KILICHOTOKEA IVORY COAST KATI YETU (HARUNA, ATHUMAN, KEVIN, BONI, AMIR, NURDIN) NA KOCHA MARCIO MAXIMO
UTANGULIZI

Kwanza kabisa tunatoa pongezi kwa mtandao huu wa jamii na Tunaomba balozi utufikishie haya tulionayo kwa jamii ya watanzania wote.

Katika maelezo yetu haya tutaeleza kila mmoja ya walioandikwa hapo juu kilichomtokea kwa kituo kabla hatujaondoka na baada ya kuwa kwenye mashindano, tunafanya hivi kwa kuwa hatuna uwezo wa kuongea na waandishi wa habari ana na pia tunaogopa kama binadamu tusije tukatereza kitu ambacho kinaweza kikatuletea madhara katika shughuli zetu za kila siku (Kucheza Mpira).
Hivyo kwa ushauri wa ndugu na jamaa zetu tukaona ni bora tutumie tovuti yetu hii ya jamii kuwaomba msamaha watanzania wote na pia kuwapa haki ya kujua nini hasa kilichotokea na pia tunaomba wanahabari watumie ujumbe wetu huu kuwafikishia habari wananchi wote wa Tanzania ili waweze kuelewa undani wa sakata zima hili na tunaomba endapo tutakacho kieleza hapa kitakuwa sio kweli atoke mbele ya jamii na kutukosoa tuko tayari kwa hilo.
ATHUMAN IDD (Chuji)
Itakumbukwa kuwa wakati nikiwa na timu yangu ya Yanga niliumia nyama za paja kitu ambacho kilisababisha Dakitari wa timu kushauri kuwa nipumzike wakati nikiendelea na matibabu ili niweze kupona vizuri kitu ambacho nilikifanya na nikaamua kwenda kwa mama yangu Tanga kupumzika wakati nikiendelea na matibabu.
Siku chache baadae niliitwa kwenye kikosi cha timu ya taifa ambapo niliripoti lakini sikuweza kufanya mazoezi na timu kwa sababu ya tatizo langu la paja na hata Dakitari wa timu alithibitisha hilo, lakini baada ya muda mfupi nikaanza mazoezi mepesi pamoja na timu na mwisho nikawa sawasawa japo sio 100%.
Muda mfupi kabla ya kwenda kwenye mashindano Kocha mkuu akaniita na kuniambia kuwa ananichukua mimi kwenda Ivory Coast kwa kuogopa kelele za watu lakini sitocheza kitu ambacho sikukielewa lakini pia sikutaka kukubali kwani niliamini naendelea vizuri na baada ya siku chache nitakuwa sawasawa 100% kwahiyo kocha ataweza kunipanga.
Tulipofika kwenye mashindano niliongeza bidii ya mazoezi ili kumshawishi kocha kuwa niko sawasawa 100% lakini hilo halikueleweka nikaendelea kubaki benchi bila maelezo ya kujitosheleza kwanini niko benchi hasa mechi ya pili tuliocheza na Ivory coast nilikuwa niko tayari kimwili na hata kiakili kwa aslimia 100 kucheza mchezo ule lakini sikupangwa.
HARUNA MOSHI (Boban)
Kucheza kwenye mashindano makubwa kama yale imekuwa ni ndoto ya kila mchezaji duniani kwahiyo kupata nafasi kama ile huwa ni bahati na kila mtu huwa anajitahidi kuonyesha kiwango chake chote ili ikiwezekana apate nafasi ya kwenda kucheza mpira wa kulipwa popote duniani kwani kunakuwa na wawakilishi wa vilabu mbalimbali vya nje kuja kuangalia wachezaji wanaoweza kuwafaa.
Siku ya mechi ambayo tulicheza na Ivory Coast nilipangwa lakini nakiri nilicheza chini ya kiwango ila tu naomba watu waelewe kuwa haikuwa hivyo kwa makusudi kwani ilikuwa ni nafasi yangu ya kuonekana hivyo ilitokea kwa bahati mbaya sana na ninasikitika kwa hilo.

Baada ya mechi tukiwa kwenye mkutano wa wacheza kocha alinisema sana kupita kiasi (kwa karibu dk15 hivi) kitu ambacho hakikunifurahisha na kama hivyo haitoshi kwa muda wote toka siku hiyo nikawa hata nikimsalimia haitikii wala hataki kuniangalia machoni kwa kweli ni kitu ambacho kiliniumiza sana katika muda wote niliokuwa mashindanoni.
KEVIN YONDANI
Na mimi pia nakiri kuwa katika mechi ya kwanza nilicheza chini ya kiwango lakini kama alivyosema Boban kuwa ile ilikuwa ni jukwaa la sisi kuonekana duniani kwamba tunaweza endapo tukipewa nafasi.
Kwa hiyo kutokana na presha ambayo kwa kweli ilinizidi nikajikuta kuwa nimepania sana mpaka nashindwa kucheza kwa kiwango kile ambacho ninakifiria kichwani kwangu.

Baada ya mechi kwenye mkutano wa wachezaji kwa kweli hilo lilikuwa ni kosa kubwa sana kwa kocha wetu kiasi cha kushindwa hata kuvumilia na kunipa nafasi nyingi na hata kuongea au kusalimiana na mimi ilikuwa haiwezekani kitu ambacho nadhani haikuwa sawa nilistahili kupewa nafasi nyingine niweze kufanya kile ambacho kila mtu alikitarajia kutoka kwangu.
AMIR MAFTAH
Kwa upande wangu mimi kosa langu kubwa ni kuwa karibu na Athuman kwa hiyo na mimi nikajikuta nimeingizwa kwenye mkumbo huo, lakini ikumbukwe kuwa mimi na Athuman tumekuwa tukila na kulala pamoja toka wakati wa Serengeti Boys. Kwa hiyo n iwatu ambao yeye anapokuwa na matatizo kama haya mimi najisia angalau kumwambia neno hata moja ambalo litamfariji kwasababu ndie mtu ninemjua vizuri kuliko mtu mwingine kambini na siwezi kumtelekeza leo hasa wakati ambapo anahitaji kuwa na mtu wa karibu.
Kwangu mimi hilo lilikuwa ni kosa kubwa sana kiasi cha kutopangwa na hata kuwekwa kwenye list ya wachezaji wa akiba.
NURDIN BAKAR
Kama ilivyokuwa kwa Amir na mimi kosa langu kubwa ni hilohilo la kuwa karibu na Athuman na mimi pia nikaingizwa kwenye mkumbo huo, lakini Mimi, Amir na Athuman tulikuwa kulala pamoja Serengeti Boys, Simba na hata sasa Yanga kwahiyo niwatu ambao mmoja wetu anapokuwa na matatizo tunakaa kama kitu kimoja kuongea na pia ifahamike kuwa hata wazazi wetu wanafahamiana kwahiyo tunapoongea ni kama watoto wa familia moja, lakini baada ya kuona kuwa kocha hafurahii uhusiano huo nikaona wacha nijitoe kwa muda na ndio angalau nikapata nafasi ya kucheza.
MWINGINE
Haya yaliyotokea pia yamumuhusisha Godfrey Boni ambaye sijui ni kwanini Kocha aliamua kumuingiza kwenye sakata hili labda anaweza kueleza vizuri (Kocha) endapo akiulizwa.

MATUKIO YA IVORY COAST
Sisi wachezaji ambao tulikuwa katikati ya sakata hili yalitukuta yafuatayo:
Tulitolewa kabisa kwenye Program ya mazoezi ya timu tukawa tunafanya mazoezi wenyewe pembeni (kwa wale waliokuwepo wanaweza kuwa mashahidi wa hili).

Tulitolewa kwenye mazungumzo ya timu kwa sababu kocha alisema anataka kuzungumza na wachezaji wake tu, ikabidi sie tutoke waongee.

Kocha alimwambia Katibu kuwa sisi asiotutaka turudshwe nyumbani ndege ya kwanza itakayopatikana kitu ambacho katibu hakukubali na hata Waziri alipoambiwa kasema yeye ndio kiongozi wa msafara kwahiyo ndie anaeamua ni nani anarudi na nani anabaki kwahiyo hakuna mtu atakae rudi nyumbani kabla ya mashindano kuisha.
UWANJA WA NDEGE DAR ES SALAAM
Baada ya kufika uwanja wa ndege waziri Mkuchika alituita (Boban na Chuji) na kutuuliza kilichotokea tukamueleza yote bila kubakiza.
Baada ya hapo tukaamua kuondoka kurudi makwetu kitu ambacho watu wengi waliona kuwa sio sawa kwa hiyo kwa ajili yao tunawaomba radhi kwa hilo lakini ikumbukwe kuwa sisi ni binadamu na yote yaliyotokea Ivory Coast yalitutesa kwa kipindi chote tulichokuwa huko tukaona hatuna hata haja ya kuwa na watu ambao hawakutaka kuwa na sisi, kifupi ni kwamba hatukutaka kuwa wanafiki na kuvaa tabasamu la plastiki.
MWISHO
Tunatoa shukurani zetu za dhati kwa Katibu wa TFF Frederick Makalebela na Mkuu wa msafara Mh. Muhammad Seif Khatibu wa kutumia busara ya hali ya juu wakati wote wa mtafaruku huu na tunawaambia kuwa huo ndio moyo wa kimichezo na kizalendo.
Tunaimani endapo wakiendelea hivi basi Nchi yetu itafika mbali kwa Tanzania ni Kubwa kuliko mtu binafsi awae yeyote Yule.

