mtangazaji wa idhaa ya kiswahili ya redio ujerumani a.k.a deutche welle aboubakar liongo akikabidhi mipira kwa kiongozi wa albino united mipira ambayo kituo hicho maarufu cha redio jijini dar wakati wa mazoezi leo kiwanja cha ocean road
vifijo kwa zawadi ya deutche welle
mikono ya shukrani kwa deutche welle
picha ya pamoja baada ya makabidhiano katika uwanja wa ocean road ambako albino united hujifua kila siku. timu hii inajiandaa kupambana na kikosi cha haki ya binadamu hapo desemba 10, 2008 pale neshno katika kusherehekea siku ya haki ya binadamu duniani.
misaada zaidi inahitjika kwa ajili ya timu hii ya albino united ikiwa ni pamoja na viatu vya kuchezea, jezi na pia kofia (za pama), losheni ya kuzuia kuungua jua, maji ya kunywa, madawa ya huduma y kwanza na kadhalika.
kuwasiliana na albino united mpigie mratibu oskar haule namba +255 716 040 550




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 11 mpaka sasa

  1. Ahsanteni DW kwa msaada, wenye kujaaliwa wengine mtaongea misaada mengine inayohitajika.

    Kuhusu kofia za pama, sidhani kama ni muhimu sana, nafikiri hiyo mechi ingechezwa usiku itakua ni vema zaidi ili kuwasaidia ndugu zetu hawa maalbino. Nategemea taa za neshno zinafanya kazi, kama wakicheza na pama, mpira wa kupiga kichwa itakuwaje?

    Haki za binadamu zifundishwe kwa jamii yote, tuache kuwabagua ndugu zetu hawa maalbino, kwani wote sisi ni sawa kwenye mahitaji. Na M/Mungu amewaumba wao kama binadamu mwingine yoyote.

    ReplyDelete
  2. Kaka Abuu, DW haingopi mkubwa...yani umekwivaaa, utafikiri prawns curry!!

    ReplyDelete
  3. OOh this is good news. Amidst all the shameful difficulties which Albinos are going in Tanzania through walu kuna wanaowafikiria. Kudos Deutche welle. Hongera sana Abu. Pamoja na kwamba tunazungumzia suala la timu hii ya mpira naadvise maalbino wa Tanzania mkiona mnatishiwa zaidi you seek assylum in Europe mtakaribishwa na kuishi vizuri zaidi. Nyinyi ndo mna haki ya kutoka nje ya nchi kuomba uhifadhi kwani your lives are in immediate danger-I believe scandinavian and US and Human rights groups can really support you on this. Hata hivyo nafurahishwa na hatua yenu ya kujiunga na kuandaa football team keep it up nikija bongo will drop what I have!!

    mama euro

    ReplyDelete
  4. bwan shemjeji mwambie abuu tarehe 6 Dec hiyoooooo yaja nimtafute wapi halafu ni longgggg holiday waiting to hear from him

    ReplyDelete
  5. Sheikh Abou, Tartibu yakhe naona katumbo kanaangukia kwa mbere utanashati mara tu utaondoka - mwambie huyu bi mkubwa apunguze mahanjumati ama lah itabidi nimuarifu Dk Mwindadi tukupangie mlo lishe Sheikh... (dRU)

    ReplyDelete
  6. Kila jema kwa ndugu zetu kuanzisha timu yao.

    Imefika wakati timu kubwa kama simba ,yanga et kuanza kuchukua hata mmoja au wawili kwenye vikosi vya ili kuendelea kutoa elimu kwa jamii kuwa MTU MWENYE ulemavu wa ngozi ni sana na mtu asiye na ulemavu wa ngozi.

    asante Tutafika tu

    ReplyDelete
  7. Samahani, kuuliza si ujinga kofia za pama ndio zipi hizo? naomba unielezee ili nijue nitawatumia vipi

    ReplyDelete
  8. ndugu zetu maalbino naomba niwashauri,mkiona hatari inazidi na serikali inashindwa kuhakikisha usalama wenu jikusanyeni muende mkapige kambi ubalozi yeyote ya USA au any Europe na mkae mgome kutoka mseme maisha yenu yapo hatarini na serikali haiwalindi na mpo pale kutafuta usalama wenu,nawahakikishia hakuna atakaye wafukuza kutokana na haki za binadamu mabalozi watafanya kitu chochote kile na ikiwezekana watawapa asylum,ila inabidi mkaze buti na lazima kuamini kweli maisha yenu yapo hatarini na ni kweli kila mtu anajua hilo..kwa hiyo nyie ingieni tuu ubalozini na mgome kutoka mseme ni kwa ajiri ya usalama wenu na serikali haiwasaidii

    ReplyDelete
  9. Ndugu zetu maalbino sisi watanzania wenzenu tunawapenda nyinyini sehemu ya jamhuri yetu,sote tuna sikitika na vitendo vinavyofanywa na wajinga wachache ambao wanadanganywa na waganga.sote watanzania tuungane na serikari yetu kulaani na kuchukkua hatua kuhakikisha mauaji ya albino hayatokei tena.
    achaneni na mawazo ya watu wanaoshauri muende nje ya nchikama wakimbizi mfano ni huyu anayejiita mama euro. hawa watu ni wajinga na akiri zao zinaamini kwamba ulaya ndio kuna suruhisho la kila kitu, huu ni upuuuzi kabisa .ni wangapi kutoka kila pembe ya Tanzani watasafiri na kuja kwenye balozi na kisha wapelekwe ulaya wakaishi kama wakimbizi?
    Sisi watanzania Tukiunganisha nguvu zetu na serikari yetu tunaweza kutokomeza mauaji haya bila msaada toka ulaya. na jeshi la police mpaka sasa linahitaji pongezi kwani mpaka sasa taarifa za mauaji zimepungua sana, na hata zikitokea baada ya siku moja au mbili wahusika hukamatwa. hongera jeshi la polisi.
    Mauaji ya albino yalaaniwe na jamii hasa vijijini tuelimishane kupitia vikao makanisa na misikiti kwamba ni viungo vya albino ni viungo sawa na vya binadamu yeyete, ha havina miujiza yoyote ya kutengeneza pesa.

    ReplyDelete
  10. bongo nuksi yaani albino akitembea peke yake kosa!!!

    ReplyDelete
  11. what!!!!???is it necessary adi mbandike ilo tambala lenu uko nyuma DW??ivi hii ni business yan kumpa mtu mnyonge kitu???
    mbona watu wa level yenu mkipeleka misaada ya akili mf chuo,organizations ndo mwabandika ila sio mipira eti mbandike!!
    yan msiwanyanyase mana huu ni unyanyapaa!!!
    mipira mingapi cjui afu bandiko kuuubwa,,nyamafu

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...