKOMEZA JAMBO HILO KUPITIA KWA VYOMBO VYA HABARI,TAASISI MBALIMBALI ZA KUSIMAMIA HAKI ZA BINADAMU ,WASOMI NA WADAU MBALIMBALI WANAOPINGA VITENDO VIOUVU KAMA HIVI!!

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 11, 2008

    BINADAMU NI WATU WA AJABU SANA KWA NINI UMDHURU BINADAMU MWENZAKO KISA NI ALBINO.NADHANI SERIKALI IPITISHE SHERIA KALI SANA KWA WATU WOTE WANAOWABAGUA MAALBINO NA KUWADHURU.

    KAMA UWEZI KUMDHURU MNYAMA SASA KWA NINI UWADHURU MAALBINO.

    POPOBAWA

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 11, 2008

    Hii inatia uchungu sana kuona roho za ndugu zetu zinadhulumiwa na washenzi wachache wenye uchu wa utajiri bila kutoka jacho. Mimi nadhani wauaji pamoja na washirika wao (waganga wa kienyeji matapeli)wanafahamika ila tunawaficha kwa hiyo nashauri hapa tuache blaa blaa na tunatakiwa kuanzisha msako wa nyumba kwa nyumba ili kuwatokomeza hawa washenzi kwani hakuna mtu mwenye haki ya kukatisha maisha ya mwenzake kwa tamaa ya utajiri.

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 11, 2008

    bwana michuzi habari yako,ndugu yangu naona baada ya muda si mrefu blog hhi ya issamichuzi.blogsport.com itakuwa yako wewe na baadhi tu ya wapenzi wa liverpool au bwawa la maini kama mnavyo jiita, juzi kati takribani kama wiki nimekutumia habari pamoja na picha za wadau wa soka wa Man.Utd walivyofanya party yao ya kusheherekea ubingwa wa ligi kuu na Champions ligi lakini hadi leo sijaona hata picha moja au hata habari yeyote kuhusiana natukio lile.

    hii inatukatisha tamaa sisi ambao si washabiki wa Liverpool na itafikia wakati mtu akitaka kujua mambo ya liverpool aje kwenye blog yako sio vizuri

    jana tu umeanzisha au kutoa taarifa kuhusu tawi la liverpool hapa bongo leo umeshafiaka mbali hii inathibitisha jinsi gani ulivyo mmbinafsi.

    jaribu kuwa kati na kila mtu atakubali web yako toa habari za party iliyofanyika Sinza najua picha unazo usisingizie mambo ya SULLIVAN SUMMIT.

    ReplyDelete
  5. HAWA NDIo WAZUNGU WETU MUNGU ALIOTUJALIA. NDIO WAWEKEZAJI HAO WENGINE MNAOWATUKUZA NI WANYONYAJI. TUNATAKIWA TUTUMIE BUSARA ZAO KIUKOMBOA HII NCHI NI RAFIKI ZANGU WAKARBU SANA NA TUNAMIKATI MINGI YA KIISAIDIA NCHI TUTAITOA WAKATI WOWOTE. BWANA L-M-O HAPO MOSHI, NIMEFIKISHA UJUMBE USIHOFU FUNGU LITATOKA, HAYA MABO YA KUTUINGIZA MKENGE MKUTANO NI KWA AJILI YETU PESA YA MKUTANO WANAKINGA WAO.CONFRENCE CRUSHER HAPA

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 11, 2008

    Biashara pasipo wateja inakufa/inafilisika

    - Hii ina maana Waganga wa kienyeji wanaotumia ushirikina (ili kutofautisha na wale wa miti shamba) wana wateja ndio maana wanaendelea kushamiri na kukua.

    - Kwa maana hiyo basi, ni ngumu kuwafichua hata kama watasema kaue Albino ama kachune ngozi ya fulani

    - Kwa ufupi ni kwamba, waTanzania wengi wanakumbatia mambo ya ushirikina, kuanzia kupata cheo, kushinda nafasi fulani katika uchaguzi, kushinda mechi, n.k ingawa si rahisi kukiri hadharani

    - Hivyo, nashauri MaAlbino wenyewe waanze kwa kuunda kamati yao ambayo itatafuta hao waganga na kuwachukulia hatua ambayo wao wanaona inafaa.

    Ni maoni yangu tu

    ReplyDelete
  7. Wadau
    Hebu jiweke kwenye nafasi yao kama vile wewe ni albino. Yaani unatembea mitaani huku ukijua kwamba kuna mijitu inakuwinda tena ikuue utaishi katika hali gani?

    Hii mijitu miuaji iteswe sana bila kuuwawa, kata mikono na miguu kisha toboa macho halafu unaliacha liishi lione adha ya kuwa mlemavu maana hawa wanaowawinda (maalbino) nao ni walemavu jamani tuwaoneeni huruma maana jamaa wanaishi kwa tabu sana kwa sababu hawawezi kuhimili jua, lazima awe na kofia, miwani ya jua na kuna wafuta fulani wanatumia kwa ajili ya ngozi zao.

    ReplyDelete
  8. Halafu sisi tunalalamika sana tukibaguliwa na kuonewa huku nchi za wenyewe, kumbe na sisi bado tunabaguana na kuuana wenyewe kwa wenyewe...Aibu sana hii!

    ReplyDelete
  9. AnonymousJune 12, 2008

    Nilikuwa kazini watu wakaona hiyo kwenye gazeti, wakaja kuniuliza whats going on huko kwenu? kwa nini wanafanya Unyama huu, Mwanangu Nooooma.Serikali do something, AIBU huku,tunaharibu sana.
    Usa.

    ReplyDelete
  10. AnonymousJune 13, 2008

    hao watu dili wewe, ngozi yao inauzwa bei mbaya kishenzi huku tuliko

    ReplyDelete
  11. Mungu mwenyezi alituumba wote sawa, na kwa sababu hiyo hakuna aliye na haki ya kuchukua uhai wa awaye yeyote yule kwa sababu yoyote. Kitendo cha kumwua MLEMAVU WA NGOZI {Albino} ni kinyume na amri za mwenyezi mungu. Watu hawa wataadhibiwa tu, na siyo mpaka siku ya kiama BALI Wakati huu tuishio. Nawapa pongezi watu wote, Taasisi na asasi za serikali na zile zisizo za serikali kwa juhudi zao ya kutokomeza mauaji dhidi ya Albino. NINASHAURI PIA Taasisi na asasi hizo zielekeze juhudi hizo pia dhidi ya mauaji ya watoto wasiozaliwa {UTOAJI MIMBA} Kwani ni unyama kama ule wa kumwua Albino. By Gabriel George gabryzach@yahoo.com

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...