Hayo ndio yaliyotokea Ivory Coast na tunaomba mzee wa tovuti ya jamii uwasilishe kilio chetu kwa watanzania na tumeamua tutoe leo kabla ya wenzetu kuondoka kwenda mashindanoni Misri na kama kuna mtu yeyote anasema kuwa haya tuliyoandika sio kweli basi awasilishe maoni yake ili watanzania wajue mbivu na mbichi.

Unaweza kuwasiliana na sisi kuhusu hili kwa email (KAPUNI) Ila tunaomba usiichapishe hii email address kwenye mtandao wa jamii.
Asanteni sana
Haruna;
Athuman;
Kevin;
Amir;
Nurdin;
Godfrey.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 52 mpaka sasa

  1. kama haya waliyoyaongea wachezaji yatathibitishwa, basi ni 100% kocha hafai, inatakiwa aondoke sasa na si mwezi huo wa saba!mimi mwenyewe nacheza mpira kocha aliyefundishwa unapokosea huwa anatafuta nafasi ya wewe na yeye kukaa na kujaribu kukurekebisha, sijawai kwanza sikia kocha anamchukua mchezaji na kusema unakwenda tu sababu naogopa maneno ya watu, huyo abaki huko huko kwao brazil na pesa na nguo zake mtumieni huko huko inatosha. cham cha soka, ni wakati umefika sasa wa kutafuta kocha aliyesomea hata kama hana uzoefu, kuna mtanzania kasoma ujerumani kwanini tusimtumie huyo anaitwa sijui mpinduzi ana, mbona kwingineko watu wanapewa nafasi kwanini sisi mpaka sijui mbrazil sijui nini, aende kwao huko akacheze samba,na anajidai sijui anatakiwa na nchi kibao labda vijitimu vya watoto china ama arabuni

    ReplyDelete
  2. Haruna Moshi kisingizio Chako hakina msingi wangapi wanasemwa Gemu wakiharibu ukisemwa sio kama upendwi ndio unapendwa na anakupa nguvu za kumuonesha sio Kumzarau au wadau mnaonaje? usimchunie Manager wako wala kumzarau hao wengine nimewaelewa kidogo.

    Kuna hao Group la watu 3 inaonesha SAMAKI MMOJA AKIOZA WOTE WANAOZA.

    TAIFA STARS; WACHENI UTOTO WACHEZAJI MKUE SASA. bado mna zile tabia za visingizio na kutaka kunyenyekewa. FROM PAZI anayeona nimekosea aseme sio kila binadamu anapatia. Kijana PAZI, Bagamoyo.

    ReplyDelete
  3. TUMECHOOOOOOOOOKA na Topic za Maximo yeye mwenyewe hataki ku SIGN tutafute mwengine sasa hivi.

    TAIFA STARS wachezaji lazima wajifunze Tabia MAximo kafundisha mengi tumshukuru.

    Lazima wachezaji Manager yoyote atayekuja wamuwekee Heshima.

    Nizamu Finyuuuuuuuu. James.

    ReplyDelete
  4. Hawa wotee ni waongo, kama wanaongea ukweli waite press conference waandishi wawaulize maswali ambayo watu wote tunataka majibu yake, hapa wanajikosha tu! Kama mtu unaongea ukweli utateleza nini wakati unachoongea ndicho kilichotokea? kama unachoongea sicho ndio unaogopa kuteleze. Ni kama mzee upara alipogoma maswali ya waandishi, mwenzake waziri kijana alirushusu aulizwe maswali hadi waandishai walinyamaza wenyewe. Nawasikitikia hawa vijana, wanaaharibu future yao kwa ujinga!

    ReplyDelete
  5. wadogo zangu: Haruna, Athuman, Kevin, Amir, Nurdin na Godfrey..poleni sana kwa sakata hili lililowakumba. Katika daraja mlofikia, mpira ni taaluma ; ndo kusema una weledi (professionalism) ikiwa ni pamoja na hali, miongozo na namna ya utendaji ili kufikia malengo tajwa (kama vile taratibu zilizokubaliwa/zoeleka, kuwa na kuheshimu/kufuata miongozo ya viongozi na njia za upashanaji taarifa)..kwa haraka haraka (ni vigumu yeyote kuamulia jambo hili kwa taarifa yenu bloguni) yaonyesha kuwa mmetiwa unyonge na mwenendo na maamuzi ya bosi wenu. Pia mwataka kuonyesha ukomavu kwa kuwaomba watanzania radhi (hongera sana !) kwa matendo yenu mara mlipowasili. Ama baada, ningependa kuwaambia kuwa nahisi hamkushauriwa vilivyo (ama sijui mmepotoshwa !) kwa hatua hii ya kuandika na kuyaanika haya kama hivi. Kwanini ?..Sababu migogoro ni sehemu ya shughuli yoyote ya kazi hasa za kiweledi (professional endeavour). Na utatuzi wa migogoro yabidi ufuate taratibu zilizokubaliwa. Nyote ni kundi la wachezaji stadi, hodari na wakusifika. Ndo kusema kwamba hamna atayewahukumu ila ikiwa mnastahiki hilo. Kama Waziri Khatib na K. Mkuu wa TFF waliweza kuleta busara zao kule CDI, mzitumie hizo na zingine-we za hapa nyumbani ili msikilizwe na hukumu ipatikane kwenye ‘tifu’ na ‘bifu’ lenu na Bosi wenu. Bosi wenu kama bosi wengine woooote ni binadamu, nyote pia hali kadhalika. Kujiosha bloguni ama popote pasipo kuwa jukwaa rasmi la utatuzi wa mgogoro kama wenu ni njia ya mkato ambayo aghalabu haitatoa suluhu ya kudumu.. aliyosema yeye na mnayosema ninyi, ingawa hayakaribiani yanaonyesha kuwa ‘kuna kitu’..hata hivyo hamna lisilozungumzika, japo kwa sasa yeye ameshika makali.. Nanyi bado mna umri mreefu wa kucheza na kutafuta riziki katikafani hii.. kwa nia ya kweli, tafuteni fursa ili utaratibu wa suluhu upite nasi tuwaone tena hivi karibuni mkiwa na Stars mkitupa burudani uwanjani.. UZENG

    ReplyDelete
  6. HARUNA HARUNA HARUNA...MBONA MAMBO YA BANGI HUJAZUNGUMZIA?? JE NI KWELI WEWE HUVUTI BANGI? MECHI YA KWANZA DHIDI YA SENEGAL ULICHEZA CHINI YA KIWANGO NA KOCHA AKAKUTOA KABLA YA HALF TIME WEWE ULICHUKIA SANA UKAGOMA HATA KUSHIKANA MKONO NA KOCHA!! SIKU HIZI KUNA LUNINGA SIO KAMA MIAKA ILE YA 70 TULIKUWA TUNADANGANYWA ETI REFA KATUUMA SIKU HIZO HILO HAKUNA.

    JE KATI YENU NANI HAVUTI BANGI? NA SWALI SI NANI ANAVUTA BANGI. NATAKA MUWE WAWAZI W=MAANA MMEAMUAKUSEMA KWELI.

    NURDIN MIMI BINAFSI NAKUPONGEZA SANA KWA KIWANGO KIZURI ULICHOKIONYESHA KULE WEQWE NDIE ULIKUWA BORA ZAIDI YA WOTE ILA HUONI KWAMBA UAMUZI WAKO ILIKUWA NI KAMA USALITI KWA WENZIO?

    ReplyDelete
  7. Hii ishu naona imegeuzwa kuwa ya kisiasa zaidi. Mimi naona Kocha kama Kocha ndio mwenye maamuzi ya juu ya nani amchezeshe na nani asimchezeshe na kwa sababu zipi. Hatakiwi kuingiliwa. Sasa inaonekana haya masuala watu hawayaelewi. Beckham alikuwa superstar tena kwenye peak akacheza unazi dhidi ya Arsenal Kwani Ferguson alimfanya nini? Kuna mtu aliyeuliza? Jaap Stam naye hivyo hivyo. Ukocha ni profession hutakiwi kumuingilia mtu au kumpangia na ndio maana tunabaki kupiga domo tu! Mwacheni Maximo kama mmemchoka basi atafutwe anayefaa afundishe mpira. Au hao wanaoongea wafundishe wao. Mpira ni nidhamu, Mazoezi na Kujituma. Na nidhamu sio kambini pekee, bali pia ni hata nje ya kambi au uwanjani. Wengi hili huwa hawalitambui. Wanaoongea kusema Maximo OOh! kafanya hili ni wanafiki tu! Wao kama ni wacheza mpira kazi yao ni kudhihirisha kuwa yaliyokuwa yanasemwa sio kweli au shutuma za kocha sio za kweli ni uwanjani na si kwingineko. Sio kuanza malumbano kwenye vyombo vya habari. Kwa hili mimi naona jamaa wamechemka.

    ReplyDelete
  8. Sina uhakika kama hii imeandikwa na wachezaji wenyewe maanake sababu zilizotolewa hapa ni za kitoto. Nadhani kisoka tumefikia point ambayo inaitwa zero tolerance ukizingatia miaka kibao ya kuwa na excuse na kuboronga. Kwa upande wa kocha ni lazima awe mkali, ukubwa jalala timu inapofanya vibaya kwa nyie kucheza chini ya viwango lawama zote zinaishia kwake.

