Hayawi Hayawi sasa yamekuwa!!!!!! Alikiba amepania kuwakata kiu washabiki wake wote wa minnesota na vitongoji vyake hapo jumamosi 09/06.
Usisubiri kuhadithiwa hakikisha unajionea mwenyewe The Best in East and Central Africa akiporomosha vibao vyake Cinderella, Nakshi nakshi, Mac muga na nyimbo mpya kama sita zitakazokufanya ukubali mwenyewe kama kijana ana kipaji.
Kwa maelezo zaidi check flier hapo juu ama nenda
Alikibausa.com

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 16 mpaka sasa

  1. i would think huu mwezi mtukufu huyo Ali Kiba anatakiwa kujiswafi....

    ReplyDelete
  2. wewe mdau nani kakwambia mwezi wa ramadhani huruhusiwi kufanya kazi.hiyo nda kazi yake kama wewe unavyobeba maboksi.embu acha kubeba box uonde kama utapata hela ya futari.acheni udaku.
    Mdau

    ReplyDelete
  3. katika dini ya kiislamu music ni haram kabisa. Na yeye kama mtoto aliyezaliwa na Waislamu(wazazi) na akafuata dini ya hiyo ya Kiislam basi huu ndio muda wake wa kuomba toba kwa Allah(sw) nafasi ndio hii hujui kama Ramadhani ya mwakani utakua hai tena pls.

    ReplyDelete
  4. wewe ananymous wa pili please please kabla hujaandika kwanza tumia akili, ufahamu alichosema mwenzio na ndio uandike sio unaropoka tu. Kuna kazi tele ambazo muislamu hatakiwi kufanya mfano ni huo musiki na kuuza pombe au kuitengeneza kiwandani au kwenye vichaka. hizi ni mfano wa kazi ambazo muislamu hatakiwi kuzifanya kabisa! ingawa wapo tele wanafanya, lakini umuhimu wa mwezi huu kwa waislamu hata hao waloamua kutofata amri za usilamu huwa wanaacha kwa muda ni kwa heshima ya mwezi wenyewe na waislamu wenzao na kwa nafsi zao. hii ndio sababu muandishi wa mwanzo alichokuwa anakisema. Najua kuna watakaosema ni maisha yake, lakini kama muislamu ni wajibu wetu kukumbushana. hili limeelezwa bayana kuwa uislamu ni kukumbushana kutenda mema na kuacha mabaya; ingawa inabaki pale pale kuwa ni hiari ya anaekumbushwa lakini ni LAZIMA kwa wanaoona kosa kumbusha.

    Jambo jengine ni kuwa anapofanya hayo maonyesho yake, watu watakusanyika na kufanya mengi ikiwemo kunywa ulevi. katika uislamu tunaambiwa "amelaaniwa mwenye kunywa ule na KILA anaemsaidia". kumsaidia ni toka anaesafisha chupa, anauza, alieweka mahali pa kunywa, alosafirisha pombe hadi hapo panaponywewa, na aliesababisha watu wakusanyike hapo kunywa kwa siku hiyo. kwa maana ali hapo anaingia. kwa sababu watu wote walifika hapo na kunywa wamefika kwa sababu yake, kwa hivyo nae ni mkosa.

    kuna watakaosema kuwa lakini kama wasingekuwepo hapo still wangelikunywa pengine, naam ni kweli lakini hawakuwepo kwengine wamekuwepo hapo kwa sababu maalum nayo ni kumuona ali.

    Waislamu tuzidishe kukumbushana kutenda mema na kuacha maovu. nawatakieni ramadhani karim

    ReplyDelete
  5. Pengine kabadili dini. Mtajuaje ?
    Saa hivi yuko amerika na anatengeneza hella. Wacha afanye kazi yake.
    Hata kama waislamu wanakumbushana, kune wengine wakiwa wamefturu, mambo wanavyofanya ni vya ajabu sana. Mbona hivi? sielewi.

    ReplyDelete
  6. I am sorry mimi sipendi kudebate mambo ya religion b'se I think that is a very person matter and belief but.... hey ....you up there.....unaweza kunambia ni watu wangapi (Muslim people) wameacha kazi zao at the breweries factories/companies just to celebrate the Holly months?


    With this economy? Lets be realistic. Halafu ukishindwa kulisha familia utamlaumu Mungu?

