kikosi cha yanga kikipozi ndani ya wanja la maracana huko brazil mwaka 1974. waliokaa tokla shoto ni bona max, maulid dilunga, michael clement, moshi dayan na gibson sembuli. waliosimama toka shoto ni satchmo, athumani kilambo, elias michael, said sanga, abdulrahman juma na omar kapera. hiki ndicho kikosi kilichoiliza simba nyamagana mwaka huo wa 1974, mara baada na wao kutoka katika ziara ya poland. wanaokumbuka historia zaidi watumegee

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 9 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 12, 2008

    katika heavyweight boxing,gazeti,la ring magazine linasema,thriller in manila,ambapo muhammed ali alizichapa na fraizer ndio lilikuwa pambano la mwisho la maana katika uzito huo,baada ya pambano,mabondia wote walilazwa hospital,katika soka ya tanzania,nikimnukuu my late father,hili game halijawahi tokea tena,Tanzania stood still on the day of the game,almanusra jini la yanga limuuwe mchezaji wa simba(sikumbuki jina,wadau nikumbusheni)

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 12, 2008

    Kwa hakika Elias Michael is the guy in black lakini naona hapa kaandikwa wa tatu waliosimama nyuma kitu kinachonifanya nitilie mashaka uhakika wa majina mengine...

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 12, 2008

    wako wapi Kitwana na Sunday Manara???

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 12, 2008

    UBINGWAAAA UBINGWAAAAAAAAA!!!!!!!!!
    WA YANGA!!! WA YANGA!!!KAJA MARA!!! GOLI SABA!!! NTOMOKO GOLI NNE!!!MIEMBENI GOLI MBILI!!!NA SIMBAA!!!! YALEYALE,B4 ELIAS MICHAEL NI HASSAN GOBOSI MAJINA YOTE NI SAWA NA MNDAU HAPO JUU WANAOCHEZA NI WATU KUMI NA MMOJA TU KITWANA,SUNDAY,WALIKUA MARIZEVU BRAVO MICHU MDAU KUTOKA CARDIFF NAOMBA PICHA ZA YOUNG KENYA,GREEN EANGLE,CITY BOYS,NUNGU,WONDER BOYS,KABAKA YEKA,POOL ENGLAND,SCOTLAND YARD,BLACK BROTHER NK.

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 13, 2008

    waliofariki ingekuwa vizuri ungeweka neno la heshima "marehemu" mbele ya jila lao. Kwa mfano marehemu maulid dilunga aliyefariki hivi karibuni.

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 13, 2008

    Michu, thanks for the pic.Imenikumbusha mbali sana. Bona Max was a good friend of mine. Nimesoma nae seco Form 1 to Form IV pale St Joseph's Dar.

    ReplyDelete
  7. Ah! Kaka Michuzi umenikumbusha mbali sana. Nakumbuka enzi hizo nilikuwa mtoto mdogo pale Ilala, Iringa Street. Watani zetu Yanga walipita mitaa ya Ilala kwa mchakamchaka huku wakiimba; " Simba karuka mpaka Poland, kurudi Mwanza kala magoli!" Tafadhali, wakumbushe watani zetu kipigo cha goli 6-0. Siku, tarehe na mwaka! Kama huna muda nitaifanya kazi hiyo na kukutumia data zote ikiwa ni pamoja na picha!

    ReplyDelete
  8. AnonymousJune 14, 2008

    Mdau Anonymous from Cardiff ,umetaja Wonder Boys, Kabaka Yeka, Black Brothers,I know wengi hawajakupata ,lakini mimi nimekupata fresh. Tonaongelea enzi hizo au sio, I mean way way back. Najua na Michu nae amekupata kwa sababu na yeye mtoto wa town vile vile. Anyways Elias of Wonder Boys and then Yanga was a friend of mine ( tumecheza ndiki pamoja michangani)you know what I mean ! and so was Willy Mwaijibe of Black Brothers and later on Simba. Anyways ghetto siku hizo Magomeni. We actually had a house across the street from Black Brothers. This stuff is for the books my brothers !!

    ReplyDelete
  9. waliosimama ni athaman kilambo,hassan gobbos,elias michael,seleman said,abdulrahman juma,omar kapera. waliochuchumaa ni kulia gibson sembuli,moshe dayan,mwinda ramadhani,maulidi dilunga na bona max. kitwana manara, sunday manara walikuwa wako reserve. kassim manara na kina adolph pondamali tostao wako bado yanga kids. kuhusu black brothers nawakumbuka kina willy mwaijibe nk. pia kuliwapo timu kama tambaza, avengers bak then.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...