    Mchezjai aliyesema alikuwa anaumwa mara akawa 100% story wala haiendani mtu akichunguza vizuri kuna walakini katika maelezo yako. Ikumbukwe kuna daktari wa timu ambaye kwa kutumia vipimo anaweza determine your fitness. Halafu wachezaji wengine mkajirundika na mgonjwa na kuwa against the coach hata kama mlizaliwa tumbo mmoja this is unacceptable. Kubwa hapo ilikuwa ni kuwakilisha Taifa.

    Labda nia ya wachezaji ilikuwa ni kuona coach anaondolewa kwa kufanya vibaya. Kusemwa na coach ilikuwa ni kitu cha kawaida kama tunavyosema na wazazi, walimu au wakubwa wetu maofisini. Kilichotakiwa hapo ni uvumilivu na kumuomba coach msamaha and ask for a second chance. Kama hili lingetokea nadhani tulikuwa na nafasi vizuri sana kwani kwenye mechi ya pili Ivory Coast presssure ilishapungua, na kwenye mechi ya Zambia ambao walisawazisha dakika za mwisho tungeweza kufanya vizuri zaidi.

    Hii kuuungana mkono toka Serengeti Boys inaweza kuchukuliwa kama some kind of mgomo baridi kwenye timu. Kuna kila sababu kuonyesha hatua zilizochukuliwa na coach zilikuwa ni sawa na nidhamu ni kitu muhimu especially kwa timu changa kama yetu.

    ReplyDelete
  9. Wameamua kuweka mambo wazi kwa kuwa mmeanza kuwasakama.Pia ni upuuzii kuwatenga watoto wako tena mko nchi za watu ni kweli Ferguson anafanya hivyi kama ni mifano yenu hiyo ya majuu?
    Pia utawanuniaje wachezaji uliowachagua wewe mwenyewe?
    Utamwambia mchezaji kuwa unaenda tu ila hutacheza naogopa kelele ?(huyu ni kocha kweli waungwana)
    Au ni wale wale tia maji tia maji ?
    Mtoto akikukosea mwite muulize nini leo mbona sio wewe.? una tatizo gani?
    Sio kununa....
    HAPA inaonekana jamaa mbabe mkubali mkatae mwenzie yule wa viungo alisema anarudi kwa familia yake saa yupo kwa Azam.SAsa hiyo familia nayo ipo hapa??????????????
    Ni wapongeze hao viiongozi wa msafara kwa kazi nzuri.
    PIA TUJUE KUWA sisi ndio tuliyopeleka timu ambayo ilicheza na Cameroon na Kina Diuof LAKINI wenzetu pamoja na hao SEnegal walipeleka timu tofauti na tuliyocheza nayo hakuna PAPA diopu wala MAMADU hata mataifa mengine pia ni hivyo hivyo sisi NI YULE TU ALIYE kuwait MRWANDA ndie hakuwepo.Hivyo hatuna haja ya kufurahia kwani timu yetu ndio TIMU PEKEE AMBAYO IMEKAA PAMOJA NA KUSHIRIKI MICHEZO MBALIMBALI KWA MUDA MREFU LAKINI HAKUNA JIPYA.
    IVory Coast sio ile ya Kiina Drogba Ghana sio ile ya kina ESSIEN.Ni wachezaji wachache na wametutoa jasho.Kwa hiyo tujue kuwa timu yetu ilitakiwa iwe na makali zaidi.Sumbua kichwa utajua zaidi

    ReplyDelete
  10. Kazi ya kocha,sie watanzania na mashabiki tunataka ushindi tu.
    Haya mengine hayatuhusu.

    ReplyDelete
  11. Hao wachezaji tatizo sio kocha bali kisaikolojia hawakuwa wameandaliwa.Kwa maelezo yao kwanza wanakili makosa yao kucheza chini ya kiwango chao,pili katika maelezo yao kitu kilichokua mbele sio uzalendo kwa taifa na timu yao bali masilahi yao binafsi kwani kama walivyosema kwamba Ivory coast walikwenda kutafuta nafasi ya kujionesha na hatimaye kununuliwa na klabu kubwa!Sikatai kila mtu anatamani maisha mazuri na mafanikio mazuri katika maisha.Hawa wachezaji kwa walioyaeleza inaonekana walipokua uwanjani kila mtu kivyake vyake walikua wakijitahidi kucheza kama mtu binafsi na sio kama timu hii utokea .badala ya mchezaji kutoa pasi kwa mchezaji abaye yuko katika nafasi nzuri ya kufunga anataka afunge yeye au kupiga chenga ili kujionyesha mategemeo yao yalikua zaidi katika ubinafsi na kusahau mpira ni timu na sio mtu mmoja binafsi ingawa kila mtu anakipaji chake binafsi.Hayo ndiyo matatizo ya wachezaji hao na cha ajabu kwa mtu anaae fikiri haya maelezo yao hayakuwaongezea sifa yoyote bali kuwaondolea yametupa nafasi ya kufahamu sio mapungufu ya kocha bali mapungufu yao.Hawa wachezaji kama angelikuja mtu mwenyepesa na kuwambia isaliti timu yenu ifungwe nitawafanyia mpango kuchezea timu za ulaya WANGEFANYA HIVYO!Kocha kwa vitendo hivyo uwa wakali kwani mchezaji anacheza chini ya kiwango chake kutokana na kua na kibarua cha ziada kichwani mwake mbali na maelekezo ya kocha.Mchezaji kukemewa na kocha wakati mwingine kupata ata kipigo ni kawaidakwa klabu za ulaya ifikia hata mchezaji kukatwa mshahara wake.Kwa maoni yangu wachezaji hao walichokifanya kuaandika malalamiko kuhusu kocha si sahihi wanapashwa kuomba msamaha.Nakwa upande wa viongozi wetu wa michezo wanapashwa kuchukua hatua kua timu yetu inaandamana na wataala wa kutosha wakiwemo masaikolojisti kuliko viongozi kibao -Watalii-Hainiingi kichwani wakati timu ya taifa iko katika michezo waziri wa utamaduni anatembelea miradi ya kuotesha kahawa!Waziri wakilimo akienda kwenye mikutano inayohusu kilimo atembelee viwanja vya nyasi bandia!?NAISHUKURU TIMU YETU,KOCHA NA WACHEZAJI KWA KILE WALICHOKIFANYA TATIZO LETU HATUKUA NA WANASAIKOLOJIA MUNGU IBARIKI TANZANIA.

    ReplyDelete
  12. Hapo wote hawana point, ni longo lngo tu za kiswahili,kwa hiyo kocha asikuseme. aaaaaaaaaaaaaaahhhhh, mambo gani. eti nilipanic kwa hiyo nilicheza chini ya kiwango, sasa kama unajua kosa lako kwanini umlaumu maximo huku ushaicost nchi. kaani nje hukooooooo. Vaeni hayo masuti yenu basi.

    ReplyDelete
  13. Yah,nachelea kuamini kila kitu sababu haruna hajaongelea kutokumpa kocha mkono na uvutaji wa bangi!anyway,kwanza Maftah, na Kevin nyie kwa sasa hamna namba ktk 1st eleven,kwa hiyo msitafute visingizio (Jabu na Canavaro wameshawanyan'ganya namba).Nurdin mi sioni kama umo ktk bifu,umepangwa na umecheza vizuri, Bony nadhani umri unakutupa mkono,kiwango chako kinashuka siku hadi siku, naelekea 30, na kwa wachezaji wengi Tz huo ni mwisho wao (hasa wanapotoka timu za majeshi,si tunakumbuka Kasonso wa simba?. Halafu Haruna,hata simba mpaka leo kambini hujaripoti, unanikumbusha matatizo uliyokuwa nayo wakati unafundishwa na marehemu Kinanda.If i were Maximo, Only Nurdin angebaki ktk timu kati ya hao wote

    ReplyDelete
  14. Mliyoyasema hapa yanafanana na ukweli lakini huenda ni kujisafisha na hata kama ni kujisafisha bado nyie wote mnaonyesha kuwa hamuwezi kucheza ulaya kwa sababu ya hasira zenu za kitoto. Chuji wewe ni mchezaji mzuri sana tena saana ukiwa uwanjani. Lakini ilitakiwa uwe mvumilivu tu. Kwa kutokuwa mvumilivu, umekosa kuonekana. Wakati mwingine inatakiwa umtumikie kafiri upate mradi wako. Mimi nilishangaa kwa kweli kwanini mechi ya kwanza hukupangwa. Na kusema kweli kinachonifanya nifikiri kuwa wakati mwingine hawa wachezaji waliingiwa na hasira na wakasema mbovu kwa kocha ni kuwa, kwanini Chuji asipangwe? Mimi nina uhakika Chuji ni kiungo ambaye amependwa sana na kocha na ndio maana nadhani kuna kitu tu.
    Jamani, mchezo wa mpira wa miguu unahitaji nidhamu ya hali ya juu. Na wachezaji wanatakiwa wakati mwingine hata wakiudhiwa wavumilie. Mimi nimehuzunika sana kutomwona Chuji kwenye Runinga.
    Nawapa pole sana

    ReplyDelete
  15. Kuna mtu ameongea point hapo juu ni kweli mpira au mchezo wowote ni una mambo makuu haya, Nidhamu, Mazoezi, Ufanisi na Kujituma. Hivi hata Movie mnaangalia nyie kina Haruna? Angalieni "Coach Carter" at least u will understand what most of people here are saying. Grow up guys, mambo yenu ni ya kitoto sana, mtu umecheza chini ya kiwango unataka upewe zawadi? C'on guys!!!!!!

