habari zimeingia sasa hivi zinasema twanga pepeta (juu walipotumbuiza oman) watasafiri kesho kwenda nairobi kwa watani wa jadi kuburudisha kwenye sherehe za miaka 20 ya taasisi ya african economic research consortium katika hoteli ya intercontinental siku ya jumatano. halafu jumamosi yake wamealikwa kutumbuiza carnivore kwenye hafla ya kutangazwa kwa mabalozi wa kampuni moja ya simu, shughuli ambayo ambasadaa lady jd (chini) kaalikwa kutumbuiza pia
mh. ambasadaa wa zain akionesha burungutu lake baada ya kuteuliwa kuwa msanii bora wa kike bongo huko kwa watani wa jadi hivi karibuni

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 14 mpaka sasa

  1. kumbe Twanga mkiwa Umangani mnajua kula pamba za uhakika zenye kuwa fanya watu waliojihifadhi mbele ya mashabiki wa Oman.
    Tunaomba iwe hivyo kila onyesho, tumechoka na ma-tracksuit-trousers.

    ReplyDelete
  2. Twanga bado wajuu bwana ukilinganisha na band zingine maana kwanza wanaalikwa sana na kutoka nje ya nchi mara kwa mara hapo utatambuwa kuwa hawa jamaa wapo juu kuliko waoote.

    ReplyDelete
  3. Michuzi nje kidogo ya mada nina ujumbe kwa dada JD.
    JD:Kwanza hongera sana kwa kuteuliwa,pili umependeza sana kwenye picha.Umevaa kiheshima,umesuka vizuri,'simpo'.Mambo ya kuacha t*mbo wazi,na nguo fupi fupi no Good eeh?.Hapa unaonekana at least una ndoa.Mungu akubariki dada Judy na familia yako.

    ReplyDelete
  4. wewe mama Asha Baraka na familia yako unaeruhusu bendi yako kupiga muziki katika mwezi mtukufu wa ramadhani si Muislamu wewe ?

    ReplyDelete
  5. Balozi Judith Nyambibo Wambura...ukiangalia hii pix nadhani ungepeneda uwe ivyo daily tofauti na kujilundika mamake up kama ufanyavyo..Capt Habash, upoooooooo??
    Hao Twanga inakuwaje ndani ya mfungo kututaabisha, Dada Asha umemeuona mwezi lkn?? ankara zina wakati wake mamaaa

    ReplyDelete
  6. MDAU - DAVID VILLA, Kweli umetoa point hata mimi imenigusa sana, JD umependesa sana kwenye picha hata mimi nimeshangaa kulikoni leo JD kawa smart hivi. JD jitahiji kila mara uwe unavaa vinguo simple kama hiv tofautitofauti, kitovu nje isiwe sanaaa kila mara s'times not always.

    Really so nice in this PIC, really Mwaaaaa dada JD, Ingia tena shop tafuta vinguo vizuriiiii kama hiko.

    JD, Nitafurahi sana kama utabadili Fomula yako ya uvaaji japo kidogooo tu mara moja moja.

    Mshabiki wako,
    SWEDEN.

    ReplyDelete
  7. Asha Baraka anaweza kuwa muislamu lkn labda yeye KOBE.si lazima sababu ni mwezi m2kufu basi kazi nayo isifanyike.

    ReplyDelete
  8. WEEE MSHAMBA..UNAYE MUULIZA ASHA BARAKA ANAPIGA MUZIKI NA MWEZI MTUKUFU SIO MWISLAM.... ULITAKA AKALE POLISI??? UTAMPA WEWE PESA NA PESA YA FUTARI????

