israel attacks gaza, palestine, middleast

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 23 mpaka sasa

  1. Huyu Gado ni mbongo au jamaa wa magazeti ya nje?? Yupo fit, ana exposure kubwa ya mambo

    ReplyDelete
  2. we gado usitake kutufanya sisi wote wajinga,siku zote israel imekuwa ikikalia maeneo halali ya palestina na dunia inajua,istoshe kuua raia wa palestina hawakuanza leo tokea enzi za yasir arafat naye walitaka kummua pia kwa makombora na yasemekana walimuua kwa sumu.so hiyo ndio tabia ya mayahud tokea enzi za manabii walikuwa hivyo.na kusema hamas wamerusha makombora na kuua raia wao inashangaza kwani wao wanamiliki vyombo vya habar dunian mbona hatukuona?na je tujiulize nani ni tatizo katika mzozo huu? dunia inajua israel ya kizayuni haitofautiani na ukaburu wa africa ya kusini inakaria ardh ya wapalestina kimabavu,na kusema hamas waliwashambulia ni strategia ya kivita mpe mbwa jina baya ummue kama bush aliposema iraq kuna silaha za maangamizi ili akaue watu,na kuitawala kupitia vibaraka.mwisho israel inaweza tu kuchokoza kiaina hamas wanapojibu tu wayaud wanapata sababu ya kufanya unyama.ndio mana hitler alitaka wasiwepo dunian hawa wanyama.alikuwa anona mbali sana,

    ReplyDelete
  3. HAMAS AND US? or hamas and israel?
    inachanganya kidogo,nilidhani US ni sawa na united states

    ReplyDelete
  4. mdau wa 12:28 sidhani kama umemmpata Gado. Anachoonyesha Gado katika katuni ni sawa na unachosema wewe; kuwa Waisrael nao wanaua raia wasiokuwa na hatia lakini hawasemwi

    ReplyDelete
  5. sikubaliani na huyo jamaa hapo juu ya kwamba wa Israel ni wanyama,hao jamaa wote walishazoea kuuana,na hakuna mwenye haki pale.vita ya wale ni hadi kiyama.mpalestina alikua ni mtoto wa mjakazi(nje ya ndoa)kiyahudi hana haki ya urithi.

    ReplyDelete
  6. We mtoa maoni wa January 09, 2009 12:38pm acha kuongozwa na hisia kama mnyama! Utawezaje kusema kuwa hamas hawarushi makombora Israel, wakati kila kitu kiko wazi kabisa. Au ndo za "kunya anye kuku, akinya bata...". Waambie ndugu zako wa hamas na hizbolah waache kuwa wanachezea petroli, huku wakiwa na mto mkononi! Maoni yako yanastahili kumuelekea zaid rais El Bashir na serikali yake kwa unyama wanaoendeleza huko Darfur!

    ReplyDelete
  7. mdau wa 1:10... nafikiri neno US hapo linamaanisha sisi na sio US kwa maana ya kifupi cha United States. I think that's an Israeli fighter because it has the star of David, which has an hexagram shaped as opposed to the stars on the US flag which are Pentagrams

    ReplyDelete
  8. Mwalim JK Nyerere hakutaka uhusiano na Israel kwa sbabu ya kuvamia ardhi ya Palestina na kuwaua. Uvamizi wao (kama ilivyokuwa wa Iddi Amin alipojiingiza Kagera), kina Verwod na Botha pale SA na Ian Smith hapa Zimbabwe) hatukubali.

    Eti Bongo tumetafsiri kuwa ni vita vya kidini kuwa Hamas ni siasa kali (terrorist) na Israel wao karibu na dini yetu. Ukweli ni kuwa walimtesa Yesu, walimakshifu Bikira Maria na mpaka leo wanimani potofu juu ya ukristo. Halkadhalika, falasafa yao ni upanuzi wa ardhi yote middle east na hasa kwenye vianzo vya maji safi, bahari na mafuta. Hawawezi kuridhika hata iweje na ndio akida yao. Sisi waafrika pia hatuwezi kusalimika na fitina yao. Tanzania imekosa fikra, ushujaa na hekima za Nyerere.

    Sasa tunategemea Hugo Chevez na Castro.

    ReplyDelete
  9. Mjengwa katika raiamwema ameandika makala juu ya hili. kwa ufupi:

    1.DUNIA inashuhudia kile ambacho tunaweza kabisa kukiita ugaidi unaofanywa na dola ‘State Terrorism’.
    2. Taifa la Israel linafanya vitendo vya ugaidi dhidi ya Wapalestina ambao kimsingi ndio wenye ardhi yao.