    ReplyDelete
  16. Haya maelezo yanaonyesha wachezaji
    wanajielewa kiwango cha mpira walichonacho ni cha Taifa hawana kabisa nidhamu au kiwango cha kimataifa wanastahiri kuwekwa pembeni kwa muda "ADHABU-NIDHAMU"

    Siwakumbuki wachezaji wengine kati yao zaidi Haruna Moshi alipokuja Denmark alikuwa kipaji cha hali ya juu kwa wakati ule,lakini kama hataki kujielewa kuwa mchezaji wa kimataifa wa malipo kunaitaji kuanzia nchini kwake kama mchezaji mzuri mwenye nidhamu wa "Clubyake" na "Taifalake" bila ya hivyo hatofika mbali, maana umri wake unakimbia.
    wachezaji wote wa bara la Africa kwa sasa ni wachezaji wa malipo wana nidhamu na kujielewa wana jukumu la Taifa lao na kimataifa kama wachezaji wa kulipwa.

    Kuteuliwa kwa mchezaji aliyekuwepo katika "matibabu" bila ya kucheza ni mojawapo ya njia inayotumika kwa timu zote za kimataifa, kuwapa nafasi wachezaji wasiwe mbali na mchezo hakuna kosa lolote hapo mwalimu MAXIMO na msaidizi wake El-BASHIR walilolifanya.

    Lakini ukosefu wa nidhamu au kutoelewa kimataifa,wameona kama wamekosewa kuteuliwa bila kucheza,
    wanayo haki kuongea na wana-habari wanao uhuru wa kujielezea binafsi lakini kuyaelezea ya kutoka kambini kwa makosa ya kujitakia ni sawa na kuomba msaada wa "media" kuwatetea,kinachohitajika kwa sasa "nidhamu na matokeo" ya mchezo kimataifa.

    "WATANZANIA WOTE WAMETOA MCHANGO WA KUWAPA MOYO NA MATUMAINI WACHEZAJI"

    mickey@mail-online.dk
    DENMARK

    ReplyDelete
  17. Haya yooooote ni majungu tu. Na nina imani kuwa sasa hivi mpo kwenye kampeni ya kutaka Maximo aondoke ili kwani manjua kuwa ninyi sasa timu ya Taifa basi. Ukweli ni kwamba huwezi kujipangia au kukamia kucheza kiwango cha juu ili uonekane kimataifa na kuchukuliwa na Liverpool et al, Cha kwanza ni kucheza ili uipe ushindi timu yako hayo mengine huja baadae.

    Halafu ninyi tayari ni wazee, sasa hivi tunahitaji vijana watakaojua kuwa mpira ni profession siyo sehemu ya majungu. Mimi mwenyewe ukiniuzi ntakuchunia tu kwa nini uharibu wakati nimeshakufundisha kila kitu?. Mpaka ukijirekebisha ndiyo tutakuwa pamoja, Maximo hakuja kumfurahisha Chuji na wenzake yeye amekuja kufundisha mpira sasa kama wewe hufundishiki unatarajia mtapatana. Tena kama angetumia "Mnali's Theory", angefanya vizuri sana. Wewe umepewa nafasi na watanzania kuwawakilisha unafikiria ucheze ili uonekane badala ya kuiletea timu ushindi?, hii kitu imenifanya nianze kuwaza kuwa Tanzania sasa kuna haja ya kuingiza somo la football katika mitaala ya shule za msingi na mpaka vyuo tena iwe ya lazima na watu wasome kiingereza. Haya mambo ya kuchukua watu vijiweni ambao wamekimbia shule na kung'ang'ania mpira kama only means ndiyo yanatuletea watu wenye mawazo kama haya.

    Kwa nini usema Maximo kauacha wewe kwa sababu ya association yako na Chuji?, unaweza kututhibitishia kwa maneno kuwa "alikutamkia ukiwa karibu na chuji sikupangi?", ukithibisha hili mimi ntaona ninyi mnakesi ya kuhoji, vingievyo ni "MAJUNGU" ya kila mwaka yanayoturudisha nyuma kimpira. Tatizo lenu mnaleta U-yanga na U-simba kwenye timu ya Taifa UPUUZI MTUPU>

    ReplyDelete
  18. Maximo tu hivyo je ukikutana na Sir Alex si utakimbilia uvunguni? Hiyo tabia waliyo nayo hawa madogo na wengi wetu toka Tanzania ndiyo inayotufanya kushindwa kucheza soka maulaya.

    ReplyDelete
  19. hawa watoto wasituletee masihara... tunataka kurudisha jina la Tanzania kwenye sura ya dunia... halafu wapuuzi wachache hawataki kufuata ushauri wa kocha... WHY??????????? wanapashwa wajue kwamba wao ni profesionals! mambo ya bla bla waache. wajifunze nidhamu, uzalendo, utii na kujituma kwa kiwango cha juu kabisa. kocha hana tatizo, anatimiza lengo! mmoja akiharibu, na rafiki yake pia hafai... (influencing power) inakuwepo. JAMANI, HAWA WACHEZAJI WAKAE NA DARASANI ILI WAELEWE HILI! KOCHA YUPO SAWA KABISA, NIA NI USHINDI NA TEAM SPIRIT!

    TUACHE BLA BLA... KWENYE MPIRA HAKUNA POLITIKI JAMANI. ACHENI UJINGA MADOGO... KAMWOMBENI MSAMAHA KOCHA KAMA HAMNA 'HIDDEN AGENDA'

    ReplyDelete
  20. acheni utoto, Teven wa MAN U ni mkali sana, anaweza cheza ligi yoyote, anapigwa benchi lakini hawezi kumkosea adabu babu Feg. na mashabiki wa MAN U, sasa nyie kupigwa benchi ndio iwe sababu ya kususia timu ya Taifa na kumchukia kocha? hata kama kocha amekosea kukuweka benchi au nje ya timu, piga mpira hadi urudi kwenye kiwango. Kwa kuwasaidia tu: pigeni magoti muombe msamaha, nafikiri mtasamehewa na mkirudi mpige sana tizi ili muwe juu

    ReplyDelete
  21. Duuh! kumbe ndiyo hivyo,basi MAXIMO hana NIDHAMU, Sio wachezaji.

    Mara ngapi ROONEY anatolewa na FAGASON kisha anatukana na kupiga bench kuashilia hakulizika lakini mbona next mechi tunaona mambo shwali.
    hata kama Boban alikasirika Kwanini Maximo akatae HI,MAXIMO HATUFAI,HANA NIDHAMU, HAYUKO FAIR

    ReplyDelete
  22. Inatia huruma sana kuona vijana wa kutegemewa wanachemka hivi!!!!
    Tulitegemea wayamalize huko na wataalamu wa haya mambo si magazetini (au bloguni) tatizo washabiki wao na wao wajinga kama wao!
    Wanawaponza.
    Watanzania tunachowapendea ni mpira tu, kama haupo, wapenzi utakaobaki nao ni wale wa zamani.
    Sasa haya maelezo ya nini?
    Cha msingi fanya juu chini urudi uwanjani ucheze, ndio thamani yako itaonekana kwetu ambao tulikujulia uwanjani.

    Ila jaribuni kutafakari fani mliopo. Ni fani ambayo inategemea uongozi, na uongozi wenyewe mara nyingi ni wa imla.
    Hivyo inapokuwa unakushinda, kufuata amri saa 24, bora ujitafutie ajira ingine, uwe meneja wako, hata sie tulioko huku kwingine, kukichoka na mwajiri tunahama au tunajiajiri!

    ReplyDelete
  23. Kwa maelezo haya wachezaji wanamakosa yao na kocha ana makosa yake. Naona kuna watu hawapendi Maximo asemwe hata akifanya kosa, lazima tufahamu kuwa kocha ni binadamu na anafanya makosa kwa hiyo tukubali anapokosolewa na yeye anajua kuwa anatetewa sana kwa hiyo anafanya vyovyote. Niliwahi kusema kuwa inaelekea anafanya mambo "kiswahili" na maana yangu ndio haya mambo wanayoeleza wachezaji. Huyu uwezo wake umefikia mwisho mwalimu aliyefundisha vizuri shule ya msingi hawezi kupelekwa kufudisha sekondari kwa kigezo hicho. Tunamshukuru kwa alipotutoa na kutufikisha hapa, sasa tunahitaji mwingine atupeleke mbele vinginevyo itakuwa sawa na mfano wa mwalimu wa msingi.