    Mimi ukiniambaia some Muslims don't do those kind of jobs at all to begin with I will buy it....and remember dhambi ni dhambi na hakuna muda ambao ukifanya dhambi itakuwa double charged na wakati mwingine itakuwa single charged....Kama unaona kuimba ni dhambi basi mngemwambia toka mwanzo hiyo kazi haimpendezi muumba .....

    We are all sinners...tusiwe warahisi kupoint fingers kwa wenzetu.

    ReplyDelete
  7. WE ANONY WA 2.01 SASA WATAKA ALI KIBA ALE WAPI JAMANI BILA MZIKI?AU WAISLAMU MNATARATIBU ZA KUCHANGISHANA PESA KWA WATU WENYE SHUGULI HARAMU KWA MWEZI HUU ILI MUWASAIDIE KWENYE ICHI KIPINDI?

    HESHIMUNI KAZI ZA WATU JAMA WE UNAZANI HELA YA FUTARI ATATOA WAPI JAMA?

    ReplyDelete
  8. Kuitwa Ali maana yake sio uislam,hilo ni jina tu.Kuna watu kibao wanaitwa Omari,Asha,Jumanne (J4) n.k lakini sio waisalam na KITIMOTO wanakula.Kwa hiyo mdau wa kwanza,wa pili na wa tatu naomba muulize kwanza Ali Kiba kama ni muislamu au la,au pengine amesilimu alivyouingia viwanja,huwezi jua.Naomba kuwakilisha!

    ReplyDelete
  9. Jamani mwacheni mtoto wa watu! Mi simlaumu hiyo ndo kazi yake, asingekwenda huko Marekani kuna muislamu ambaye angemfidia hizo pesa ili Ali awe kwenye mfungo???? Na hao waislamu wanaofanya kwenye mahoteli ya Kitalii tena kwenye Bar nao wameacha kazi muda huu??? Na wanaofanya Tanzania Breweries na Serengeti beer je?

    ReplyDelete
  10. hawa watu wanao mlaumu ali ni wale wanao uharibu uislamu wanaongezea mambo yao ili watu waiogope dini yetu hii.hebu kila mmoja atulie na dini yake na wengine pia tunawakribisha ktk uislaamu msijali ya hao waosha vinywa ambao wao wanayoyafanya hawayasemi.kama kweli ni waungwana waweke na picha zao tuwaone.uislamu sio mgumu watu ndo wagumu

    ReplyDelete
  11. anon wa kwanza na wa tatu naombeni mtaje kazi zenu zinazowapatia kipato tafadhali!
    mi nataka niwaonyeshe tu ni vipi kazi zenu ninaconnection na maovu
    jiangalieni wenyewe sio kunyooshea watu vidole tu
    mnadhalilisha waisilamu wenzenu ndo maana waisilamu wanadhaniwa hawana elimu kazi kucheza bao, kunywa kahawa, ugomvi na kubishana sababu ya wachache kama nyie

    ReplyDelete
  12. Tungetokea blue nile aisee, ila watu tuna swaum zetu kuja kumcheki huyo jamaa itakuwa ngumu.

    ReplyDelete
  13. i can never understand uisilamu....so i gave up! mara wengine wanasema hivi, mara wengine vile, it is just too confusing!

    ReplyDelete
  14. kuna wengi humu wanauliza au ku debate bila ya point sahihi. Kwa ufupi muislamu kuna kazi hatakiwi kufanya full stop. alouliza tunataka afanye nini, jawabu kuna kazi tele zinazoruhusiwa na dini yake.

    tatizo ni kuwa watu hawapigi kelele kwa waislamu wengine wanaofanya kazi kama kwenye ma bar, viwanda vya bia na kwengineko, kazi ambazo ni mwiko katika dini yetu. hupigwa kelele wakati huu wa mfungo tu jambo ambalo sio sahihi.

    alotaka kujua kazi yangu mimi ni mwalimu, haya nionyeshe connection hapo.

    ReplyDelete
  15. Asiyejua maana usimwambie maana, ni sawa na kumpigia mbuzi gitaa!

    ReplyDelete
  16. Sasa mwalimu inamaana huko uarabuni mabako kila mtu ni mwislamu kila mtu ni mwalimu au huko kwao hamna kazi mnazoziita "Haramu" Bwana msiwaaribie watu na imani zao....Unatakakuniambiwa walimu wote ni watakatifu? Au ualimu ni upi unaouongelea kuna walimu wa aina nyingi tu na wengine ni very controversial too kwa watu wengine...

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...