Hi Bro.Michu. Habari za majukumu, pia ninawasalimu sana wapenzi na mashabiki wote wa blog hii ya jamii, natumaini wote wazima wa afya njema na mkifurahia ushindi wa Obama.
Msaada tutani kwa jambo hili: Naomba misemo au methali 12 ya kiswahili ihusuyo watoto, anae jua naomba anisaidie tafadhali.
Asanteni sana kama mtaweza kunisaidia kwa hili.
Ninawasalimu sanaaaa...!!!
Kila lakheri kwa yote!
B.F.CHIBIRITI.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 25 mpaka sasa

  1. Sasa Chibiriti umepata Tenda ya kufundisha Methali huko una maanisha unataka kufanya ufisadi kwa kutumia vichwa vya watu, yaani kujipatia pesa kwa wazungu kwa kuutuuliza maswali mmh hujambo hapo~! nakupa njia moja wasiliana na baraza la kiswahili hao wana methali na vitendawili vingi sanaa watakutumia maana hao nia yao ni kusambaza kiswahili.
    Mdau south Korea

    ReplyDelete
  2. 1. Mtoto umleavyo ndivyo akuavyo
    2. Mtoto wa nyoka ni nyoka
    3.

    ReplyDelete
  3. 1.Mtoto umleavyo ndivyo akuavyo

    2. Mchelea mwana kulia hulia yeye

    4 Samaki mkunje angali mbichi

    5 Asofunzwa na mamaye hufunzwa na walimwengu

    6 Asie sikia la mkuu huvunjika guu

    7 Mchuma janga hula na wakwao

    8 Mtoto kwa wazazi hakui

    9 Nyota njema huonekana alfajir

    10 Uchungu wa mwana aujuae mzazi

    11 Mtoto wa nyoka ni nyoka

    12 Mtoto akililia wembe mpe, ukimkata shauri yake.

    BONUS: Mtoto wa mwenzio ni mkubwa mwenzio, usione soo mpe somo...!

    ReplyDelete
  4. Asofunzwaa na mamaye hufunzwa na ulimwengu.
    Mwana umleavyo ndivyo akuavyo.
    Mtoto wa nyoka ni nyoka.

    ReplyDelete
  5. 1. Mtoto umleavyo ndivyo akuavyo. Kama wewe Chibiriti!
    2. Mtoto akililia wembe mpe.
    3. Mtoto asipochafuka atajuaje..!!?
    4. Mtoto Mkaidi hafaidi mpaka siku ya Idd
    5. Mtoto akijamba ujue kashiba
    5.......wengine...

    ReplyDelete
  6. mtoto akililia wembe mpe umkate.
    mwanga mpe mtoto kulea.
    mwana wa ndugu kirungu.

    ReplyDelete
  7. 1. DUNIA NI WATOTO.
    2. ASIYE NA MTOTO NA ABEBE JIWE.
    3. RAHA YA DUNIA NI WATOTO.

    ReplyDelete
  8. mtoto umleavyo, ndivyo akuavyo
    mtoto akililia wembe mpe
    mtoto mkaidi hafaidi mpaka siku ya idd
    mtoto si nguo ukaomba mtu
    mtoto wa nyoka ni nyoka
    usipoziba ufa, toto iko chungulia

    by nana
    czech republic

    ReplyDelete
  9. 1. Ngoma ya kitoto haikeshi...

    2. Mtoto halali na fedha bali na kinyesi

    ReplyDelete
  10. 1)MTOTO HALAZIMISHWI KULA ANALAZIMISHWA KUSOMA

    SIMBA MWENDA POLE KAFUNGWA SPEED GAVANA

    UKITAKA CHA MVUNGU FUNUA MATANDA CHUKUA

    HABA NA HABA TAHAMAKI NAKWISHA

    MWANA MTEMBEZI HULA MIGUU YAKE

    ReplyDelete
  11. Jamani muoneneeni chibiriti huruma. waonsha vinywa hamna dogo? Chbiriti anale watoto. anafanya kazi kwenye day care, kwa hiyo anapaswa kuwafundisha watoto lugha tofauti ili wawe bi-lingual
    hongera kaka chibiriti
    Esther Mswalu ---- Rome.

    ReplyDelete
  12. 1. Wimbo mbaya haimbiwi mtoto
    2. mchawi mpe mtoto amlee.
    3. mtoto alilia wembe mpe umkate
    4. mkono mmoja haulei mwana
    5.mwana mkaidi hafaidi hadi siku ya idi
    6.mwana mkuwanawe ni mwenzio
    7.kulea mwana si lelemama
    8.kulea mimba si kazi kazi kulea mtoto
    9.mwana wa kuku hafunzi kuchakura
    10. mwana wa mtu ni kizushi akizuka zukanae.
    11.mwana maji wa kwale kufa maji mazoea.
    12ucheshi wa mtoto ni anga la nyumba.
    wako mdau
    james
    Holland

    ReplyDelete
  13. 1.Gemu la Yanga na Simba mtoto hatumwi soda dukani kwani atabaki hukohuko
    2. Usicheke kundu la nyani kwani lako hulioni.
    3. Shetani kampanda jini.
    4.

    ReplyDelete
  14. Chibiriti hii methali Maalum inafundisha subira na kusamehe kama mzazi kwa mtoto na wengine wanaokuhusu kwa UKARIBU MNO--- MTOTO AKINYEA MKONO HUUKATI UKAUTUPA---Unajisafisha maisha yanaenda.

    usa

    ReplyDelete
  15. Mtoto si Nguo kwamba utainunua.

    ReplyDelete
  16. It takes the whole village to raise a child

    The first half of our lives is ruined by our parents, and the second half by our children.

    A child educated only at school is an uneducated child

    Children are umpredictable

    It is a wise father that knows his own child.

    Children are like fruits they are sweetest just before they turn bad

    ReplyDelete
  17. 1. Mtoto wa mwenzako ni mkubwa mwenzio. Unaweza kumla tu.

    ReplyDelete
  18. We mdau wa soth Korea hauna jipya. Mpe methali mwenzako. Siyo mpaka aende baraza la kiswahili. tema cheche kama unajua issue. vinginevyo ushauri wako ni potofu.

    ReplyDelete
  19. "MTOTO WA MWENZIO KIZUKA AKIZUKA
    ZUKA NAE"

    ReplyDelete
  20. jamani wadau mmesahau...........

    heri ya paka kukamata panya kuliko mtoto wa kambo vitendo anavyofanaya.

    ReplyDelete
  21. Mwana wa mwenzio mbebe kalala akiamka si wako.

    Teke la kuku halimuumizi mwanawe.

    Dubai.

    ReplyDelete
  22. Ukali wa simba lakini anazaa.

    Unanunua mbeleko na mwana hajazaliwa.

    Dubai.

    ReplyDelete
  23. chelewa chelewa utakuta mtoto si wako.

    ReplyDelete
  24. DUUH KUMBE HOLLAND KUNA WASWAHILI. INGEKUWA MASHINDANO MDAU WA HOLLAND KASHINDA NA FIKIRI ALIWAKUWA NA MBARUKU KTK KIPINDI CHA MINU ZA KISWAHILI AU KWAO NI MSA
    MDAU WAKO
    KISIJU PWANI

    ReplyDelete
  25. Asanteni sana wadau, kwa msaada wenu.Nimefurahi sana.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...