    ReplyDelete
  24. POINTI ZOTE WALIZOZUNGUMZA HAO WACHEZAJI NI DHAIFU.NI UZEMBE NA TABIA MBAYA NA SASA WANATAKA WAONEWE HURUMA NA KOCHA.SWALI NI KWANINI UCHEZE CHINI YA KIWANGO? NA WAKATI UMEFUNDISHWA NA UKASEMA UMEELEWA SOMO.JE HAWAKUJUA KUCHEZA KWAO CHINI YA KIWANGO KUMEIANGUSHA TIMU NZIMA..WACHEZAJI NA KOCHA NA TAIFA ZIMA?NIMESOMA HIZO POINTI ZAO NI KICHEKESHO UTAJUA MOJA KWA MOJA TATIZO NI LA WACHEZAJI.MIMI NINGEWAAMBIA SASA KAMA UMECHEZA CHINI YA KIWANGO BASI HAMFAI..MNATAKA NINI TENA.MMEPEWA NAFASI MMESHINDWA KUITUMIA SASA MNALALAMIKA NINI?NDIO KOCHA ANA HAKI YA KUWASEMA YEYE NI MWALIMU NA MWALIMU ANA HAKI YA KUULIZA UNAPOFELI HATA KAMA NI KWA DAKIKA 30 ANAYO HAKI KWA SABABU ATAULIZWA YEYE.WATANZANIA TUNA MATATIZO TUKIELIMISHWA TUNAKUJA JUU TATIZO UELEWA WA WATU WENGINE MDOGO HATA MLETEWE KOCHA TOKA MBINGUNI KAMA HAMTABADILI UELEWA WENU MTABAKIA PALE PALE.USWAHILI NA MAJUNGU SIKU ZOTE.

    ReplyDelete
  25. inasikitisha kuona hao ndio wachezaji wetu timu ya taifa (unprofessional)kabisa.NI YUPI ALIEONEWA SASA HAPO??HAPA TUSIDANGANYANE BWANA ISSUE NI BANGI TU HAMNA CHA ZIADA THAT`S IT.WALALAMIKAJI WOTE NISHAVUTA NAO SANA BANGI TENA NI MAJIKO HASWA HASWA SIWAZINGIZII.TUANZE NA CHUJI;KOCHA NDIE MWENYE JUKUMU NANI ACHEZE NA NANI ASICHEZE HAINIINGII KABISA AKILINI MAXIMO ANAVYOPENDA USHINDI ASIKUPANGE WAKATI ANAJUA UNGEWEZA KUMSAIDIA.NENDA KISHA RUDI NA SABABU NYINGINE YA MAANA ZAIDI YA HIO HATUTAKI MCHEZOMCHEZO HAPA MKIAMBIWA BANGE ZINATIA KIBURI NA KISIRANI MNABISHA UNAONA SASA???HARUNA:HAIWEZEKANI IKAWA KILA SEHEMU UNAONEWA WEWE TU WAAMUZI,TFF,WACHEZAJI WENZIO LAZIMA WEWE NDIO TATIZO LAKO MWENYEWE TU.HUNA SIFA ZA KUWA MCHEZAJI WA TIMU YA TAIFA NA WALA HUNA SIFA ZA KUCHEZA NJE YA BONGO AMBAKO WATU HAWATAKI MZAHA NA SOKA KWAVILE WAMEWEKEZA PESA ZAO NYINGI NA WEE UTALETA KIBURI CHAKO CHA BANGE.NASHANGAA UMESHINDWA OMAN TENA DARAJA LA CHINI NDIO UTAWEZA ULAYA WEWE??YAANI UMEFIKIA KIASI UNAVURUNDA UWANJANI UNATAKA BADO UANGALIWE TU KWAVILE HARUNA MOSHI??MI NINGEKUWA KOCHA NINGEKUTOA MAPEMA ZAIDI YA HAPO I SWEAR MY GOD ONA MECHI AMBAYO HUKUVAA HATA JEZI VIJANA WAMESHINDA.MAFTAH:I FEEL SORRY FOR U MY FRIEND U ARE JUST LUCKY U DONT DESERVE TO BE IN THE SQUARD TUAMBIE ULITAKA NANI AKAE NJE ILI UANZE WEWE??NSAJIGWA AU JUMA JABU??YONDANI:KIDOGO NIMEKUELEWA UMEONGEA MTAZAMO WAKO NA UPO SAHIHI GAME ULIIPANIA IKAKUKATAA IT HAPPENS SOMETIMES NA PIA NADHANI ONGEZA BIDII NAUKUBALI UWEZO WAKO.NURDIN:SIO KWAVILE FULANI NI BEST YAKO NDIO UMTETEE HATA ANAPOKOSEA TABIA ZA KISHKAJI KAZINI NDIO UFISADI PROFESSIONALLY ULITAKIWA UWE MUWAZI KWA BEST YAKO CHUJI BIG UP ILA PUNGUZA BANGI NA WEWE CHEZA SOKA.HAWA JAMAA WADAU WOTE MI NAVUTA NAO BANGI NA PLACE YETU KUBWA YA KUVUTIA NI SINZA.WAMEONYESHA U-SELFISH WA HALI YA JUU KUJIONA WAO NI BORA ZAIDI YA WACHEZAJI WENGINE WA STARS WHICH IS PLAIN WRONG.WACHEZAJI WOTE WALIOCHEZA TAIFA LIMEWAAMINI NA WALISTAHILI KUWAKILISHA NCHI KAMA KOCHA ALIONA HIVYO

    ReplyDelete
  26. Acheni uswahili kazini, watu wazima wanalalamika kama vitoto vya mama wa kambo.

    We unataka kuchekewa kazini wakati unaharibu. Kumbe ndo maana huwa hatufiki mbali na makocha wetu.

    Mi naona maximo anafanya vizuri kikazi, na ni bosi ambaye lazima ahakiki nidhamu kazini. Vijana wanaleta dharau na utani kazini.

    Panatakiwa pawe na somo la nidhamu kazini.

    KAZI SIYO MAPENZI NI UCHUMI.

    ReplyDelete
  27. USHAURI WANGU MMOJA TU KWENU WOTE WACHEZAJI WABONGO.VIPAJI MLIOKUWA NAVYO NA MNAVYOHISI MNAVYO KAMA HAMTOTAKA KUJIENDELEZA ZAIDI YA HAPO MLIPO NA KUJITUMA ZAIDI KUCHEZA SOKA LA NJE ZAIDI YA TANZANIA MTAKUWA AMFIKI POPOTE NA BAADA YA MIAKA MITATU TU WOTE MTABAKI MAJINA MNAANZA KUTEMBEA TEMBEA OVYO MITAANI MNALIA SHIDA,NASEMA HIVI SIO KU WAKEJELI BALI NI UKWELI HALISI WA SOKA LETU NYUMBANI NA WOTE MNAWAONA WALIOVUMA ZAMANI MITAANI.
    SASA MNAPATA NAFASI YA KUITWA TIMU YA TAIFA BADALA YA KUONESHA VIPAJI VYENU KWA WAKALA WA NJE HILI MSONGE MBELE KIMCHEZO NA KIUCHUMI MNAOTA PEMBE NA KUSHINDWA KUJUA KWAMBA KOCHA NDIO MWENYE NENO LA MWISHO POPTE DUNIANI.MIGOGORO YA MAKOCHA SIO MAXIMO TU MAKOCHA KIBAO WANAKUWA NA MIGOGORO NA WACHEZAJI WAO MARA KWA MARA NA NIKAWAIDA.NIKACHO WAPA JEURI WACHEZAJI WAKUBWA NI KWAMBA WASHAJIJENGA VIZURI KIMAISHA NA POPTE PALE WANAPATA TIMU.SASA KAMA NYIE MMERIDHIKA NA HAPO MLIPO BASI ENDELEENI KUKAA NAYO HAYO MAPEMBE NA KAMA MNAJIONA MNA HAMU YA KUFIKA MBALI BASI KATENI MAPEMBE YENU NA MUANZE KUJITUMA ZAIDI HILI MKACHEZA NCHI ZA NJE MLIPWE VIZURI.
    NAFASI HIZI NI CHACHE SANA NA UKISHINDWA KUZITUMIA UTAKUJA KUJUTA BAADAE.
    NAKUMBUKENI SOKA NI MCHEZO UNAOTOA VIPAJI VIPYA KILA SIKU,SASA MKIJIONA KWAMBA NYIE NDIO BORA ZAIDI MTAKUJA KUSHANGAA CHIPUKIZI ANAKUJA MPYA AMBAYE YUKO JUU ZAIDI NA WASHABIKI HAO HAO WANAOWATETEA WAKAWASAHAU.
    MDAU wa soka la biashara.

    ReplyDelete
  28. Tunataka kocha anayetabasamu tu wachezaji wanapoboronga? Wachezaji wamekiri kucheza chini ya kiwango, na wanawaomba msamaha watanzania kwa utovu wa nidhamu uliofuatia baada ya kocha kuwachukulia hatua za kinidhamu. Kuboronga katika mechi ile ya kwanza ndiyo kulikotufungisha virago, hatujui hilo? Jamani tunahitaji watu serious kama Maximo pia katika serikali yetu. Mafisadi wametutesa sana kwa kutunyima mafanikio katika kila nyanja ikiwemo uchumi na michezo. Hivyo, kiongozi jasiri aina ya Maximo anayeweza kutoa kibano kibano kikali kabisa bila woga kwa mafisadi wote na washirika wao anahitajika nchini kwetu!! Wachezaji kama mlivyoungana kujitetea hapa, onyesheni ukomavu kwa kumuomba Kocha msamaha kwa kumkosea heshima. Kutengeneza kundi dhidi ya Kocha hakutawasaidia lolote!!

