JK akimpongeza bosi wa masoko wa Vodacom Tanzania Ephrahim Mafuru kwa mchango mkubwa wa kampuni hiyo kusaidia sana michezo na burudani nchini, ikiwa ni pamoja na kudhamini ligi kuu ya bara. Hii ilikuwa katika hafla ya dina la mchana ambalo JK aliwaandalia Taifa Stars na wafadhili wa timu hiyo ya Taifa inayojiandaa kwa michuano ya CHAN baadaye mwezi huu huko Ivory Coast.
JK akikumbataiana na kocha wa Taifa Stars Marcio Maximo Ikulu leo
JK akipeana mikono na nahodha wa Taifa Stars Nsajigwa
JK katika picha ya pamoja na Taifa stars baada ya dina la mchana Ikulu leo
JK akipozi na wafadhili pamoja na Taifa Stars leo Ikulu

Rais Jakaya Kikwete amewaeleza wachezaji wa timu ya soka ya taifa 'Taifa Stars’ kuwa wanaweza kufanya vizuri na kushinda fainali za Kombe la Mataifa Afrika kwa wachezaji wa ndani zitakazofanyika Ivory Coast kuanzia Februari 22 hadi Machi 8 mwaka huu.
Rais Kikwete alisema hayo, wakati wa chakula cha mchana na wachezaji hao Ikulu, Dar es Salaam leo, ikiwa ni kuwapongeza kwa kufuzu fainali hizo na kuwatakia kheri kwenye michuano hiyo. Alisema kwa vile wamefuzu fainali hizo, basi wasikatishwe tamaa ya kukutana na mataifa makubwa, bali wajione sawa na kimya kikubwa kina mshindo mkuu.
Habari kamili




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 17 mpaka sasa

  1. Asante kaka Michuzi kwa kutuhabarisha. Ila tu kiswahili chako cha "dina la mchana" ndio kinaniacha hoi kabisa. Mimi nadhani "chakula cha mchana" ingefaa pia.

    ReplyDelete
  2. Hongera sana Mhe Rais Kikwete kwa kupata muda wa kushiriki chakula na Timu yetu ta Taifa ya Mpira wa miguu. Ni imani yangu siku moja timu za Taifa za Mpira wa wavu, mpira wa pete, mpira wa mikono, mpira wa kikapu, riadha nk. zitapata pia nafasi ya kushiriki chakula na Mhe Rais kikwete katika suala zima la kuwapa moyo wanamichezo wote wanaoliwakilisha Taifa katika michezo ya kimataifa.

    ReplyDelete
  3. kaka michuzi hata mimi umeniacha taabani na lugha uliyotumia mi nadhani dina ni chakula cha usiku au mnasemaje wadau pamoja na hayo nampa shavu rais wetu kwani amekua mfano.athumani japan

    ReplyDelete
  4. Wadau nauliza tuu wala msije mkanivagaa maana humu watu! usipokaa sawa utashangaa!

    hiviii kama walijua wanaenda lunch , isingekuwa sawa kama nao wangevaa official? I know it does not matter neither bite kuwa walivaa jezi lakini kwani walikuwa wametoka Karume mazoezini?

    Je isingependeza nao wakavaa formal, not necessarily suti . lakini kipicha ( na narudia tena sio kwamba ukivaa suti ndio chakula cha dina ya Ikulu kinashuka utamu) si ingependeza na wao wangevaa formal ili nao wakae mbele?
    maana , ingawa naheshimu kuwa wao ndio wafadhili, maana namwona Imani, mzee Bomani, Kocha Maximo etc .. lakini pia wachezaji wakiwa katika hali ya kivingine pia inapendeza maana jezi tumeshawaona nazo hadi ukifunga macho unaihisi picha na jezi. Namwangaliaga mfano Beckham unaweza muona akiwa katika hafla , anavaa formal na akiwa kimchezo anavaa kimchezo na inakupa ladha kumjua mtu katika hali anuwai!
    natamani kumwona Nsajigwa , Chuji, etc wakiwa na Suti wakila. au hawana? lolololol miyeee.

    NYOTA

    ReplyDelete
  5. kaka Michuzi, dina la mchana ni lunch yaani lanchi tehetehe kwikwi. ila huwa na enjoy sana matumizi yako ya lugha, yanakufanya mtu unacheka na ku refresh mind. Thanks

    ReplyDelete
  6. Duh Bwana Mafuru wa Voda UMEVUNJA KABATI (UMEPENDEZA SANA)!!!

    ReplyDelete
  7. annon apo,,ni kanuni kuvaa jezi zao kila waendapo
    ni jambo zuri kalifanya presidaa yan uku ndo kuwaenzi wanamichezo mara mojamoja si vibaya kuwaliwaza kama ivo na "dinner la mchana km michu" hahahahaaaaa

    ReplyDelete
  8. tuna kuombeeni mungu muoshe nyoyo zetu huku tuliko hatusemi kwa wapopo kila kitu wao tuuuu sie tuna nini riadha hakuna box hakuna lol. tutoeni kimasomaso basi

    ReplyDelete
  9. Prezidaa hakuacha kuingiza uYanga wake kwenye issue za kitaifa namnukuu
    " Sio kusema wale hawatuwezi sisi wakati techinically hamfanyi maandalizi yeyote "

    Hapa kama sikusei alikuwa akimaanisha tambo za Simba kwa Yanga kabla ya mechi yao ya mwisho na kama sikukosea anamaanisha baada ya Yanga kuikimbia Simba pale uwanja mpya wa taifa.