    ReplyDelete
  9. ama kweli asiyejua maana usimwambie maana ..wewe anony unaeniita mie mshamba kama ndio asha baraka mwenyewe au familia yako chunga akili wewe .... kwani hiyo twanga ina pesa kiasi gani ? na huo uwezo kakupa nani ? jamani tunafanya ya dunia tusijisahau ! lazima tueleweshane! huyu mama ni muislamu na mekulia katika uislamu kwa hiyo anjua fika huu ni mwezi wenye utukufu wa kiasi gani sio kufanya ufiraubni . miezi ya kawaida khata mimi najimwaga twanga kupepeta lakini lazima tupe ramadhani hadhi yake , sasa kama yeye mwenye bendi ya kiislamu anafanya hivyo unawapa picha gani watu wa dini nyingine ? ina maana sisi hatuujali mwezi wetu ? kwani huo mwezi mmoja ndio watakufa na njaa ? si washukuru na watu wa southern sudan wasemaje ? tena msinitibue kabisa saa hizi , mimi nilikuwa nauliza swali tuu tena la msingi sas usiniite mshamba , labda mshamba wewe na huna upeo wa elimu si ya dunia wala akhera unaeona muislamu kupiga mziki ramadhani inaswihi , mbona mwaka jana hiyo twanga pepeta nakumbuka walipumzika mwezi wa mfungo sasa kulikoni ??!!ama ndio faranga zimekua tamu matokea yake watoto wa kike kukaa uchi stegini na kukatika mwezi mtukufu mama asha tafadhali mama fikiria hilo !! jamani hata kama sisi binadamu ni wajuaji lakini tujitahidi tusimkashifu Mungu tena kwa dhahiri.....haya mwee! Narudia tena mshamba mwenyewe tena usinisababishie nikachafua hali ya hewa humu kwa kak Michuzi na namuheshimu na kunibatilishia swaumu yangu ! Mshamba mwenyewe unaetetea ujinga badala ya kuelewesha wenzio wakikosea . Mshamba weee

    ReplyDelete
  10. UNAONA SASA WEWE..MSEMA KWELI.. MIMI KOBE NAWALA SIFUNGI SASA WEWE UNAYEFUATA HIZO NGUZO ZA UISLAMU MIMI NIMEKUTUKANA MSHAMBA UMENIRUDISHIA TENA MARA NYINGI TUU SASA ULICHOTKIWA NIKUNIELEWESHA MAANA WEWE UNATANGAZA DINI KWELI WEWE NI MWISLAMU KWELI??? UMESHINDWA KUSTAHIMILI TUSI DOGO MWEZI HUU MTUKUFU HA HA HA TEH TEH ... SAUMU YAKO NI BURE NAKUSHAURI KAA KAMA KOBE WA MICHUZI USIFUNGE MAANA NUNAJISHINDISHA NA NJAAA TUU...!! IMANI YAKO USIKOSESHE WATU RAHA BUREEE ASHA BARAKA SIO MTOTO MDOGO NDIO MAANA NAWAPENDA WAZUNGU HAWAPIGIANI KELELE DINI NA HAWASALI NA MUNGU KAWAPA KILA KITU NA ANAZIDI KUWAPA NA WENZIO WAISLAMU HUKU WANAUZA PIZZA ZILICHANGANYWA NA NYAMA YA NGURUWE MWEZI HUU NA NIWARABUA ORIGINAL SIO HAO WABONGO WAKUCHOVYWA UPO HAPOOOO WEWE .. WEWE MWENZANGU ULOLETEWA DINI..MSEMA UKWELI!!! WALIAMBIWA NA WAZAUNGU RUDINI MAKWENU VITA VIMEISHA WALIKWENDA MAKANISANI WAKIA NA KULA HAWAKULA WAKAWAONEA HURUMA NCHII HII IMEJA NGURUWE SUPER MARKRT ZOOOTE NA WAO WAMO AAA BWANA DUNIA HII FUATA IMANI YAKO KAA KIMYA.. UPOHAPO WEE MSEMA KWELI!!!!

    ReplyDelete
  11. Huyo ?anayejiita Msema Kweli!
    ni msema kweli feki,Tafadhali asitumie majina ya watu wengine kutoa maoni! Hii hitaleta vurugu katika biashara ya mziki.
    Msema Kweli mwenyewe halisi hawezi kutoa maneno kama hayo!
    MAMA ASHA BARAKA SONGA MBELE
    ACHANA NA WANAFIKI.
    Ni mimi msema kweli(Halisi)

    ReplyDelete
  12. 1. sijakutukana , kwani kuitwa mshamba kwangu mimi sio tusi , kuna kitu mzungu anasema "figure of speech " na ila tuu sikupenda wewe kuniita mimi mshamba wakati nimeuliza swali tena la msingi.ulinishangaza tuu na ufinyu wako wa mawazo na mameno yako ya kashfa. na kumbuka nasema haya sio kwa kukutukana ni kwa kukuelewesha msimamo wangu.

