sura za wadau zinajieleza huko abidjan usiku huu...
kidedea kililia hadi filimbi ya mwisho katika wanja la felix houphet boigny
mashabiki kibao walijitokeza kuipa taff taifa stars huko abidjan, wengine wakiwa wamesafiri na timu
bendera yetu ilipendezesha jukwaa la wabongo, ila ndo hivyo tena. gemu...
mpira umeisha na stars imelala 0-1 kwa senegal huko ivory caost katika mtanange wa CHAN. Pichani ni wadau wakifuatilia mechi hio ya taifa stars na senegal katika luninga kubwa iliyowekwa na tbc wakishirikiana na kampuni ya nova media katika viwanja vya bustani ya mnazi mmoja gaden usiku huu. february 25 taifa stars inakutana na wenyeji iliyopigwa 3-0 na zambia katika mechi ya ufunguzi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 31 mpaka sasa

  1. inafaa tufanye bonge la party kwa kuwa tumefungwa kidogo

    ReplyDelete
  2. oyaaaaaaah anfild vipi haujakwisha?

    ReplyDelete
  3. Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya tunaomba ukitumiwa links za live matches utuwekee ukurasa wa mbele na sio kuziacha kwenye comments,ili tuweze kufuatilia na sie tulio mbali kwani huku hawaonyeshi michezo ya Africa.
    vipi wewe lini utatoa adhabu ya viboko wilayani kwako....?
    teh teh
    Mdau

    ReplyDelete
  4. Dah..Roho inauma sana,siku ilikua nzuri baada ya looserpool kuponea chupuchupu kwa waarabu wa manchester,ila stars imetia doa..Tuombe Kheri Insha'allah,Sasa Uncle Marosti ungetuambia walichezaje..matatizo yalikua wapi??kama tuwe na matumaini au laa na vitu kama hivyo,
    Tafadhali.
    Cheupe

    ReplyDelete
  5. Historia imejirudia.

    ReplyDelete
  6. LAKINI CHENGA TUNWALAA HASSA KIPINDI CHA PILI!!!!!
    VIJANA WETU WANJITAHIDI SSANA LAKINI HEIKUWA BAHATI ILA TUTAJARIBU TENA MECHI IJAYO.
    MUNGU IBARIKI TANZANIA.

    ReplyDelete
  7. kwa mtazamo wangu naamini hiki ni kipindi cha mpito kwa timu ya Taifa stars, ukitilia maanani makosa madogo madogo ambayo kimsingi huwezi kumlaumu kocha yameizamisha timu!, wasiwasi wangu ni je kwa muda gani inabidi waendelee kujifunza?.Hatuhitaji kocha wa kigeni kutueleza umuhimu wa kuwa muwakilishi wa nchi yako, Msola, Mziray,Msoma, Msomali,Bendera,Gama, Magram na wengineo walijaribu kwa nafasi zao, naamini ni kipindi cha Maximo kujaribu..

    ReplyDelete
  8. Msiwe na Shaka tutaifunga Ivory Coast na tutamaliza na Chipolopolo! Msiwe na wasi mpira tunao.

    ReplyDelete
  9. kwani tanzania bado tuna tanganyika? hiyo bendera inakuwaje hapo? au ilikuwepo Office za Ivory toka enzi za Tanganyika wakafikiri ndio bado tunatumia iunguzeni moto mie mbara ila huo ubaguzi wa utengeno.

    ReplyDelete
  10. Ila Michuzi kitu kimoja cha kuzangatia
    ktk mpira wa kisayansi na wa kisasa, hivi ni kweli ktk washambuliaji wetu wote waliopo Abijan kuna hata mmoja mwenye sifa za kumiliki ball, kumuegemea beki na 'pace'(kasi)??". Kama kweli wewe unaujua mpira na umeiangalia hiyo game live kwa makini kabisa utanielewa vizuri, ninacho kisema hapa ni kwamba Senagal wachezaji wao wengi ni ma'tall' au siyo bwana na wana stamina ya hali ya juu wameumiliki mpira karibia asilimia 76 kitu ambacho ni wazi Stars walikuwa wana utafuta tu mpira, kwani mpira mbele kwa washambuliji wetu ulikuwa haukai hakuna hata mmoja alioonyesha ana weza ku'hold' mpira kabla ya mid fielders wetu hawajafika ku'suport' strickers wetu.
    Wote walionyesha kuwa hawana nguvu.

