mshindi wa big brother richard akiwa na kanumba wakisoma skripti kwa ajili ya muvi lao wanalocheza pamoja. baada ya kulamba mkwanja wa nguvu richard hajabweteka. amekuwa bize katika kuendeleza fani aipendayo ya filamu. mtembelee kwenye mtandao wake ucheki alivyo bize. hakika kijana huyu ni mfano wa kuigwa kwa wote wenye mafanikio katika umri mdogo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 19 mpaka sasa

  1. big up biggie braza!

    ReplyDelete
  2. Nasikia mke yake ana mimba. kweli yuko bize!!!!!

    ReplyDelete
  3. watani wajadi bwana eti.. mke yake ana mimba.

    ReplyDelete
  4. If the wife is pregnant that is a good newz,coz i started to think ni ukubwa wa pua tu....,

    ReplyDelete
  5. Kazi nzuri Ricky. Vijana wengine wa Tanzania wanapaswa kuiga mwendo kama huu. Hata sisi watanzania tunaweza kufanya mambo makubwa kinachotakiwa ni kujituma na kufanya vitu vyeti kwa uhakika. Ricky, mawingu ndio yawe kukoma chako. Endelea salama na baraka zetu zote

    ReplyDelete
  6. you go boy
    (binti mgeni hapa)

    ReplyDelete
  7. we Rihard bwana mbona umevaa tshirt ya wanawake!! That is a Tshirt or blause for women man!!!!!

    ReplyDelete
  8. Hali ya uchumi si shwari

    2009-02-06 10:50:17
    Na Boniface Luhanga, Dodoma


    Hali ya uchumi nchini si shwari kutokana na kuyumba kwa uchumi duniani.Kutokana na hali hiyo, uchumi wa Tanzania umeathirika ambapo thamani ya shilingi imeporomoka kwa asilimia 15.

    Hali hiyo ilielezwa jana na Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo, na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Benno Ndulu, wakati wa semina maalum kwa wabunge iliyolenga kujadili matatizo ya kiuchumi yaliyojitokeza duniani na athari zake katika uchumi wa Tanzania.

    Akifungua mkutano huo, Mkulo alisema Tanzania itakabiliwa na awamu ya pili ya athari za msukosuko ambao unatokana na kushuka ama kuzorota kwa uchumi wa dunia.

    Mkulo alifafanua kuwa madhara ambayo yanaweza kujitokeza ni kupungua kwa bei za bidhaa muhimu ambazo Tanzania inauza kwenye nchi zilizoathirika na msukosuko huo, ikiwemo Marekani na Ulaya.

    Vilevile, alisema mauzo kwa masoko mapya kama China, India, Korea na Uturuki yanaweza kuathirika kutokana na kupungua kwa mapato ya nchi hizo yatokanayo na biashara kati yao na nchi za magharibi.

    Pia Mkulo alisema idadi ya matumizi ya watalii wanaokuja Tanzania, inaweza kupungua kutokana na kushuka kwa kipato cha wananchi kwenye nchi zao.

    Kwa mujibu wa Mkulo, athari hizo zinaweza kusababisha uchumi wa Tanzania kuporomoka kutokana na kupungua kwa mapato ya fedha za kigeni na hivyo kushuka kwa thamani ya shilingi iwapo haitaweza kupunguza mahitaji ya bidhaa na huduma zinazoagizwa kutoka nje.

    Kadhalika, Waziri Mkulo aliwaambia wabunge kuwa athari nyingine ni kupungua kwa uwekezaji, hasa uwekezaji wa moja kwa moja kutoka nje kutokana na wawekezaji hao kushindwa kupata mitaji katika masoko ya mitaji ya kimataifa.

    Kwa upande wake, Profesa Ndulu alisema licha ya msukosuko wa masoko ya fedha duniani, sekta ya fedha nchini bado ni madhubuti na salama.

    Akiwasilisha mada katika mkutano huo uliofanyika katika Ukumbi wa Pius Msekwa, mjini hapa, Gavana Ndulu alisema hali hiyo inatokana na benki 31 kati ya 34 zilizoko nchini kuwa na mitaji madhubuti inayokidhi kiwango cha mtaji unaoweza kuhimili madai.

    Profesa Ndulu alisema sababu nyingine zilizofanya sekta ya fedha nchini kuendelea kuwa salama ni ukwasi wa kutosha kukidhi malipo kwa wateja na uwiano wa mikopo kwa amana.

    Alisema soko la fedha la Tanzania pia halijaathirika sana kutokana na kiwango kidogo cha muunganiko na masoko ya fedha duniani.

    Sababu nyingine alisema ni kutokana na usimamizi madhubuti wa benki na kiwango kidogo cha mikopo kutoka nje na umiliki mdogo wa dhamana za asasi zilizoathiriwa na msukosuko huo na malipo kati ya benki kuendelea kuheshimika pamoja na biashara na riba katika soko la fedha.

    Hata hivyo, Profesa Ndulu alithibitisha kuwa soko la fedha za kigeni lilipata mtikisiko.

