Ilikuwa ni makamuzi kwenda mbele wakati wa tamasha la MAKUYA lililofanyika mkoani Mtwara....we acha bwana ngoma za asili ni mazoezi tosha kabisa. Na nyie mlioko majuu siyo kila siku akina Ali K tu waalikeni na hawa!







taswirazzz zote zimeletwa na mdau kwame mchauru aliyeshuhudia tamasha hilo. kwa habari zaidi za tamasha hilo litaloandaliwa kila mwaka kuenzi utamaduni wa kusini nenda

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 7 mpaka sasa

  1. absolutely beautiful - home sweet home! Mtwara has some of the most amazing dances; it's just a joy to watch!

    ReplyDelete
  2. hiyo ngoma inaitwa 'nkalimala", ilikuwa ikipigwa na kibwagizo cha de de de dee dezo !!nakumbuka sana wakati nacheza halaiki na mwalimu Bwamkuu, enzi hizo mechi za RTC na Bandari na Mamlaka ya Korosho. nilikuwa naokota mipira uwanjani, nakumbuka siku moja Rashid Mandanje wa RTC alilamba chenga timu yote !! ilikuwa raha kweli kweli.

    ReplyDelete
  3. KWAME MCHAURU! UNA UHUSIANO NA MAMA MMOJA WA SIKU NYINGI MACHACHARI WA TANU HENZI HIZI LINDI, ALIKUWA MATAWI YA JUU SANA KATIKA CHAMA. HUYU MAMA ANA ASILI YA NEWALA AU MASASI KAMA SIJAKOSEA. ENZI HIZO NILIKUWA KATOTO KADOGO, ALIKUWA ANAFAHAMIANA SANA NA MAMANGU PALE LINDI NA NEWALA.

    ReplyDelete
  4. MIE NIMEOA "BINTI" KUTOKA "MTWARA" HAO NDUGU WANAFAHAMU SANA KUCHEZA "NGOMA"..NANIHII..AIJUAE "MGEMA"

    ReplyDelete
  5. Aksante sana bwana Mchauru,umenikumbusha nilipkuwa mdogo hao wanaotembea kwenye magongo na waliovaa mananilii usoni tulikuwa tunawakimbia!!Jioni ukigoma kuoga unatishiwa kuletewa hilo 'jini'!!Hiv vitu vinaendelea kupotea nchini.Thanks wana Mtwara.

    ReplyDelete
  6. Nawapongeza sana ADEA ambao ni waandaaji wa tamasha hili lililofanyika mwishoni mwa mwezi Agosti hapa Mtwara. Kwa kweli MAKUYA ni tamasha lililovutia sana na kukonyonga nyoyo za wazee vijana,watoto na wageni wa ndani na nje ya Tanzania. Iwapo kweli litaandaliwa kila mwaka ita kuwa ni kivutio kikubwa na litasaidia kutangaza utamaduni wa Wamakonde, Wamakua na Wayao ambayo ni makabila makubwa ya Mkoa wa Mtwara.

    ReplyDelete
  7. Mlitangaze mpaka nje ya nchi, watalii na wanafunzi watafiti wa anthropology watajazana ntwara, ndio njia zenyewe za kukuza uchumi. Igeni mfano mwakakoga, tamasha la majahazi, sauti za busara, na utalii wa kuangalia shughuli za uzalishaji kama mashamba ya spices.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...