    Ili stars angalau waweze kushinda walau hata mechi moja kwa dizaini za wachezaji wetu tulionao kama tunavyo wafahamu( wengi wao wana kosa maumbile makubwa wapo kama under 20 vile!!) inabidi wacheze passing game na ndo maana JK alimptia Maximo hiyo deal afundishe Brazil type.
    Kazi kweli kweli...
    Mpenda Soccer

    ReplyDelete
  11. UKUBWA WA BENDERA SI HOJA, HOJA NI USHINDI, HUO NDIO ULIOTUPELEKA HUKO NA SIYO KUONESHA KUWA TUNAO MAFUNDI CHEREHANI WANAOJUA KUSHONA BENDERA KUUUUUUBWAaaaa... zaiiiidi duniani.TUACHE SIASA KWENYE MPIRA.

    ReplyDelete
  12. Kumbe mlikuwa mnawaonea Wakomoro bure, walikuwa vibonde. Katika sakata haswa, mnawala chenga tu....

    ReplyDelete
  13. Ile ndiyo ilikuwa mechi pekee ya kushinda. Sasa fikiria mechi ijayo tunakutana na mwenyeji ambaye ametoka kupokea kichapo cha 3-0.

    Mpira waliocheza Zambia sidhani kama tutaweza kwenda na ile kasi.

    Kwa mtaji huu, tayari tumetolewa.

    ReplyDelete
  14. Tumefungwa lakini kiwango kinapanda. Poa

    ReplyDelete
  15. Stars acheni mipira ya juu huku nyie wengi mkiwa wafupi.Halafu mjifunze kucheza mipira ya vichwa.Sijaona bado mchezaji wa kucheza Ulaya labda Mrisho Ngassa ambaye commentator alimwita 'danger little boy'+Man of the match!!!Haya mashindano ndiyo yatatupa haswaa picha halisi ya timu yetu ya Taifa.Msife moyo Stars bado.Tafuteni draw na wenyeji Mwisho Zambia watawabeba.

    ReplyDelete
  16. WABONGO MPIRA WETU UKO MIDOMONI NA KWENYE TV..UWANJANI NI HAKUNA KITU!

    BY THE WAY TUSUBIRI KWENDA KUWAPOKEA UWANJA WA NDEGE..WATAPELEKWA BUNGENI? OHH HAKUNA BUNGE KWA SASA..

    ReplyDelete
  17. tumejitahidi kadri ya uwezo wetu na japo tulikuwa vibonde kheri sie wenyeji tu wamebebeshwa mzigo mkubwa tumejitahidi sana na vijana walikuwa wanajituma sana nawapa hongera na uhakika wataendelea vizuri kwani ilikuwa tupewe kibano kikubwa zaidi ya hicho
    mdau toka stellenbosch wine land

    ReplyDelete
  18. Kweli Mheshimiwa Michuzi, Mimi binafsi nimefanikiwa kuiona mechi hii kupitia Internet. Nilifurahi kuiona timu yangu ya taifa katika michuano muhimu Africakwani i jambo ambalo ni nadra sana kwa Tz. Inaonekana bado kweli tuna safari ya kupiga hadi kufikia hatua ya kucheza kwa kiwango cha wenzetu!
    Kwanza mwanzoni kabisa mwa mchezo, nilishangaa kuona Goal Keeper akibishana kidogo na Kocha, inaonekana kuwa haikupangiliwa nani atacheza nafasi hiyo au vipi? kwani alibadilisha jezi akiwa tayari uwanjani katika hali ya ubishi kidogo, mimi sikufahamu jambo hilo!
    Pili wachezaji bado stamina hajiawa ya kuridhisha na vilevile kujiamini ni jambo la muhimu. Huenda, naamini, mechi zinazofuata kutakuwa na mabadiliko kidogo. napenda kuwa optimistic.

    ReplyDelete
  19. Eti ni kweli tulifungwa kwa sababu tumekatazwa kuvuta msuba/ndumu?

