Brother Michuzi.
Hivi karibuni nilitembelea Lukuledi wilayani Masasi mkoani Mtwara. Nikakuta wenyeji wa huko bado wanakula Panya na wanawapenda sana tu.
Hivi karibuni nilitembelea Lukuledi wilayani Masasi mkoani Mtwara. Nikakuta wenyeji wa huko bado wanakula Panya na wanawapenda sana tu.
Nilipowauliza kama ni kwa sababu ya ukosefu wa nyama zingine,walisema Hapana, nyama zingine ikiwemo ya ng’ombe ni nyingi. Ila wanakula panyakwa ajili ya HAMU TU.
Siku hizi panya hawa hawaitwi tena “Yeila” au “Atoro”, baliwanaitwa MKANDA NJE kutokana na kambainayofungwa katika kila fungu ndio wanaifananinsha na mkanda.
Fungu moja linauzwa shilingi 200/= na kila fungu lina panya watano. Ifahamike wazi kuwa panya hawa wanaoliwa sio wale wanaokaa ndani ya nyumba bali hawa huchimba mashimo porini na hukaa huko maporini kwenye mashimo yao.
Yaani hawa ni panya mwitu a.k.a 'samaki nchanga'
Mdau
Perez.
mdau perez!
asante perez kwa nyuzzz hizi na picha. mie mwenyewe mate yananitoka. naendelea kukaribisha wadau kutuletea vitu kama hivi na vinginevyo toka kila pembe ya dunia isomwapo globu hii ya jamii. tuma kupitia issamichuzi@gmail.com. msisahau salamu, nondozz na kadhalika....
-michuzi
WOW! nakumbuka mbali sana, unajuwa nafurahi sana kuona watanzania nasi tunaweza kujua milo yenye protin zakutsha,
ReplyDeletekulingana na taarifa za kitaalamu nikwamba panya wapo katika jamii ya wanyama wenye redmeet.
Pia wataalamu wanasema wadudu kama SENENE, KUMBI KUMBI, MENDE, INZI, NA BUIBUI NI JAMII MOJA PIA.
kwahiyo wazee kama mtu anakula panya kwake nisawa akila pia kima,mbuzi,kondoo na wanyama wa aina hiyo.
nawale wanaokula kumbikumbi na senene wanatakiwa kula pia panzi, inzi, na hasa mdudu mnono mende.
just kuproove mmonyeze mende bonyeee, then kumbi bonyeeee, then senene bonyeeee utaprove ninalolisema.
nihayo tu,
G7
UK
dah!!!, hivi vitu bana...acha niwaachie wenyewe.
ReplyDeleteBooSt3D.
Lo ! hata mimi mate yananitoka. Nasikia ni watamu sana hasa hasa kwa kulia na ugali wa mhogo.kau kau kau,tamu sana .
ReplyDeleteTuache utani jamani. Hii mboga ni tamu kichizi yaani ni bora shinda nyama ya mbwa ama paka wanazokula wahehe. Kazi nzuri sana Kaka Michuzi!
ReplyDeleteYangu macho. Unajua kila kabila duniani wana mambo yao. Wa-Japan wanakula KILA KITU kinachotoka ndani ya bahari...wanakula KILA AINA YA MNYAMA WA BAHARINI, SAMAKI NA WANACHOITA "SEA WEED". Wanachukua mimea ya aina yote ya baharini mpaka ile ambayo inasadikiwa kua ni sumu lakini wao wanajua namna ya kula...Ukiiga....utapasuka msamba...!! Ukitaka usalama...kwa wale wanaotembelea "hasa nchi za Asia" huko Japan, Indonesia, Phillipines, Taiwan, China, Korea na nyinginezo; we sema tu ni Vegeterian..la sivyo.."UTAKULA SAMAKI NCHANGA"...!! Asanteni...!!
ReplyDeleteTobaaaaa! Alosema binaadamu wote ni sawa alikosea, alipaswa kufafanuwa usawa huo ni katika nyanja zipi?!!!
ReplyDeleteHivi jamani mnakula panya kwani kuku, mbuzi, ng'ombe au kondoo hakuna huko kwenu eeeh??
Si naskia kuna bahari huko, au hata samaki wameisha???!!