    Alisema baada ya kuimarika kwa kipindi cha mwaka mmoja kuanzia Novemba, 2007, thamani ya shilingi miezi mitatu iliyopita, imeshuka kwa asilimia 15 nchini, Kenya asilimia 9.7, Uganda asilimia 20 na Afrika Kusini asilimia 50.

    Alisema kushuka huko kwa upande mmoja kunatokana na msukosuko wa soko la fedha ulimwenguni uliowafanya wafanyabiashara kuamini kuwa fedha za kigeni zitaadimika na hivyo kutafuta za ziada kwa lengo la kulimbikiza.

    Akichangia mjadala huo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Mazingira), Dk. Batilda Burian, alisema ipo haja kuweka mkazo katika uzalishaji wa mazao ya chakula, hali itakayoiwezesha nchi kujitegemea kwa chakula na kuuza nje kupata fedha za kigeni.

    Naye mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (Chadema), alisema ipo haja kwa Taifa kuliangalia kwa mapana zaidi suala la msukosuko wa kifedha duniani.

    SOURCE: Nipashe

    ReplyDelete
  9. heeeeeeeee me nilidhani ni demu uyo ric-----rd!!
    hahahahaaaa ze t-shirt sijui kibode suti?afu apo wapi yan iyo house nimeipenda...

    aya yote maisha

    ReplyDelete
  10. Sasa wewe richard kunenepa hivyo ndio nini???acha ushamba bwana keep figure yako ya zamani au ndio kimechanganya...

    ReplyDelete
  11. kina kaka punguzeni Ubobishi jamani picha nyingine unaweza ukasema Huyu jamaa ni demu nini kumbe ni mitindo yenu mingine mingine.

    molisa watson masaki!!!!

    ReplyDelete
  12. washambaaaaaaaaa nyote mnayesema kavaa blouse ya kike .angalieni mavituzzzzz ya calvin clein,larph lauren na madisigner wa kiume wa majuuuuuuu,mtaona mambo ya bigii blaza hicho kishati huvai kama unakitambi lazima huwe umeumbika kama totoz hout ricard.
    mnayesema hiyo t-shirt ni kwasababu mmepitwa na wakati kavaeni kanzu na mashirt yenu ya dubai.zaidi ya haya tembeleeni tovuti za tommy hilfinger,calvin clein,na wengine.
    ndo mtaelewa alichokivaa ricard ni nini.
    biggggiii blaza vaaa vi slim fit t-shrt kinoma you looking sexxxxxy.mwa mwa mwaaaaa.

    biggi blaza fun.south afrika
    SOGA:-) :-)

    ReplyDelete
  13. mavazi hayo kama mtu mbaya usivae yanafaa wenye uzuri kama mademu tuuuu.
    embu mpeni pumzi biggi blaza jamani kaumbika kuna ubaya gani mkimsifu,ingawa kuponda kweni hakumrudishi nyuma lakini mpeni credit jamani he! hamchoki kuponda?,basi ngoja nimsifu mimi kwa niaba yenu

    kaumbika
    handsome
    gazuka ndo usiseme tuliona kwenye bba
    vinguo vyake vya kisera vinampendezaaaaa.

    ReplyDelete
  14. eti kavaa blouse au t-shirt ya kike basi kama kuna jike linavaa t-shirt kama hii litakuwa SAGAJI,hii t-shirt kama polo mnasema nini acheni kuchonga.

    (meno ya juu hoyeeee)
    situmai kitinda mimba.

    ReplyDelete
  15. UCHUMI WA TANZANIA UNAYUMBA/UTAYUMBA! SI HUYU HUYU BENO GOVANA WA BENKI KUU ALISEMA TANZANIA HAITAADHIRIKA NA WORLD CREDIT CRUNCH, NA DR SHAYO WA UK AKAMBISHIA WATU WAKAJA JUU KUMPONDA DR SHAYO NA MASHAKA SASA ANASEMAJE UCHUMI UNAYUMBA/UTAYUMBA? SHAME ON YOU DR BENO/BOT GOVERNOR.

    ReplyDelete
  16. na wewe kanumba ilo panki lako utafikiri baba yake madenge kwenye kitabu cha sani.
    jessica mlope,

    mikocheni b.

    ReplyDelete
  17. You guys are so shallow. How about we focus on their accomplishments instead of their clothes. Imagine if people judged YOU on your clothes only.

    ReplyDelete
  18. Hongera sana Richard, keep on, fani ya filamu ni adimu tz huu ni mwanzo mzuri kwako na kwetu wote. Nakunga mkono naomba tuwasiline, email address yangu tinasenga@yahoo.com muulize Kanumba anaijua hiyo address yangu kwani alipokuwa huku USA tulikuwa tunawsiliana na huwa tunaongea sana kuhusu fani yetu.Tuwasiliane tusaidiane pale tunapoweza kuwasiliana. NI MIMI MAMA

    ReplyDelete
  19. shogazzzzz,,,
    ila tunaomba msiige yan ku-copy na paste mipicha ya noriwood na uzungu
    inaboa sana,,,
    ila keep kazi vijana

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...