king kikii (shoto) akiwa na wakongwe wenzie katika muziki, shem karenga (kati) wa tabora jazz na dk. remmy ongara aliyekuwa matimila na sasa anaimba injili baada ya kuokoka
Bwana michuzi pole kwa kazi ndugu yangu nashukuru sana kwa yote unayotuletea katika huu mtandao wa jamii.

Ningependa kukufahamisha ile album ya mzee wetu Maestro Kikumbi Mwanza Mpango a.k.a King Kiki iliyochukuwa jina la Raisi wetu Jakaya Mrisho Mikwete imetoka na inapatikana hapa Uingereza katika duka la sterns music lilipo pale Warren st.

Sasa hivi albamu hiyo iko kwenye chart ya juu pale dukani na ni namba mbili kwa mauzo na inategemea kuingia kwenye maduka ya hmv na zavvi next week, na hapa chini nyimbo namba tatu coco imepigwa kwenye radio froots ya Uk,bbc.na pia album imepata review kutoka katika magazeti kama froots uk.sound of city na charlie gillet wa bbc.

watanzania wote mnaoishi nje ya nchi tununue album ya huyu mzee wetu kutoka pale www.sternsmusic.com

ili na wazee wetu wanufaike na jasho lao.Album imetengenezwa katika kiwango cha kimataifa.Na kule Dar es salaam itaziduliwa mwezi wa kumi na mbili iko na nyimbo tisa.
Bofya hapa kwa habari zaidi:


na hapa:

Mdau Yusuf, London

/2008-10-13T14_52_39-07_00

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. KING KIKI YUPO LONDON SIKU IZI?

    DUH HUYO REMMY NDIO KANENEPA HIVO SIKUIZI. SASA MBONA KASIMAMA NA WANADUNIA?

    ReplyDelete
  2. heeee we anonymous 3:59 vipi wewe??yani kama Remmy kaokoka ndio asisimame na watu ambao hawajaokoka?????kwani kuna ubaya gani hapo??wako wanatenda dhambi kwani??we vipi?????

    ReplyDelete
  3. tupe option ya kununua online. si unajua maisha yetu huku ...

    ReplyDelete
  4. michuzi tunaomba sisi tulio huku utusaidie tupate cd za miziki ya remmy .

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...