bitozi siwatu 'runner' akiegemea mojawapo ya ma bmw ya kwanza kuja bongo. enzi hizo ilikuwa ujiko kuibuka na chombo kama hicho hata kama babaa'ko alikuwa hana. asante sana runner kwa mapicha haya ya kumbukumbu ya enzi zenu za ubitozi
matozi ya gerezani yakiwa ymca
ma dj wa enzi hizo toka shoto dj young kim, dj roonie na mr A
kama wewe hukucheza disko mbowe hutambuliki kama bitozi enzi hizo
mabitozi wa gerezani wakiwa disko la ymc enzi hizo



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 22 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 24, 2008

    Dduuh! bwana mdogo katika picha ya mwisho kaanza kujirusha tangu age hiyo.. kweli enzi hizo kiboko. Hawa bongo flava hawana kitu. kujirusha enzi hizo hatakama nilikuwa sijazaliwa.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 24, 2008

    Ranner jamani nimefurahi kukuona humu leo longtime nimekumiss sana swahiba wangu.

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 24, 2008

    Kweli hao ni mabitoz wa longtime, huyo msela wa picha ya nne pembeni ya alieshika kitambaa(dereki) ukimcheki mguuni ana viatu enzi hizo tulikwa tunaziita 'Kung-Fu Shoes' vilikuwa maarufu sana!

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 24, 2008

    Dah enzi hizo, ukikuta demu disco lazima ni mlupo, maana mademu wachache sana walio tulia walikua wanaenda club .

    Halafu ilikuwa fully kujiaachia no worry ya ngoma wala nini, mambo poa tuu, enzi hizo ukinasa na gonjwa ni a quick shot of Penicellin na uko fiti, hakuna mambo ya kucheza salama.

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 24, 2008

    michuzi muongo,toka lini bitoz akatoka gerezani

    ReplyDelete
  6. AnonymousJuly 24, 2008

    wakati huu michuzi,ulikuwa ujadondoka jijini nini?

    ReplyDelete
  7. AnonymousJuly 24, 2008

    dah,mshkaji hata mie kung fu shoes nilikuwa nazo, za bluu. hivi kipi kilianza, kung fu shoes au raba mtoni?

    ReplyDelete
  8. AnonymousJuly 24, 2008

    Aisehh !! pale naona jamaa kaingia disko na viatu vilivojulikana kama "Kungu-Fu" shoes.
    Enzi hizo nilikua bado nina miaka mitano tu.

    Nice one michuzi. Kumbe ndo zako hizi.

    ReplyDelete
  9. AnonymousJuly 24, 2008

    daaamn pembeni ya mshikaji mwenye kung fu shuz, mchizi ana air force.
    that shit is cold!

    ReplyDelete
  10. AnonymousJuly 24, 2008

    anony wa 6;37 huzijui kung-fu shoes kwa sababu kulikuwa hamna za rangi ya blue zilikuwa nyeusi tu,duh ulitaka kutupiga kamba humu humu.

    ReplyDelete
  11. AnonymousJuly 24, 2008

    Aah! mwanangu runner mwanangu, kumbe ulikuwa una BM? wakati huo dada yako "kidoti" alikuwa wapi? Sema nae wangu, nimefurahi sana kukuona, kumbe handsome siku nyingi.

    Dada yako wa Fourways.

    ReplyDelete
  12. AnonymousJuly 25, 2008

    Gerezani ! Gerezani! Anonymous kweli enzi hizo kiboko. Hapo kwenye backyard ya late Abdulwahid Sykes (RIP) ndiyo mwalimu aliwanza reforms za sororities za wakina mama wakislamu na ku intergate them into TANU. Mwalimu peke yake amewapa credit beni and lelemama socities. Kenya ili ban lelemama socities.Hapo ndiyo Bibi Titi (RIP) ali cheza na mama zetu and was inspired by muslim women who were owners of their homes since early 1930's.
    Hapo ndiyo wakina mama wali mgomea Mzee Londo(RIP)kuvunja majumba zao na kujenga NHC and mwalimu agreed with them when he came to inagurate NHC owned by a mama Saidi. Gerezani kama Harlem. Grezania ni Mecca ya waswahili
    Sasa wewe unjua gerezani ipi? Sorry about my bad swahili.

    ReplyDelete
  13. AnonymousJuly 25, 2008

    Hao walikuwepo hapo kuna kina marehemu pia ambao walishatutoka.
    Kuna marehemu SHORTY; Marehemu MAGURUWE; SIWATU, ANU, RUMI, AMITONI , JERRY, ABDUKADI, KITITA, TRAVOLTA, KHALID, BARAZA na wengine mpaka nimewasahau sura zao,.
    Hapo ilikua YMCA Disco Toto Sundays.

    Hapo ninavyokuambia kila mtu kwenye hizo picha ana dischaji buku teyari kuzamia anytime.



    Ezza.

    ReplyDelete
  14. AnonymousJuly 25, 2008

    michuzi, weka picha za Piza enzi za Gymkhana. Watu hawajui watu wametoka wapi bwana...enzi hizo za Pazi, Vijana, Magnet, JKT, BOT, BIMA, na Jeshi (abc).....Mzee wa chama Malai na Kimario.....Runner yuko wapi na Magazeti....

    ReplyDelete
  15. eh michuzi leo umefika mbali, hao jamaa wote nawafahamu majina tu nimeyasau, siwatu na ronnie wakicheza nyuma yupo imani rafiki yake ronnie enzi hizo, hamizi kibwaya, gerry enzi hizo mkitoka ymca disco toto mnauganisha mbowe

    ReplyDelete
  16. AnonymousJuly 25, 2008

    SIWATU yuko wapi siku hizi? mara ya mwisho nilimuona malay freights.alikuwa na besti wake anaitwa OTTO.

    ReplyDelete
  17. AnonymousJuly 25, 2008

    enzi hizo nguo zote za dukani

    ReplyDelete
  18. AnonymousJuly 25, 2008

    naona hapo suruali ni michael jacksson style

    ReplyDelete
  19. masikini!!! nimeangalia tena nmemuona na marehemu shotii RIP

    ReplyDelete
  20. michuzi na yule binti aliyekuwa anaishi mtaa wa kiungani je unamkumbuka?

    ReplyDelete
  21. AnonymousJuly 26, 2008

    Hivi mnazikumbuka kumbi zenyewe? 1.SEA VIEW, MBOWE, BAHARI BEACH, SILIVER SANDS, YMCA na nyingine nyingi tu enzi hizo watu walikuwa wanasema wanaenda BUGI, hii ni dansi ya kuanzia jioni hivi hadi mishale ya saa nne hivi ni ya vijana, na watu waliokuwa wanaenda ngoma wengi sana ni watoto wa uswahili si wa Osterbay kwa watoto wa vigogo walikuwa wanaona kama ni kujidhalilisha kwenda disco yaani kujishusha daraja hivi kuchanganyika na walala hoi, na enzi hizo watu waliokuwa wanaenda Ulaya sana ni walala hoi si sasa watoto wa vigogo ndo wanaong'ang'ania kwenda Ulaya enzi hizo ni mabaharia tu ndo waliokuwa wanaenda Ulaya na kurudi na maguruwe HII NI GARI YA KIFARANSA WASWAHILI WANAIITA PIJOTI 405, ENZI HIZO dar ILIKUWA SAFI NA RAHA TUPU SI SASA.

    ReplyDelete
  22. AnonymousJuly 26, 2008

    oyaaa,anon 5.21 ilikuwa pijo 504,siyo 405

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...