    3. Kwa zaidi ya miaka 2000 iliyopita kikundi cha Wayahudi kilipambana vikali dhidi ya himaya ya Waroma katika iliyokuwa Palestina ya zamani. Kikundi hiki kiliitwa Salote, wenye hasira kali ikiwa na maana pia kuwa kilikuwa ni kikundi cha kisiasa na kidini chenye imani kali.
    4.Wasalote walipambana kisiasa dhidi ya dola ya wavamizi ya Waroma.
    7.Mwanzoni mwa miaka ya 1900, Mazayuni wa Kiyaudi walianzisha ujenzi wa makazi ya Wayahaudi katika iliyokuwa Palestina ya zamani.


    8.Baada ya Vita Kuu ya pili ya Dunia Moja ya shambulizi la kigaidi la Wayahudi ni dhidi ya Hoteli ya Waingereza iliyojulikana kama King David Hotel katika mji wa Jerusalem. Jengo la hoteli liliangamizwa na watu 89 waliuawa.

    Baada ya Vita Kuu ya pili ya Dunia wahamiaji wengi zaidi wa Kiyahudi waliendelea kuingia katika Palestina iliyokuwa katika udhamini wa Waingereza. Lengo la kisiasa la Wayahudi la kuanzishwa kwa taifa la Uyahudi lilipelekea kuanzishwa kwa vikundi zaidi vya kigaidi vyenye mitazamo ya kitaifa. Viwili kati ya vikundi hivyo ni Irgun na Stern ambavyo vilitumia mbinu za kigaidi katika kuendesha harakati zao. Miongoni mwa mbinu hizo ni matumizi ya mabomu ya barua.

    9. Tangu mwezi Septemba 1947 hadi kutangazwa kwa taifa la Israel , mwezi Mei 1948 vikundi vya Irgun na Stern vilijulikana sana kwa matumizi yake ya mabomu ya barua.

    Kabla na hata baada ya kutangazwa kwa taifa la Israel, vikundi vya Irgun na Stern na baadae taifa la Israel vimekuwa vikiendesha mashambulizi ya kijeshi dhidi ya Wapalestina. Vitendo hivi viangaliwe kama matendo ya kigaidi dhidi ya watu. Katika kufankisha malengo haya, Israel imeendesha mashambulizi mengi ya kigaidi katika vijiji na maeneo ya Waarabu.
    10. Takribani watu laki saba walikimbia makazi yao katika vita vya awali kati ya Waarabu na Waisrael. Watu hawa hawakuruhusiwa kurudi makwao. Hii ndio sababu Wapalestina wengi wanaishi kwenye makambi ya wakimbizi ndani ya ardhi yao na hata katika nchi jirani kama vile Lebanon.

    ReplyDelete
  10. Na hisi US inamaanisha sisi na pia Marekani kwa sababu silaha zoote za sireli ni misaada ya marekani.

    ReplyDelete
  11. We anon wa Jan 09, 2009 3:24 PM, hivi kama unajuwa maandiko watoto 13 (wa kiume 12) walizaliwa na ndoa ngapi sambamba?

    SOMA Genesis 29:16 mpaka Genesis 30:22

    Majina ya wake wa Jacob/Israel ni
    1. Leah
    2. Rachel
    3. Bilhah (Rachel's servant)
    4. Zilpah (Leah's servant)

    ReplyDelete
  12. Munaongea upuuzi mtupu,palestina ni wa mama wa kambo tena aliyekuwa mfanya kazi wa ndani.Wayahudi ndo watoto wa ndoa,wamechokozwa kwa kurushiwa mabomu kila leo,mlitaka wafanyeje? na kama aAmerica inasupport israel,nyie mnao lalamika ndani ya USA simrudi TZ au mwende huko wa hao wapalestina,acheni uhuni.Wapalestina ni wachokozi kwisha.michuzi post msg usiibanie.

    ReplyDelete
  13. LAZIMA ISRAELI IFANYE HIVYO LA SIVYO JEHANAM YAWASUBIRI.

    IMANI za dini ndo msingi mkubwa vita hivi. Wayahudi wanataka ardhi ili JEWISH MISIA aje. WAKRISTO wanashangilia kwa sababu bila nchi ya Israeli YESU HARUDI.

    Na kinachofanyika kwa Wayahudi ni halali kwa imani yao na imani ya kikristo maana wanatakiwa kuuwa watu woote mpaka waishe kwenye ardhi ya ramani iliyotajwa kwenye biblia.

    Ushahidi, hebu angalia aya hizi:

    1.Nchi hiyo ya ahadi imetajwa ramani yake katika Exodus 6:8,
    Exodus 23:31 na Deut 1:6-8. Utaona kuwa wakiisha wapalestina wanaingia walebanoni, wasiria na wairaki

    2. Wamepewa wawauwe watu, wanawake na watoto bila kubakiza soma Deut 2:33-35, pia Deut 20:16-17 wasibakishe uhai hata kidogo.