Ama kweli alojisemea mwenyewe Michuzi "kizuri kwa bata mzinga hakiwi kuzuri kwa kuku"
Mashariki ya mbali huku tunakula vitu vya ajabu zaidi ya panya wa huko Ntwara.
ReplyDeleteKwa hiyo big up kwa wadau wanaojichana.
Ni vile tu unavyokifikiria kitu basi kinakuwa
Huu ni udaku wa nyama uliozidi mipaka. Njaa zinatusumbua lakini saa nyingine inabidi kufa kiume. Ungetegemea mkoa kama Mtwara uko karibu na bahari kwahiyo alternative ya kula samaki ipo. Panya sio kitoweo
ReplyDeleteMichuzi, hawa YEILA ni watamu mno. Kuna watu wanadhani tunakula sababu ya kukosa nyama. Hapana, kuna ladha ambayo huwezi kuipata kokote ambayo iko kwa hawa ATORO. Niko Dar, ila huwa naletewa wa KUONJA toka Masasi kila inapowezekana - O'C
ReplyDeleteMimi sojawahi kuwala lakini nawaunga mkono walao.Kula tu ilimradi sio sumu.Je walao vyura, konokono. KWA AFYA YETU
ReplyDeletemalisa
wajaju!,njomba nindikumbikila kusu namemne!ndinganje wekunogwa namene na ugwali wa magaga,niko darisalama wa porin hawapatikani leo lajima niwakamate hawa wandani,ji kazi ifanyiki nyawe ngoja nirudi nyumbani nikawatege...
ReplyDeleteWatamu sana, inanikumbusha nyumbani, I cant wait to visit.
ReplyDeleteLICHA YAKUWA LISHE BORA NI DAWA NZURI NA INAZUIA NANIHII
ReplyDeleteMtwara kubwa wandugu sio kila sehemu bahari imefika, hata na hivyo walipo samaki aina nyingine za nyama haziliwi? Mi ni mwenyeji wa Masasi, nikienda kijijini kwetu wenyeji wanakula samaki nchanga kwa raha zao, hawagombwi
ReplyDeleteKusema ukweli vyakula vinatofautiana sana unapotoka sehemu unayoishi/uliyozoea. Kuna watu hapa hapa bongo hawawezi kula utumbo wa mbuzi au kondoo...utasikia ayaaaa (keshaona kinyaa). Ila pia nilishtuka kuona watu wanakula utumbo wa kuku, ilhali wa mbuzi naona sawa.
ReplyDeleteNiliwahi kwenda Zambia, hawa panya wanaheshimika sana kama kitoweo. Pia huko wanakula madudu dizaini ya washawasha na wako radhi uwanyime mboga zote uzijuazo ila hivi viwili usiwanyime.
Haha, watu wanashangaa panya kuliwa hizi ni jamii tu amabzo zinaona panya kama chakula kingine tu, kuna watu wanawashangaa hawa watu lakini mimi nimesafiri sehemu nyingi hapo Bongo watu wanakula panya nitaanza na Mbeya maeneo ya Umalila yaani Mbeya vijijini wanakula sana pany aho, Mbozi kwa wanyiha na Wnadali wa ileje wanakula sana panya hao wakiwa shambani wanawawinda sana na kwenda kuwachoma wakati wa kula ugali mchana, wasafwa wa mbeya wanakula sana panya wa aina hiyo mitaa yote ya uyole wanakula sana hao panya, ukija wasukuma wa kule vijijini magu na kwingineko wanakula sana panya hao, maeneo ya dodoma wilaya ya kondoa kuna watu wanakula sana hao panya ,
ReplyDeleteHuku Nchi za watu
Maeneo ya China mashambani panya ni chakula chao ghali sana kutokana na upatikanaji kuwa mgumu lakini wanapendwa mno panya mmoja nafikia hadi $ 40
Huku slovakia kuna sehemu wanaliwa sana hao Panya tena kwa bei kubwa sana,
Kule kulikokuwa na Euro 2008, Viena kuna maeneo wanafuga ng'ombe kwa wingi kuna mashamba kidogo panya wanaliwa sana na kuwidwa na watu kama vile wnawinda swala kwa hapo bongo,
Ni hayo tu najua wengi wazee wenu wanakula sana panya huko bush mnajifanya kishangaa hapa,
Mdau, HongKong
Wewe Kama Misupu vipi! unakuwa kama vile siyo n-zalendo wa huku
ReplyDeletekusini? HAPO JUU UMEKOSEA UMEANDIKA
MTWARA badala ya NTWARA!
