Ndugu Michuzi,
kupitia mtandao huu wa jamii,ninapenda kuwatangazia watanzania wote katika jiji la Dallas na maeneo yote ya Marekani kwamba, Kanisa la Umoja litakuwa na ugeni mkubwa kutoka nyumbani Tanzania kuanzia tarehe 1.5.09.

 Kwaya ya Azania Front Cathedral kutoka D.S.M itakuja kumsifu Mungu katika jiji la Dallas.Tunaomba kila moja atakae soma tangazo hili amjulishe mwingine.Kanisa la Umoja ni kanisa ambalo limeanzishwa na linaendeshwa na watanzania pamoja na watu mbali mbali wanaozungumza lugha ya kiswahili.

Mpaka sasa kanisa hili limeshaleta waimbaji mbali mbali katika jiji hili la Dallas  kama Cosmas Chidumule, Rose Muhando, Mkasa junior,Mfalme Daudi na watumishi wengine wengi kutoka nyumbani.

Mwisho tunapenda kuwakaribisha watu wote katika ibada zetu  siku za  jumapili kuanzia saa kumi na mbili kamili jioni mpaka saa mbili kamili. Kumbuka kuna mafundisho maalumu ya watoto.
   Anuani:
12727 Hillcrest,
 Dallas 
Teaxs 75230

   Simu:
214 554 7381,
682 552 6402,
817 875 4764,
469 2791762.
   Karibuni sana.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Mnaonaje safari ijayo muwaalike wasabato masalia,maana ni karibu mwaka sasa wanasubiri zali kama hilo.

    ReplyDelete
  2. Kwa aliyetuma hiyo habari nafikiri haiko sahihi, mimi nikiwa ni miongoni mwahao wanakwaya sisi tumepata mwaliko toka kanisa la kilutheria la Oklahoma City kupitia mwanakwaya mwenzetu aliyerudi toka huko Oklahoma. Naomba kurekebisha hilo.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...