mbiu ya mgambo ikilia, ina jambo. leo ni leo mitaa ya neshno watani wa jadi yanga na simba watapokutana mapemaaaaa, kuanzia saa nane alasiri juu ya alama, kugombea nafasi ya mshindi wa tatu wa kombe la kagame cup ambalo leo linafikia tamati kwa mchezo wao huo, kabla tusker ya kwa watani wetu wa jadi na uganda revenue authority ya ukweni kucheza fainali baadaye saa kumi.
hapa leo bwana hamna cha nini wala nini, mwamuzi ni kipyenga cha mwisho baada ya dakika 90, maana kelele zilizidi mitaani.
nyepesi nyepesi toka redio mbao zinasema timu moja katika hizo itaingia mitini na kukubali kulipa faini ya kutofika mchezoni kwa kile kinachojulikana kama 'heri fedheha, kuliko lawama'.
ah, sie yetu macho na masikio...
tupe matokeo ya yanga na tusker kwanza ndio tutakwambia nani zaidi au ulikua ruvuma na mnazi mkuu wa jangwani akizindua daraja
ReplyDeletengoja nishangae kiluguru, jaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa kwani yanga c bingwa wa kagame na tshirt walishachapisha, sasa mbona unatuuliza nini tena,mkifungwa hauleti matokeo mapema akipigwa mnyama dk 2 nyingi ushaandika tena kwa herufi kubwa MNYAMA KAULIWA TAIFA, michuzi una fitna mzimba ana afadhali,yanga zaidi magazetini ila lunyasi zaidi uwanjani.
ReplyDeleteBro michuzi leo natamani ningekuwepo neshno kwani nazimiss nyimbo zetu na nderemo!!! hapana nakumbuka baadhi tu!!
ReplyDelete1. Mdebwedo, mdebwedo,mdebwedo!
2. yanga wamebana wamebana wameachi... * 3
3. Maneno maneno, siyaweziiiiiii *3
4. OoOo,OoOo,OoOo
5. Msimbaziiiiiiiiiiiiiii dume la mbegu!!!3
musimind wazee ni mtizamo tu.
G7
UK
Simba na Yanga nawatakieni mchezo mzuri,tumesononeka tumeshindwa kulibakiza kombe nyumbani lakini ndiyo mambo ya mpira wa miguu,mzidi kujitahidi.LEO NAWAOMBA MCHEZE MCHEZO MZURI(PROFESSIONAL FOOTBALL),FAIR PLAY.MARA ZOTE MNAKUWA MNAKAMIANA NA KUHARIBU GAME.HAMNA PRESSURE YA KOMBE TENA,SO TOENI BURUDANI.NAWATAKIENI MCHEZO MZURI.
ReplyDeletekaseja ataiokoa yanga leo...kuepuka kuitwa yeboyebo..!!
ReplyDeletedk 90 au 120 zitaamuwa..!
naomba utupe matokeo mapema muheshimiwa misupu....!
mdau sitokihomu!
Hao yanga wamechokaa kama Igembensabo!
ReplyDelete