    ReplyDelete
  20. Alafu wabongo kwa comments zisizo za msingi, mnaongoza, sijui nijivue uraia? wewe kweli na akili zako timamu kweli unaweza kusema hiyo bendera ni ya tanganyika? hivi wewe umelogezewa au ndio mibangi? Wewe kama kweli umeweza kuiona hiyo bendera na macho yako, huoni kama hiyo bendera ina rangi nne? Huoni kama bendera yenye rangi nne yani Kijani, Njano, Nyeusi na Blue ni Bendera ya taifa la Tanzania, au ndio mibangi inawasumbua? Au kwasababu rangi za njano na nyeusi zimeelekezwa vingine ndio useme bendera ya Tanganyika? wewe ndondo nini? Au nikupe mfano wa Uingereza, umeshawahi jiuliza kwanini wana bendera aina mbili? na mbona watu hawajigawi, sisi hiyo bendera moja mshaanza oooh, sijui mimi mzanzibari nimetengwa, oooh mimi mbara nachambia bendera, chukueni time...hiyo ndio bendera ya taifa la Tanzania, kama hamtaki chukueni pipa mkaichome, kama uwezo huo mnao...pumbaf!

    by Mzalendo 101

    ReplyDelete
  21. strikers wa tanzania ni wafupi sana sijui kwanini mabeki na midfielders wanajaribu kuwapatia mipira ya juu. sasa ngasa na tegete wana mili kupambana na wachezaji kwa mipira ya juu??

    ngassa na tegette wana speeed kali mpira wanayo weza kufanyia kazi ni ile ya kukata mabeki yani through balls. kwasababu hawaja pewa pasi za namna hizo sithani kuna scout wowete pale uwanjani aliona uwezo wa hawa vijana...

    inauma sana striker asipo pewa msaada wa mipira inayoendana na uwezo wake. nathani ngasa na tegete wangependa vigine

    mi nadhani tukitaka kushinda, basi mipira ya juu tusicheze maana possesion tunatoa bure..labda mipira ya juu ichezwe wakati wa hatarini kwenye lango letu la goli.

    MPIRA WA PASI ZA CHINI TU!

    ReplyDelete
  22. MAzalendo wewe ndio Zero wa mwisho kijana pole, huna uzalendo fahamisha watu kwa uzuri. Bendera hiyo haijakaa Kama ile bendera ya Tanganyika Rangi ni tofauti ila hakuna bendera ya tanzania yenye michoro imenyooka kati tu yetu imeenda kiupande Tunakuja kwenye uwengereza sasa Uwengereza wana Scotland Bendera yao Wales yao Na England na N Island Yao kweli then wana ya British kwa ujumla turudi sasa kwetu ndugu zetu Zanzibar wamekubaliwak uwa na Bendera ya Unguja na Pemba, Tanzania Bara tumebaki na ya pamoja sasa Hii hapa ilikubaliwa lini? tujulishane kuuliza si ujinga na nakuomba ukitujibu tujibu kwa heshima na adabu ndio uzalendo. Tufahamishe vizuri tuelewe zaidi ya hapo tutajikuta tunarusha bendera za nchi nyengine kabisa.

    ReplyDelete
  23. michuzi kwani wewe sio mzalendo? hzi koment za watu walio utumwani ulaya,kutaka timu yetu icheze kama za ulaya unaweka za nini,hawajui historia ya mpira na wanashabikia ukoloni. MPIRA HAUKUZWI SIKU MOJA, WALA MWAKA MMJO. ndo machester wapo na kocha miaka 20.wengine wanashabikia maumbo, asernal kuna maumbo agani pale.WATANZANIA MFIKIE WAKATI MUWE NA UZALENDO,HAO WAKOLONO MNAOSHABIKIA, HATA KAMA KIYU CHAO NI KIBAYA WATAKISHABIKIA TU.
    MICHUZI, KOMENT HIZO ZA KUKATISHANA TAMAA TAFADHARI USIZIKE.

    ReplyDelete
  24. kweli timu ya tanzania imebadilika kimchezo kwa kipindi kifupi,yaani jana mamecheza mpira safi sana kiwango cha hali ya juu,kwa mtazamo wangu,subirini watakuja fanya maajabu ktk mechi zilizo baki
    kidumu chama cha mapinduzi,
    taifa star oyeeeeee

    ReplyDelete
  25. Mungu bariki wachezaji na makocha,
    Mungu bariki washangiliaji uko,
    Mungu bariki mpira wetu,
    Mungu ibariki Tanzania.