    2. sijui nikwambie ! maana wewe licha ya ushamba niliokurudishia mwenyewe mimi naona ni upeo wako wa elimu ni finyu sana tena sasa kwa kweli utanipotezea muda kukuelewesha , in short ni kwamba Uislamu una nguzo zake bwana sawa, na mtu kama Muislamu ili uukubali ni lazima uzifuate, sawa sisi ni binadamu unaweza kulegalega kwa hiyo basi onyesha hata imani na kujali , na kuna mambo ambayo Muislamu akiyafanya kwangu mimi in my opinion ni sawa na kafiri tuu na moja wapo ni kula Nguruwe kwa kukusudia , hata mlevi wa tikatika anemuogopa mungu na hali muislamu yeyote anemuogopa mungu hagusi nguruwe, ataishia kulewa weee lakini ikifikia nguruwe anakuambia hapo hapana, sasa huyo mla na muuza nguruwe tena kwa kukusudia mimi sidhani kam ana uislamu wowote . unaweza ukaitwa beatrice na ukaswali sala tano, unanipata ama unataka nikufafanulie zaidi? kwani jina ni nini ? mimi nikutajie jina langu haliendani na dini yangu .
    3. Kuna tofauti na yule ajuaye na akaacha kutekeleza na asiye jua ama hajapata chance ya kujua kutokana na mazingira una habari hiyo ? usimlinganishe mzungu asiye na dini na mtu anejua anafanya nini. na mtu ambae ni muislamu kuuza pizza za nguruwe nini tuu mwezi wa ramadhani hata mwezi wa kawaida hiyo ni mungu wako na shimo lako.Ama na wewe umo kundini ndio maana hufungi . jamani kam ndio mnayofanya huko ugaibini rudini nyumbani.

    4. wewe unaelekea ni mbeba maboksi tuu wewe mana hata sikuelewi unaongea nini hebu nieleweshe vizuri hii habari ya rudini nyumabni vita imekwisha ?unaongea nini na hiyo mada yako ya mwisho yaani naona umechoooooka pole.

    mwisho bwana jua y akwamba fainali ni kwa mwenyewe Subhannahu wa Taala siku ya parapanda litakapolia kumbuka hiyo! mimi siko hapa kumjudge mtu lakini watu kama wewe unaediriki kuniita mimi mshamba kwa faida zako na huna pointi ya maana ndio huwa nawamaindisha , kaa ufikirie na kila mtu ana shimo lake lakini tumeambiwa tuu tukumbushane na kukosoana pale unapoona mwenzio kakosea sio unamuacha apotee zaidi huwezi kujua.

    ReplyDelete
  13. halafu wee anony nimesahau kimoja hebu kwanza achan na huo ulimbukeni wa kuabudu wazungu na kuabudu vya wazungu wewe hiyo slave mentality itakuisha lini lakini ? wazungu eeh wazungu eeeh so what ? hivi wewe mshamba una habari ya kuwa kuna watu wameahidiwa pepo hapa hapa duniani ? je unajuaje kam hao wazungu wako hii ndio pepo yao ?

    ReplyDelete
  14. HAYA BWANA MSEMAKWELI NIMEKUELEWA NA NIMESHAANZA KUFUNGA KWA KASI ZOOOOTE NA WAZUNGU SIWAABUDU TENA NA WALA SIWATAKI NA SHULE NITAKWENDA KUJIANDIKISHA KESHO KAMA ULIVYONIAMBIA UPEO WANGU MDOGO NITAUFANYA UWE MKUBWAAAAAAAAAA KUTOKA HAPO ULIPO MPAKA HUKU..... SAUMU NJEMA

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...