JK akiongea na muasisi wa Chama Cha TANU Mzee Omar Selemani Mwenye umri wa miaka 104 alipokwenda kumjulia hali nyumbani kwake mjini Dodoma leo asubuhi. JK, ambaye pia ni mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM alikuwa mjini Dodoma kuendesha vikao vya Kamati kuu na Halmshauri kuu ya CCM.Rais amerejea jijini Dar leo mchana.
JK akiwa amembeba mtoto Ramadhani Juma(5) ambaye ni kitukuu cha Muasisi wa Chama Cha TANU,MzeeOmar Selemani wakati Rais alipokwenda kumjulia hali muasisi huyo nyumbani kwake mjini Dodoma leo asubuhi.Rais Kikwete tayari amrejea jijinji Dar. Picha na mdau Freddy Maro wa Ikulu.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 17 mpaka sasa

  1. Tunakushukuru muungwana kuwakumbuka wazee wetu. hawa ndio wenye baraka na busara. unafanya utaratibu mzuri sana kila ukipita dodoma unawapa salam.
    muungwana soma kitabu cha uamuzi wa busara kimetungwa na mohamed Said ili uwakumbuke wazee hawa ambao wametoa mchango mkubwa.

    ReplyDelete
  2. MTOTO ANAMSALIMIA RAISI WA TANZANIA KAVALISHWA BENDERA YA UK.....WEWEEEEEE TANZANIA TAMBARARE ANYTHING GOES

    ReplyDelete
  3. Pelekeni picha yake "Guinness World Records". Hawa jamaa wakifika 100 tu wanatutambia sana, lakini sisi wazee wetu wanaishi kwa mitulinga hadi 110+ wala hatuwapambi!

    ReplyDelete
  4. Natumai JK umepata maoni na mawaidha mema kutoka kwa mzee. Naona bado yuko ngangari haswaa. Nategemea 20015 atakuwa hai na kupiga kura.

    ReplyDelete
  5. kaka michuzi nilishituka kuona ile namba tano kwenye mabano, mwanzo nilifikiria ni miaka mitano ila nilipoiangalia picha vizuri nikaona kuwa yule dogo hawezi kufikia huo umri...... tuweke sawa kaka tukusome vizuri

    ReplyDelete
  6. Mi nlifikiri muasisi ni marehemu mwalimu JKN. Hapa inabidi mtupe ushahidi wa kutosha.

    ReplyDelete
  7. NICE BLAZER JK. LOOKS LIKE IT'S A RALPH LAUREN. JK GOT WAYS WITH KIDS, CONGRAT'S.

    ReplyDelete
  8. MUUNGWANA HUJULIKANA KWA VITENDO VYAKE SAFI J.K KWA KUWAKUMBUKA WAZEE WETU UTAONGEA NAYE LAKINI HUSIA HAWACHI KUKWAMBIA NDIO HAO WENYE BARAKA NA MAWAIDHA MEMA

    ReplyDelete
  9. JK NA MAMA SALMA nina wasiwasi mpo njiani kuongeza mtoto mkiwa hapo hapo Ikulu, (joke)maana mapenzi yenu kwa watoto hayana mfano. MUNGU AWABARIKI SANA KWA UPENDO WENU

    ReplyDelete
  10. Duh! Ni aina ya uzao au inakuwaje... babu ana miaka mingi lakini ngangari! Mtoto anaonekana mdogo sana lakini ana miaka mitano (5)! Wanabaiolojia mpo?

    Mungu muongezee huyu mzee miaka mingi zaidi, Mungu mbariki Jk, Mungu ibariki Tanzania.

    ReplyDelete
  11. khaaaa 104???kweli ipelekeni guiness book jamani!!

    uyo mtoto ana miezi 5 au miaka 5??

    ila JK kwa pamba?hajambo!hahaaaa zinga la b******oo

    ReplyDelete
  12. Sawa!Lakini hebu tujiulize,hapa nchini idadi ya wazee wenye umri uliozidi miaka 65 au hata 70 hawazidi milioni 3 nchi nzima!Je,serikali inawajali wazee hawa kwa kiasi gani?Je,ina takwimu na kumbukumbu zao za wapi walipo na wana hali gani ya maisha?Kila mmojawapo wa hao wazee kwa njia moja au nyingine alishiriki kikamilifu katika ukombozi na ujenzi wa nchi hii!Na sio wale tu waliojitokeza waziwazi katika uongozi wa kisiasa!Walikuwepo waalimu,wauguzi,madereva,wakulima,
    wafanyabiashara,wavuvi na wafugaji na wengine wengi.Wao ndio walioifikisha nchi yetu hapa ilipo!Hivi sasa wamezeeka na hawana nguvu tena ya kujihudumia wao wenyewe binafsi na familia zao.Je,Serikali imebuni mpango gani unao fanana na "social security funding"kwa ajili ya wazee wote hawa bila kubagua walikuwemo katika siasa au la hasha.Je,huu ugeni wa Kikwete kwa huyu mzee wetu muasisi wa tanu tuuchukilie vipi?Was it a Public Relations Exercise intended to attract attention of the Party Faithfulls?Or was it driven out of guilty conscience for the aged and old?Or was it purely a coincidence?Or was it a monitoring and feedback process for the good of the Party Supremacy?More Questions than Answers!

    ReplyDelete
  13. mtoto huyo ana miezi mitano. hebu tupunguze kukalili tu kwamba ikiwekwa (5) basi ni miaka mitano. Angalia mtu/kitu katika mukhtadha wake. Kwa muonekano wa mtoto huyo hawezi kuwa na miaka mitano ima basi atakuwa na ulemavu wa kudumaa jambo ambalo siamini kuwa ndilo.

    Wazee ni dawa.

    ReplyDelete
  14. Jamani mimi nafikiri huyu mtoto ana miezi mitano sio miaka mitano. Nakumbuka wakati nina miaka mitano nilikuwa nachunga ng'ombe, mbuzi na kondoo. Ila tu siku nikamkumbatia ng'ombe miguu ya nyuma, nilipigwa teke languvu.

    Na wewe anon wa hapo juu ni mwaka 2015 na sio 20015. (mwaka wa uchaguzi) nanimeona wengi mnawafagilia watu wawili wanaojua kuandika essay (mashaka na shayo.



    P.E.D

    ReplyDelete
  15. Mdau unayefikiri Mwalimu nyerere alikuwa mwanzilishi wa TANU unaonyesha jinsi gani wewe na wenzako kama wewe hamjua historia ya nchi hii!

    ReplyDelete
  16. Mh, annon wa March 09, 2009 11:15 ana maswali jamani,sijui nani wa kumjibu masikini. Anaonekana na mahasira na maisha..manake hizo ! ! baada ya kila sentensi. Pls don't dwell on pessimism, try optimism because it is a better way to look deal with many situations.

    JK, big up man of the people!

    ReplyDelete
  17. Refreshing JK and salute to you Mr. President for bringing attention to our history. Thank you for taking time to visit Mzee Selemani. Je wagapi leaders wana jaribu ku preserve history yetu.? Without you most of us would not be aware of Mzee Selemani.
    History matters. Jamani and still standing tall! Songa Mbele!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...