    Maoni yangu ...

    Ni kweli Yanga waliikimbia Simba na Yanga techinically hawakuiweza Simba ila tu kuna tetesi kwamba yeye Prezidaa na washirika wengine walitumia mambo mengine mbalimbali ili yanga iishinde Simba na wala si kwamba Yanga iliishinda Simba mechi ya mwisho techinically ...HAPANA
    Yanga iliishinda Simba kwa njia zisizo za kitechnically bali ni kwa mbinu za nje ya uwanja ikiwamo mmoja wa viongozi tuliompigia kura waTanzania wote kutumia madaraka yake vibaya

    Hii ni salamu yangu kwako kaka

    "Watch your steps, We Tanzanians are watching you very closely" and

    There is an English saying that goes ...

    Things going around will come around your angle ... so get prepared"

    We need a President who will respect whole Tanzanians as citizen but not a president who will make every efforts to make sure Yanga beat Simba

    Shame on you

    Grow !!!!!!

    ReplyDelete
  10. Bwawa la maini mheshimiwa kafanya poa kula dina la mchana na vijana kuwapa moyo ila kwenye kuvaa kama alivyo sema mdau hapo juu sio poa utazani wametoka karume kwenye mazoezi, NMb inabidi wanunue suti kila vazi lina sehemu yake. Nampongeza Kikwete na wadhamini wote.

    ReplyDelete
  11. Anon 11 feb, 8:27. mbona wako sawa tu hapo, labda wangevaa bukta hapo tungeangalia vyengine. Tabia za hawa wanamichezo mara nyingi hupenda kuvaa tshirt zao hata mtaani ukikutana nao sasa sijui ni huku bongo tu au vipi kwangu mimi haisumbui sana.

    ReplyDelete
  12. Wabongo tumezidi kuendekeza nguo na mavazi. Wachezaji wote hapo wamevaa sare zenye sura ya kimichezo. Mlitaka wavae nini zaidi? Isitoshe utamaduni wa masuti tumeiga tu kimagharibi. Wachezaji wangetinga na migolole napo ingekuwa poa tu.
    Isitoshe nguo hazichezi mpira. Tuliocheza chandimu tunakumbuka tulivyokuwa tunawatesa wachezaji wanaokuja na viatu vyao uwanjani. Hivyo hivyo pekupeku watu wanapiga chenga, matobo na mabao!

    ReplyDelete
  13. Anon 11:36

    Perhaps u r the one who needs some growing to do. It is not prudent to come to conclusions on the basis of your myopic evaluation of the president's comments...nowhere in his comments that you decided to use does he mention Simba or Yanga.

    Better yet, your English needs some serious dusting off, so I suggest you do the needful and watch YOUR STEPS!

    Otherwise, you live and you learn!

    Mnyama Mbaya

    ReplyDelete
  14. walitakiwa wavae suti kama viongozi wao pia wewe anon 11 feb, 9:44 kumbuka swala hapo sio kucheza swala ni dina la mchana na wala sio mambo ya kuiga. Sasa unaturudisha nyuma timu inalala jeshi la wokovu viongozi wanalala New africa hotel.maana mwishowe utasema hata kulala 5* hotel ni utamaduni wa magharibi.

    ReplyDelete
  15. Anony wa February 12, 2009 11:17 AM

    Is my English poor ...?
    wow!!! I am happy though my English is poor you have understood it and come to my corner with pointless comments ...
    No wonder you are one of those Yanga fans who cant be creative enough but disturbing our President to use his power to beat Simba...
    By the way you seems to lack innovation and original ideas but just jumping to issues you dont have any clue of ...
    I afraid I cant tell you anything more ... You sound to be an empty tin ... who will publicize everything only for prestige of being recognized that he/she is the one who talked about the story/scandal first ..

    Infront of Public eyes he is our president but behing it he is a President of Yanga and take this fact, he and and his Yanga team mates enterfered the perfomance of Simba and Yanga match soon after he heard that Yanga escaped Simba fearing another prolonged defeat ...it pained them and they decided to put external efforts to make sure that Yanga win the match against Simba by crooks and hooks and it realy happen because he is a president and people fear him due to his title as a president.

    He didnt mention Yanga ...yes but people who can read between the line can smell that ..!!!

    We need a President who will respect all Tanzanians as citizen but not a president who will make every efforts to make sure Yanga beat Simba.

    Poor me I have "emotional president"

    ReplyDelete
  16. Nyie anon hapo juu misupu amewashinda kumrekebisha kiswahili ambayo ni lugha yetu mnaanza kugombana kwenye lugha za watu.Natamani mzee kifimbo cheza angekuwepo amchape misupu kwa kuchafua lugha (dina la mchana) teh teh teh

    ReplyDelete
  17. Anon 11:17 AM, February 12

    Inaelekea walimu wako walipata taabu sana (kama ulipitia shule!).

    Poor you indeed...it's just too bad (and sad) that your shortsightedness makes it almost impossible for you to reason beyond what meets the eyes (and ears).

    With your way of thinking, I'd say you unarmed yet extremely dangerous.

    The costs of freedom of speech, mama mia!

    Mnyama Mbaya

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...