    Mdau..TRD

    ReplyDelete
  29. "TULIMWELEZA WAZIRI BILA KUBAKIZA" NA MAJUMUISHO (CONCLUSION) WALIYOITOA INAONYESHA WANAO UWEZO MDOGO WA KUFIKIRI NA KUELEWA.NIMESOMA HIYO TAARIFA NI KICHEKESHO NA AIBU..KUMBE KOSA WANALO...KUCHEZA VIBAYA NA KUFANYA TIMU ISHINDWE.BASI TUMESHAPATA JIBU.SASA KAMA UMECHEZA CHINI YA KIWANGO HILO NI KOSA LAKO MCHEZAJI SASA UPANGWE MECHI NYINGINE UBURUNDE TENA? SAHAU!KWA SABABU UNAOGOPWA?HIYO NI SAWA UMEPEWA KAZI UKAHARIBU NA KULETA HASARA..JE KWA KUHARIBU KWA NINI USIFUKUZWE?UELEWA MDOGO NA USWAHILI UNACHANGIA HAYA MATATIZO YOTE..NIMESOMA HIYO TAARIFA NI UPUUZI MTUPU.

    ReplyDelete
  30. Watu wanasahau mambo upesi sana. Kabla Sir Ferguson hajamtema Beckham ManU alishawahi kumtandika daluga usoni. Beckham angekuwa mbongo sijui angefanyeje lakini angalieni nyota yake inavyoendelea kung'ara. Maximo bado hajamtupia mtu daluga.

    ReplyDelete
  31. Mdau wa 7:01

    Naungana na wewe kwenye vipaji vipya. Tatizo la wachezaji wetu wakiona kipaji kipya wanatafuta njia ya kukishusha ili wasinyang'anywe namba badala ya kuongeza juhudi na kujituma zaidi wasitupwe. Wachezaji wengi sana ni wateja wakubwa wa kwa bibi nyau, wanapewa vidawa vya kienyeji wanaona basi ni kila kitu hata wakifika uwanjani wanajua wanadawa, mazoezini hawaendi, kocha asipowanga wanamloga awapende na kuwapanga badala ya kuweka juhudi kwenye mazoezi na kujituma uwanjani. Hawa ndiyo wachezaji wetu wanaotaka waonekane kwenye soka la kimataifa kwa mechi tatu tu za CHAN, Kama wangekuwa na lengo hilo wangejihidi wapate mechi zote tano. Hawa mi wala siwasikitii Maximo Oyeeee!!!

    ReplyDelete
  32. Big up watanzania. Haya majungu na hadithi za "he said she said". Not an excuse. Nidhamu, utii, kujishusha na kukubaliana na hali na mazingira. Kama jeshini tu-cha msingi ushindi na to hell with visingizioz. Too childish, too much politics na kuchonga jadi yetu.

    Wachezaji angalieni ushindi, future yenu na sio kujiona babkubwa na sasa mnataka support ya watanzania na kumuondoa kocha.

    Mastaa wa bongo inatosha kuonekana kwenye tv na magazeti na sio kasi ya ushindi kwa kila hali na mazingira.

    No good excuse for failure.
    Acheni usupastaa mchangani

    ReplyDelete
  33. Hii taarifa kweli ni kichekesho, hivi kweli nyie vijana mko seriuos?

    Nina hakika 100% kuna mtu amewadanganya na amewaandikia hii taarifa kwa manufaa yake binasfi na kundi lake. Kama mngekuwa mmeshauriwa vizuri basi mngekwenda kwa Mwalimu wenu kuomba msamaha na si vinginevyo.

    Kazi ya mwalimu ni kufundisha na kupanga timu, kazi yenu ninyi sio kuifanya kazi mwalimu iwe ngumu au ishindikane. Kwa kifupi Maximo was very right hawezi kufanya kazi zake juu ya wachezaji, yeyote anayekwenda kinyume na maelekezo yake will responsible na face consequences. Hii ipo hata kwenye maofisi yetu, umeshindwa kufuata maelezo ya kazi yako, you will be fired na kesho yake anaajiriwa mwingine aliyetayari kufuata maelekezo na dunia inakwenda mbele. Kaaeni mkielewa kwenye profession hakuna mchezo ukitaka kumuonesha bosi wako wewe ni zaidi kuliko yeye kwa ujinga-ujinga unapigwa chini kwani utakwamisha maendeleo au kazi.

    Tena naona hao vijana wasirudushwe tena kuvaa jezi za Taifa Stars, kama kuna mtu anawapenda sana basi awafuate huko vilabuni mwao akacheze nao danadana.

    ReplyDelete
  34. Timu ya mpira inatakiwa inacheza kama platoon ya jeshi. Yaani mko wote no matter what and u listen to the leader, period. Hapo ndio unapata team working under trong leadership. Ulizeni story za ndani za Fergie na David Beckam. Hakuna kubembelezana ni mkwara hadi mtu anadhani ni mwisho wa dunia. Wacheza wetu kama wanataka kuingia ulingo wa kimataifa, hilo ni lazima liwepo.

    Pamoja na yote mmefanya vizuri hadi mlipofika ila tunajua mngeweza kutuvusha zaidi kama mngekuwa mmefuliwa kitabia. Sasa mnajua what to expect. Msife moyo, ni kujifunza na UMOJA uzidi.

    ReplyDelete
  35. HII MAANA YAKE NINI?
    maana yake kwamba soka la Tanzania ni chnag mno na wanasoka wake ndio hivo hivo.
    Mchezaji wa Taifa iweje uanze kutapika matapish mazito kama haya kupitia mtandaoni? U wapi uprofesheni?
    Nahapo ndipo unaposhindwa kushangaa kwa nini kiwango cha Tifa Staz ni cha chini mno. Niliangaliza mechi zetu za CHAN kupitia mtandao, sikuona mchezaji yoyote a maana, nikabaki kujiuliza wako wapi wale kina Hussein Masha, Hamza Mponda, Felician Fumo, Abdallah Burhani, Peter Tino, Zamoyoni Mogella, Beya Simba, Yahya Tostao, Alphonse Modest, na wengineo waliotingisha enzi hizo?
    Hawa jamaa wa leo, ashakum si matusi, ni cha mtoto tu, hawana spidi ya kusakata kandanda, wako doro ile mbaya ake.
    Na ndio hayo yanayoweza kumhamakisha meneja wa timu. achezaji wetu hawana maturity ya kutambua uzito wa mechi wanayocheza. Eti wengine hujig=fanyaga hata kususa.
    Na kama hayo hayatoshi, eti nao leo wanajitumbukiza katika malumbano ya kujibu hoja kupitia blogu. Maana yake nini?
    Kwa kweli tuna safari ndefu sana kufika wenzetu walipofika. Kwa mentality hizi, hata aje Maurinho soka letu litaendele tu kudorora, vijana bado vichwa vyao havijapevuka.
    Mndengereko,Ukerewe

    ReplyDelete
  36. Wadau wa soka,
    Nafikiri mnakumbuka hii mada tulipoileta ni kabla ya hawa wadogo zetu hawajaleta malalamiko yao. Wadau tumejaribu kuonesha wazi assessment yetu juu ya management ya Maximo kwa Stars. Sasa nataka niwashirikishe jambo ninaloamini na ninalolifahamu.

    Maximo ametusaidia kwa kiwango chake. Pia mazingira aliyoyakuta wenzake wa nyuma wala hawakubahatika kuyapata. Tunakumbuka Mkwasa, Mshindo Msola, Kibadeni nk walivyokopwa hata posho ya kutunza familia zao wakiwa makocha Stars. Kambi ilikuwa inakopwa Jeshi la Wokovu. Ubora wa TFF umeweka mazingira ya kukuza soka.

    Ujio wa Maximo:
    Ni muhimu wadau kujua kuwa Maximo hakuwa chaguo la TFF. Alichaguliwa na Kikwete (kama anavyochaguliwa mkuu wa wilaya) na hata TFF hawakujua katokea wapi?

    Kwa nini ni muhimu kuwa na kocha aliyechaguliwa na TFF?

    According to TFF, kocha waliyekuwa wanamhitaji ni atakayeendana na mikakati ya TFF ya kuinua kiwango cha soka Tanzania nzima (hapa ieleweke kuwa si Timu ya Taifa tu). Kama mnavyoshuhudia TFF inaleta mabadiliko mengi kwa kutumia sheria, kanuni na taratibu za kisoka incl. vilabu kuwa na timu za vijana na wanawake, Copa Coca cola, Taifa Cup, viongozi watendaji wa kuajiriwa na mikataba kwa wachezaji, TFF iwe institution (si ya mtu 1) nk. Lengo ni kuinua soka NCHI nzima. Sifa za kocha ambaye TFF walimhitaji ni pamoja na
    1. kufundisha soka,
    2. kufundisha makocha wa hapa kwetu na
    3. kuisaidia Tanzania kutekeleza mikakati yake ya muda mfupi, wa kati na mrefu kuendeleza soka.

    Hivyo, sifa za kocha waliyemtaka TFF ilikuwa awe pia ni MKUFUNZI (instructor) anayetambulika na FIFA.

