michael jackson akipokewa uwanja wa ndege wa dar na aliekuwa waziri wa mambo ya nje enzi hizo balozi hassan diria. sio kweli kwamba alifunika uso wake kama ambavyo redio mbao zinadai

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 7 mpaka sasa

  1. ENZI HIZO GAY'S WALIKUWA ADIMU KUPATIKANA.

    ReplyDelete
  2. Nakumbuka watu walilamika kwa nini Mzee Diria, waziri mzima alienda kumpokea uwanja wa ndege.

    Pia Michael Jackson alifupisha hiyo ziara, alisema eti Dar es Salaam kununuka. Na monkey wake anaumwa. Unakumbuka alifika na monkey pale Kilimanjaro Hotel na alifanya uharibu chumbani.

    Wakati huo Mrema alikuwa Waziri wa Mambo ya Ndani. Aliamuru mji wa Dar usafishwe mara moja. Alisema na nakumbuka alisistiza kwa kushika pua yake, "Hata Michael Jackson alikatisha safari yake kwa sababu Dar es Salaam kunanuka! Hata hamwoni aibu!"

    Mji ulisafishwa! Wadau, waliokuwepo mnakumbuka ule uchafu city centre kwenye mafleti. Ilikuwa balaa! Malundo ya taka taka na joto Loh! Harufu unachukuliwa na upepo na kwenda mbali!

    ReplyDelete
  3. The Wako Jackson amekwisha hana lolote kwa sasa hivi. Hata hizo mbwembwe zake zote kwisha. Aende tena kwa madaktari wakamrudishie uafrica wake maana alifanya plastic surgery ya uso ili awe mzungu tajiri. Je sasa mziki na utajiri vyote vimeisha. Kuna sababu ya yeye kuendelea na hiyo sura ya kizungu wakati ni mwafrica toka Nigeria??

    ReplyDelete
  4. Habari za kuaminika zinasema kuwa Wacko Jacko yuko hoi shauri ya madhara ya kubadilisha rangi na kuchonga pua na mambo mengine aliyofanya. Pia hana hela, kafilisika shauri ya zile skandali za kufanya ngono na watoto wa kiume wadogo.

    ReplyDelete
  5. Ebu mwacheni Michael na nyie mnao mhukumu hamna uhakika wowote....inaonekana mnasoma sana "gossip colums" za kwenye tabloids zisizo na habari za kuaminika. Alishtakiwa na yule mtoto lakini mwisho wake ilionekana kabisa kuwa ile familia ya mama na watoto wake walikuwa wanatakata tu pesa za Michael. He found not guilty hivyo msimpakazie.

    Ni kweli Dar na Tz nzima ilikuwa chafu na kulikuwa kunanuka sio siri. Nje ya hoteli ya Kilimanjaro ambayo wakati huo haikuwa hata na 3 star status watu walikuwa wanauza samaki....na hakukuwa hata na hoteli nzuri yoyote.....Yes Michael was a super star and still is, some of us tumekua na miziki ya Michael na daima tutampenda.
    Kwamba ana financial difficulties....so what? Mbona US as a country sasa hivi nao story ni hiyo hiyo? Giant car companies na stock markets zote ziko hoi...

    Live Long Michael, some of us Love you for your talents no matter what!.

    JK - Toronto.

    ReplyDelete
  6. nasikia Michael kasilimu, habari hizi ni za kweli?

    ReplyDelete
  7. Mr. Michuzi kuna kitu kimoja nimenotice, ni kwamba hauandiki kabisa miaka waliyokuja hawa macelebrity. Sina nia ya kuwa a pain in the ass, lakini ningependa sana kujua exactly walikuja mwaka gani, kuanzia, Muhammad Ali, Michael Jackson, Malcolm X, Sidney Poitier etc. Kama hauna information hiyo, hamna tatizo.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...