    ReplyDelete
  26. mzalendo 101???
    khaaa iyo bendera ya wapi jamani?
    mboni mistari iko so strait sio vile mshazari sijui!!!
    au bendera ya muungano siku izi?
    khaaaa

    ReplyDelete
  27. Bendera ya British ni ya sehemu za utawala wake ila kila mtu ana bendera yake ndio wao sheria zao wanajuwa wao wenyewe huko na wabeba sababu hata Canada wapo kwenye hiyo bendera Moja Royal Union wamebadilisha jina kuita Great Britain kwa zile nchi nne. Canada bado wapo chini ya Queen wa Uwengereza Nafikiria sina huwakika. Huku Tanzania 1.Tanzania Bara na Visiwani tunatakiwa Tuwe na Raisi Mmoja tu.

    2.Zanzibar Miaka 5 Raisi Kwao Miaka 5 Bara Wao Visiwani wawe na Bendera yao kama waliyonayo sasa hivi na sie Tuwe na Yetu.

    Sababu kama Zanzibar wana raisi na serikali basi ni nchi lenye Taifa ya kujitegemea tunatakiwa tuwe Pamoja Tanzania Bara hawana Bendera ya Bara kwahiyo hiyo Bendera mnayoona hapo ya Nchi gani tuna aibisha mpaka kwenye bendera sasa.

    ReplyDelete
  28. Bongo tunakuja, salaam zao,
    Wiki moja kabla ya mashindano kuanza ungeulizwa nani ataka bingwa , Mara moja Ivory Coast na Ghana wangekuwa kwenye top two.
    kiko wapi, wote wamepigwa tena mwenyeji ndio kapigwa kama mtalii.
    Kimsingi Ifikie wakati Watanzania tujivunie Timu Yetu Ya Taifa, kuwa na timu bora yenye kushinda kila Gemu sio kitu rahisi, Hawa Zambia waliomkamua Ivory Coast mbona walikuwa mdebwedo kwenye Cahllange Cup!!!
    Mwalimu Maximo anajitahidi kadri ya uwezo wake na hata wachezaji wanjituma sana, Hili ndio kandanda, hata Maximo akiondoka bado watanzania Tutatakiwa kujenga timu itakayotoa ushindani Afrika na Dunia nzima, ni maisha, namaanisha ni jambo endelevu, ni vema tukumbushane kuwa kupata mafanikio ni kazi , kuyaloinda mafanikio ni kazi zaidi, hivyo tuzibeze tu, ila tujipange kudumisha mafanikio ya soka tuliyofikia, Kufungwa bao moja na wale senegal mechi ya CHAN kwetu TZ ni achievement showing tht now,we can compete even with those who have FOOTBALL ACADEMIC SCHOOLS for TWO DECADES NOW>
    Mungu ibariki Tanzania
    Aluta continua
    Mdau
    Nelspruit,South Afrika

    ReplyDelete
  29. usemi wa babu rukhsa bado unafanya kazi tz ni kichwa cha mwenda tehe tehe tehe

    ReplyDelete
  30. Wewe Anyonyi February 23,3:26pm..wewe ndondo sana, hivi wewe bado una-stress na bendera tu..tengeneza ya kwako basi tuiite ya Taifa, maana umekalia kujua sana utadhani wewe ndio baba wa taifa, hata bila hiyo bendera soka tunaliweza vile vile, Bendera ya kishabiki sio lazima iwe authentic wewe jehu...lazima uwe mbunifu wa kiushabiki kama kweli wewe ni mshabiki sio unakalia pumba tu humu ndani na comment zako za kikoloni...mimi nawafagilia sana wadau walioingia mifukoni mwao na kutoa nauli ya kwenda kuipa support timu yetu ya taifa kwasababu wao ni wana uzalendo na ndio maana wakaamua kuwa wabunifu na kutengeneza bendera yenye rangi nne za taifa la TANZANIA..Utake usitake hiyo ndio bendera ya TAIFA LA TANZANIA, kama vipi kashtaki..acha porojo hapa!

    Mzalendo wan on wan.

    ReplyDelete
  31. iyo picha ya 3 toka juu,,,
    uyo ni BATILDA BURIANI AU??ilo lemba aswa...
    bendera ya wapi iyo weee michu?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...