    Nakumbuka TFF waliomba FIFA iwasaidie kutafuta kocha wa sifa hizo ili aje kujenga soka, kukuza na kulea vipaji vya vijana wetu. FIFA ilitoa ushirikiano na TFF waliongea na:

    a. kocha wa zamani wa Cameroon akawa very expensive. Pesa za kusaini mkataba tu (acha mshahara ilikuwa mara 2 ya mshahara wa Maximo kwa miaka 2).

    b. kocha wa Kongo DCR akawa anataka TFF isubiri hadi Juni amalize mkataba na Kongo wakati sisi tukikabiliwa na Africa/World Cup qualifiers July.

    Hapa alikuwa anatafutwa kocha mwenye uzoefu na mazingira ya Afrika ambaye kazi yake inakuwa kubwa (kufundisha timu, kusimamia kocha wa vijana, wanawake, kufundisha makocha wa vilabu, kutoa technical support kwa TFF ku-implement Strategy yake, etc). Bahati FIFA wakatuunganisha kwa Leal ambaye FIFA wanamkubali kwa hali ya kisoka ya Tanzania. Na kwenye mechi ya Community Shield kati ya Man U na Liverpool (kama sikosei), commentator alimwonesha akiwa jukwaani na kusema kabisa kuwa yuko kwenye mazungumzo na Tanzania. Ni kocha na mkufunzi wa muda mrefu anayetambuliwa na FIFA. Pia ni M-Brazili kama Maximo.

    Kufumba na kufumbua serikali ikaja na jina la Maximo na haikujulikana anatokea wapi {ingawa aliwahi kufundisha timu ya Livingstone (nirekebishwe km nimekosea) ya Scotland kwa muda}. TFF wakaduwaa na hawakuwa na cha kufanya. Kwa hiyo haya yanayotokea hatushangai kwani Maximo hana uzoefu na timu za taifa, si mkufunzi (hivyo suala la saikolojia ni doubtful) na hata kufundisha makocha wa ndani hajafanya. Hivyo, lengo la TFF bado liko mbali kufikiwa. Hizo zifa zinazotajwa tumshukuru lakini kwa kweli TFF walidhamiria kukuza soka kwa mapana yake. Tunachokiona ni kuchukua wachezaji Yanga (10), Simba (6), Mtibwa (3), na wawili watatu wa hapa na pale. Na kuwabadilisha kila siku.

    Nilisukumwa kutoa mada kutokana na inconsistency za Maximo (of course na "ufungwa" wa TFF). Kwa upande wa Maximo

    1. Alitamba CHAN Ivory Coast kuwa anajivunia kikosi chake kwani ni vijana tupu, average age ni 22 years (refer to www.cafonline.com). Leo kaja nyumbani anataka timu iwe 70% vijana.

    2. Kila siku husema huchagua wachezaji kuzingatia rekodi yao ya NIDHAMU,nk. Sasa hao wooooote aliyewahi kuwachagua hakujua rekodi zao????????

    3. Kwa kipindi chote alichokuwa nao NIDHAMU imeshuka wiki moja ya kuwa Ivory Coast???

    4. Yeye kama mwalimu alifanya jitihada gani kuwaweka kwenye mstari????

    5. Je anatoa motisha gani kwa wachezaji wazoefu ili kuwajenga wale wadogo kisaikolojia? Au anawa-treat wale wakubwa sawa na wadogo? Yaani Ferguson am-treat van Der Sar,Rio Ferdinand,Giggs sawa na Luis Nani,Anderson,Welbeck????? Saikolojia inakuja hapo.

    6. Ana ushirikiano wa namna gani na makocha wa ndani??

    7. Hukaa na makocha wa vilabu anakotoa wachezaji kujua wachezaji anaodhamiria kuwachagua?

    8. Akiwaambia wanahabari kuhusu nidhamu mbaya za wachezaji, je huwa wazi ili hata wachezaji wengine (na wadau) wajue na kujifunza???

    Nafikiri jibu analo Maximo mwenyewe.

    Kwa upande wa TFF, wala wasirudi nyuma. Lengo libaki pale pale kuendeleza mpira wa Tanzania kwa ujumla...si Stars pekee. Hivyo TFF imwache Maximo amalize muda wake. Kikwete kawaambia TFF wajiandae kumlipa kocha wa Taifa,hatamlipa tena. Nafikiri wakati umefika wa kutafuta kocha mwenye sifa zile mlizozitaka (coach, Instructor na mwenye kulea wachezaji na mpira kwa ujumla). Yeye amalize muda wake lakini kwa sasa ni kumtafuta mrithi wake mapema na kutafuta wadhamini/mipango ya kumlipa. La sivyo, tutaendelea ku-implement hiyo Strategy nusu nusu.

    Ieleweke kuwa TFF ililazimika kumkubali Maximo kwa kuwa aliletwa na Kikwete. {Mnakumbuka Kikwete kwenye Press Conference aliwashutumu wazi wazi TFF kuwa yeye katoa ofa ya kumlipa kocha wa Stars na TFF wamelala tu. Of course, hii kauli iliwachoma TFF kwa kuwa walikuwa wanahangaika usiku na mchana kutafuta kwa kutumia msaada wa FIFA ila wengi walikuwa ghali mno kwa serikali kumudu kwani Tanzania si soka tu. Michezo mingine na uchumi vinadai. TFF walikuwa very considerate kwa wa-TZ}. Kwenye hili, kauli ya Kikwete ilitusononesha wadau tuliokuwa tunajua harakati za TFF.

    TFF iache tabia za kizamani. TFF inasema inamsubiri Maximo aseme chochote kile juu ya wachezaji wasio na NIDHAMU ili wachukue hatua. Yaani hata kama Maximo ndiye mwenye makosa? TFF wawaweke chini na kuyamaliza. TFF haifikirii hilo. Badala take wanasubiri Maximo aseme anataka TFF ifanye nini kwa watovu wa nidhamu. Nafikiri hii ni uzamani. Namna nzuri ya kuboresha management ya soka ni kuwa pro-active si reactive. Pia, hata bila ya Maximo kusema, itumike ripoti ya meneja wa Timu na TFF iwaite wachezaji wale waandike maelezo yao na kamati ya nidhamu iwahoji na wamsikilize Maximo na mwisho (mara nyingi mtoto ndiye mwenye kosa) uamuzi wa busara na wa kujenga utolewe.

    Wadau tuna safari ndefu ya kufikia malengo, lakini tusigeuke nyuma. Naamini wadau ni chachu ya mabadiliko nchini.
    I stand to learn more from you all.

    Mdau mwenzenu

    Geoff I. Mwambe

    Mannheim

    ReplyDelete
  37. TATIZO LETU WATANZANIA TUNA "OLD SCHOOL MENTALITY" HATUKO TAYARI KUFUNDISHWA KITU KIPYA AU KUELEKEZWA TUKIAMBIWA TUFANYE HIVYO YANAZUKA MANENO MANENO YA KICHINI CHINI AMBAYO NI MAJUNGU.NADHANI HATUJAWEZA KU-TUNE AKILI ZETU KUPOKEA KITU KIPYA ZAIDI YA KUFANYA TULICHOZOEA SIYO KWENYE MICHEZO TU HATA MAKAZINI(HUKO NDIO USISEME)WATU WAPO WAPO NA ZILE MENTALITY ZA ZAMANI ZAMANI TU KITU AMBACHO KINAFANYA MABADILIKO YAWE MAGUMU KATIKA KILA KITU TANZANIA.UKIANGALIA TU HAYO MAELEZO HUNA HAJA YAKUELEWESHWA TATIZO NI NINI KILA KITU KINAJIELEZA...MAJUNGU BAADA YA KUSHINDWA KU-PERFORM.MBONA WACHEZAJI WENGINE HAWAGUSWI NA MAXIMO?KWA NINI HAWAJIULIZI HATA INGEKUWA MIMI NI MWALIMU UKIFANYA VIZURI SIKUFUATI FUATI LAKINI UNAFANYA VIBAYA LAZIMA NITAKUULIZA MBELE YA WOTE.KWANI KUNA SIRI GANI?UMEFANYA VIBAYA,BASI UWAJIBIKE SI KUPIGA DOMO NA KULALAMA.NDUGU WATANZANIA TUNA MWENDO MREFU MBELE KAMA HATUBADILIKI...UJINGA MTUPU

    ReplyDelete
  38. MAXIMO IS THE BEST COACH. KWA MAPENZI YA TIMU ANACHUKIA KUCHEZA BELOW STANDARD. MMEZOEA MAKOCHA MARAFIKI WANAWA-DEKEZA KWAKUJIONA MASUPASTAA

    NDOMANA HAMUENDELEI WALA SOKA YA BONGO HAIINUKI.

    BIG UP MAXIMO-GOOD JOB-WAMEZOEA WABONGO MAJUNGU, MANENO,MIDOMO, MAJUNGU, KUDEKA NA KUBEMBELEZWA

    MNGEKUWA VITANI TUNGEKUFA WOTE KWA AJILI VISINGIZIO KAMA HIVI. BE THE SOLDIERS BOYS-BE SERIOUS.

    MAXIMO AMEONESHA NI BEST KAMANDA-HADEKEZI

    ReplyDelete
  39. JAMANI NYIE MACOCHA MNAO LAZIMISHA AJIRA PELEKENI BASI HIZO CV ZENU, ALAAA MBONA MWABOA HIVYO? TUMEWACHOKA KABISA YAAANI MWATIA KINYAAA, BASI NENDENI MKAMLOGE, MAANA NYIE MMEZOEA KULOGA HATA KWENYE GAME MWALOGA, KAA!
    LINDO BOY.