    3.Wameamuriwa kutowaonea huruma wakati wa mauwaji Deut 7:2, 7:16

    4. Wameamuriwa wasiwauwe kwa mpigo bali kidogokidogo kila mwaka Deut 7:22-23

    5. Wameamuriwa kufanya watumwa watu wasioishi kanaani tuu na wakikataa wawashugulikie Deut 20:10-15

    WAACHENI WENZENU WAFATE DINI YAO ILI WASIENDE MOTONI NA WAPATE KUMFURAHISHA MUNGU.

    ReplyDelete
  14. israel kilicho halali kwao umoja wa mataifa ndio wa kulaumiwa kwa sababu waliwatawanya waisreli ili hilo taifa life lakini huwezi kushindana na mungu hilo ni taifa teule kwake hata kama walimkana yesu, walianza kukusanyika toka kila mahali ili kuikomboa nchi yao, km mnakumbuka wengine walikuwa uganda, palestina hiyo nchi walipewa na umoja wa mataifa, Israeli wanajaribu kurudisha nchi yao hakuna atakayepinga hilo ni suala la kibiblia. yerusalem ni israeli si palestina hiyo toka zamani inajulikana. mkitaka kushindana na Mungu kaeni upande wa wapalestina halafu mtaona, muulizeni misri waisraeli walimfanya nini.

    ReplyDelete
  15. NYIE MNAOSEMA WAISRAEL PALE SIO ARDHI YAO WAPI NDIO ARDHI YAO HAO WAISRAEL?????

    ReplyDelete
  16. KAMA KOMENTI ZA January 10, 2009 3:57 AM NI SAHIHI BASI DINI SIYO CHANZO CHA AMANI. NA KAMA NI KWELI BASI NI HATARI SAANA KITABU HICHO.

    NA NAONA WATU WANASHANGILIA, SAFI SAANA.

    ReplyDelete
  17. Ni ardhi yao na wanatakiwa waichukue kwa kuuwa kikatili bila huruma kila mwaka kama anon wa January 10, 2009 3:57 AM alivyoonyesha.

    ReplyDelete
  18. We anon wa January 10, 2009 2:25 PM, ni kushindana na MUNGU au na mtu mwenye silaha za nguvu? Au unamaanisha silaha hizo zimetoka mbinguni?

    Maana kuna mataifa hayaamini MUNGU na yana silaha kali za kumshinda anayeamini na kashika jiwe, mshale, au vikatuni vya silaha. Ha ha haaaa!!!

    Ushindi wa kivita ni maandalizi mazuri ya kisilaha na zana siyo sala au imani. Sawasawa na kufaulu mtihani ni maandalizi mazuri ya kusoma sio kusali.

    Kama ingekuwa kusali au imani ndiyo njia ya mafanikio basi vatikani ingeongo katika kila kitu kombe la dunia, technolojia, miss universe, reachest billionare, nk. lakini tunaona hata roman empire yao ilivyoanguka.

    USIFIKIRI KWA MOYO BALI KWA UBONGO.

    ReplyDelete
  19. mliotaka maandiko "kwa usahihi" mbarikiwe saaafi sana duh!!
    kwa ufupi israel hiyo ni nchi yao tena ni adi iraq uko na nchi karibia za kiarabu,pateni picha itakuweje apo!!!
    afu israel wanalipa kwa makosa waliofanya kutotii KUTOKOMEZA KABISA IZO VIZAZI WALIVIACHA SO NI MWIBA KWAO,ila adi kieleweke wakitubu kwa Jehovah kila kitu mswano,yan watapata na waarabu wataishi kwa amani,mkasome kitabu km sikosei isaya,jeremia.
    palestina wajanja saaaaana wanajenga ngome za kijeshi ktk raia/makazi ya watu ili israel wakipiga watanagzie dunia eti wanaua raia,afu kwa imani ya hamas/hizbola kufa kiivo ndo thawabu,,,jaman izi imani???
    michu post hii

    ReplyDelete
  20. kuuwa raia, wazee wananwake na watoto kwao si tatizo ndivyo Mungu kawaambia katika biblia. Hata kama vyama hivyo vya kigaidi visingekuwepo. SOMA VIZURI.

    ReplyDelete
  21. Nimesoma mistari ya anan wa January 10, 2009 3:57 AM, nimegundua kwa nini viongozi wakubwa wa dini hawakemei vita hivi. Inaonyesha nao wanataraji matokeo. Sasa hata ile amani na upendo tunaona ni kiini macho.

    ReplyDelete
  22. YAN WEE ANNON Jan 10,3:57 am
    UNA AKILI SAAAANA UBARIKIWE,,JAMEN SOMENI MAANDIKO
    ila hapana jaman kuna wakristo wengi tu palestina,yan sielewi kabisa

    ReplyDelete
  23. Hata kama kuna wakristo palestina ili mradi hawataki kupisha ardhi basi nao wanazuia urudiji wa kristo, kwa hiyo kipigo tuu.

    Hata kama ni wakristo lakini walitokana na ishmael basi kipigo kipo pale pale!!!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...