Tafadhali rekebisha ondoa hiyo M na weka N yaani NTWARA
watu bwana mnamatatizo sana kama wewe unakula panya kivyako hakuna anaekuingilia. ila usipende kuweka makabila ya watu wengie toka lini wasukuma tukala panya???
ReplyDeleteau umedata tafadhari sana data kivyako kwanza naona kinyaa hata kuwaona harafu unatia kabila langu wee vipi??
sisi tunakula maziwa na ugali sio wadudu kama panya koma ukomae uwe na adabu siku nyingine usirudie.
wewe ononymous wa hong kong
ReplyDeletewewe ni mzushi hujatembea lolote
naunamazoea ya kitoto kama kwenu mnakula panya basi unazani wote taratibu,
sio watu wote waroho kama wewe kuwa hong kong unakula kila ukionacho utakula na kinyesi cha watu. ila kwa tarifa yako mwanza hakuna mtu anaekula panya toa umbea wako hapa kama huna cha kuongea kaa kimya
Hakuna ajabu au kinyaa, Wachina wanakula mbwa na nyoka, wafaransa wanakula vyura (frogs)- wengine wanakula mijusi, wadudu wa aina mbali mbali. Isipokuwa tu wanyama kama panya huwa na wanaweza kuambukiza magonjwa kama ya typhoid, rabies, n.k. hivyo idara ya afya ihakikishe kuwa hawa panya ni salama kama vile inavyofanywa kwa nyama za n'gombe, samaki n.k.
ReplyDeleteNyoro
chiumbile mulungu cha kumemena, haidhuru almuradi si sumu, ukishangaa ya musa utakutana na ya firaun, kule znz Bwej... kwa kenge vipi maana mpaka mtu anaatoka mabaka ya m-ba kwa kula kenge.
ReplyDeleteBrother michuzi wacha watu waseme but this kitoweo ni bomba mno na ukionja huachi. Nawapa big up watu wa Ntwara especially kule Masasi na nnawakumbusha wanablog kuwa sio Ntwara tu!! maana hata kule Mbozi wanatafunwa kama kawa!! humuambii kitu Mnyiha kuhusu hii asusa.
ReplyDeleteMdau, Brasil!!
Yaani na nyie wengine ati wanasupport sasa ukila panya utapata akili gani kama sio ya panya as well na kuwa mwizi tu ndio maana huko Mtwara maendeleo bao na akili za watu bado zimelala, kumbukeni kuna impact kubwa sana ya chakula unachokula na akili yako kujengeka achilia mbali mwili. Panya wana magonjwa mengi sana related na binadamu na ndio maana wanatumika kama sample katika dawa nyingi duniani. Yote hiyo njaa tu mkija hapa mtamaliza njiwa wote mjini hapa au kule uholanzi wale bata nanii kwenye zile canals ndio itakuwa watasaulika mtu yeyete anayekula panya awezi kupata akili ya maarifa hata siku moja hata kizazi chake.
ReplyDeleteLondoner
Kuna kabila fulani wanakunywa juisi ya kijambo.
ReplyDeleteWakipikwa kwa tui ya kolosho utazimia, ni mboga safi kwa mtandaha/ugali wa muogo. Pnya huliwa na watu wengi sana duniani, niliwahi kuwa CHAD watu wa dini zote hula panya kule tena wanawapenda sana, nyama nyingi sana za aina huliwa duniani, nimewahi kuwa Camerron, watu wa dini zote hula sana nyani, tena wanapendwa sana, London nimeona mwenyewe katika kipindi cha ready stead cook katika BBC hiki kipindi huwa kila siku jioni kama sikosei ni cha local sio BBC international hivyo watu wa huko nyumbani hamwezi kuona walipika nyama ya mamba na kenge watu wakala wakaisifu sana kuwa anafanana na ya kuku, so those things are not something not right, it okay. Chini kuna club/bar watu wanakula sehemu za siri za binadamu huzipata watu sijiuwi lakini nahisi toka hospitali watu wakifariki, nimeona mwenyewe kweye TV DOCUMENTARY watu wakichana sehemu za siri za wanaume.
ReplyDelete