    ReplyDelete
  40. JAMANI HEBU NAOMBA TUELEWE WACHEZAJI HAWA, WANAFANYA MAMBO YA KIPUMBAVU, WANATAKIWA WAELEWE KUWA KATIKA TIMU ZA TAIFA HUWA HAKUNA MAJINA YA KUTEGEMEWA KAMA INAVYOKUWAKATIKA KLABU.

    IELEWEKE WACHEZAJI WOTE WANAITWA KATIKA TIMU YA TAIFA NI WALE WEN YE VIWANGO VYA JUU KATIKA NCHI NZIMA, IELEWEKE TANZANI YETU INA MIKOA 26 WACHEZAJI WALIKUWA ISHIRINI NA NATU, HIVYO WANATAKIKA KUSHUKURU NAFASI YA KIPEKEE YA KUITWA KATIKA KIKOSI CHA STARS WALIYOIPATA.

    SUALA LA KUPANGWA KATIKA TIMU UWE UMEPONA ANA UNA KIWANGO CHA JUU SANA, HAJARISHI KUMLAUMU MWALI KWA SABABU HIYO NI KAZI YAKE ANAONA NI NANI ANAFAA KUCHEZA MCHEZO GANI.

    MBONA KUNA WACHEZAJI WENGI HAWAKUCHEZA NA HAWAJASEMA LOLOTE, AHALAFU HAWA WANAOBWATU UKIWAULIZA WANATAKA KUWA WACHEZAJI WA KULIPWA SASA WATAWEZA KWELI.

    KUNA WACHEZAJI WA KULIPWA NJE WANAKAA NUSU MSIMU AMA MSIMU MZIMA HACHEZI NA HAZUNGUMZI LOLOTE KWA SABABU ANA HESHIMU MAAMUZI YA MENEJA WA KLABU YAKE.

    JAMANI WATANZANI TUNAKWENDA WAPI, MAXIMO NI KOCHA MZURI SANA NA IELEWEKE ALIIKUTA TANZANI IKIWA KATIKA HALI MBAYA SANA NA WALA TULIKUWA HATUITAMANI HATA KUISIKIA TIMU YETU YA TAIFA.

    CHUJI KAJENGEWA JINA NA KOCHA HUYO, BOBAN KAJENGEWA JINA NA KOCHA HUYU TENA NASTAHILI KUMUHESHIMU KWANI KAMA KUMTEMA ALIKUWA KISHAMTEMA SIKU NYINGI KAMA WATU MAKUMBUKA ALIFANYA KOSA MCHEZAJI HUYU LA KUCHELEWA KAMBINI KAONDOLEWA KATIKA KIKOSI CHA STARS KWA NINI HILO HALIKUMBUSHII??????

    NAIMANI TANZANI NI KUBWA NA INA WACHEZAJI WENGI, NA TUTAFANYA VYEMA HATA TIMU YOTE ILIYOKWENDA IVORY COAST IKIAMULIWA KUVUNJWA, KWA SABABU HIVI SASA WACHEZAJI WANA KIU YA KUCHEZA SOKA TANZANIA NA IFAHAMIKE KATIKA TIMU YA TAIFA SI SEHEMU YA KUTENGENEZA JINA ILI UWARINGIE WENZAKO WE NANI BWANA.
    WATANZANI WENGI WNAIPENDA TIMU YAO NA HATUTAKI KUSIKIA UPUMBAVU WETU.

    SASA MMETANGAZA KUJIOTO TUONE KAMA TANZANIA HAITOFANYA VIZURI KATIKA MICHUANO YA KIMATAIFA INAYOKUJA, NA HII NI NAFASI TOSHA KWA KOCJHA WETU MWENYE KIWANGO KUTENGENEZA VIJANA ALIOWAITA KWA KUWAHATUPO KATIKA MICHUANO YOYOTE KWA SASA.

    KI UFUPI NINAMUOMBA YOYOTE ANAEJUA SOKA AFUATILIE MKASA NA SIR FUGERSON NA BECKHAM HADI ILIPOFIKIA WAKATI KIUNGO HUYO ANAUZWA KUTOKA MAN UTD HADI REAL MADRID, MBONA HAKUZUNGUMZA LOLOTE NA KULIKUWA KUNA MKWARUZANO MKUBWA KATI YAO NA MPAKA LEO BECKHAM HAJASEMA LOLOTE, NAIMANI YEYE ANA MALENGO YAKE KIMAISHA NA KUTAKA KUULINDA MPIRA WAKE PIA, SASA IWEJE HAWA VICHENCHEDEEEE WATUUMIZE KICHWA!!!!!!!!!!!!!.

    ReplyDelete
  41. mh ni vizuri tusikie na upande wa pili unasemaje kuhusiana na hili (maximo) mimi naamini si kila siku mchezaji anakuwa fiti uwanja kwa 100% sasa hatujui kama kocha alikuwa na ushahidi mwingine zaidi ya huo uliomfanya afanye maamuzi hayo. Nafikiri pia wachezaji wanahitaji vitu vingi sio mazoezi peke yake na elimu saikolojia wapewe na inawezekana pia Maximo alikuwa na stress sana na presha juu ya kushinda maana huo ndio mtihani wake uliokuwa umebaki. Viongozi wa msafara na uhakika mtakuwa mmeandaa ripoti ya mashindano ambayo mtaiwakilisha kwa wahusika na ripoti hii itakuwa na maelezo ya kina kuhusiana na hili na kama Maximo aliteleza ni vizuri akaelezwa na kama ni wachezaji ni vizuri wakaelezwa hii yote ni katika jitihada ya kukuza kiwango cha mpira hapa Tanzania.

    ReplyDelete
  42. Maelezo haya yanadhihirisha wazi kwanini wachezaji wetu wengi hawawezi kuendelea kisoka, wanasema walikuwa chini ya kiwango halafu bado walitaka wapengwe kucheza, kocha anamamlaka ya kumpanga nani acheze na nani akae benchi. Pia nyie wachezaji acheni ubinafsi na majungu kama hauko fiti unang'ang'nia upangwe ya nini? Hata waliopangwa si watanzania na wana haki ya kucheza kama nyinyi. Ushauri wangu: Ongezeni bidii ya mazoezi na muwe adabu ya kufuata malekezo ya kocha na viongozi wa timu ili mnyanyue kiwango chenu.Chukulieni kukosolewa kama changamoto ya kufanya mabadiliko ya uchezaji na tabia zenu

    ReplyDelete
  43. nini hiki sasa?
    utoto,umaarufu unawasumbua sana na hamna profesheno kabisa
    yan nimesoma tu ao juu wawili nikachoka kabisa izo sababu za "KUFISADI NCHI"

    grow up vijana na acheni bangi na uswahili
    taaluma ni tofauti na bla-blah

    KIPILI kasema sawa sanaaaa,mmezeeka sana tunaitaji soka la makinda wachanga,tatizo kujuana kwingi soka la bongo,yan hao-hao km jezi bwana??

    mnaboa sana

    ReplyDelete
  44. Kufumba na kufumbua serikali ikaja na jina la Maximo na haikujulikana anatokea wapi {ingawa aliwahi kufundisha timu ya Livingstone (nirekebishwe km nimekosea) ya Scotland kwa muda}. TFF wakaduwaa na hawakuwa na cha kufanya. Kwa hiyo haya yanayotokea hatushangai kwani Maximo hana uzoefu na timu za taifa, si mkufunzi (hivyo suala la saikolojia ni doubtful) na hata kufundisha makocha wa ndani hajafanya.
    quote..
    Geoff Mwambe.

    Please fanya utafiti kwa habari yako hapo juu.
    Kama wewe hujui, si kosa, kwamba ulishangaa kuona hilo jina, si kosa, lakini kusema hadharani kwamba ofisi ilishangaa ni kosa kubwa. Mimi japo si mfuatiliaji, kidogo niliona mchakato uliokuwapo wakati ule!!!
    Kama tunajadili maelezo ya wachezajibasi tuendelee nayo, kuna mjadala wa maximo uko humu humu jiunge na tuma maoni yako.
    Maximo si Mtanzania, ataondoka atuachie soka letu, je litabaki na watu wa aina gani?
    Tutetee ujinga huu kwa ajili tunataka maximo aondoke? La hasha, Vijana wamekosea sana, wanajimaliza wenyewe, malengo yao hayatimii, malengo ya taifa hayatimii. Kazi ya soka si rahisi, kama ambavyo wengi wangependa iwe, inahitaji nidhamu masaa yote, ni jambo gumu kwa yeyote kati yetu.
    Lakini kama hawa wameamua wanataka tunawasaidia, tunawajenga kwa kuwasema wabadilike, kwa faida yao na ya wapenzi wa soka, si kwa kumtetea maximo au waliomleta.
    BAHATI MBAYA SOKA BILA NIDHAMU HAIPO, LABDA KWA STAREHE LEADERS CLUB JUMAPILI.
    lazima kushinda mwili, a bangi, na kiburi, nk.

    ReplyDelete
  45. Uhitaji kufikili sana ili kupata jibu/ inaonekana vijana walikuwa wamevimba vichwa walijiona kuwa wamefika kileleni. iki ndicho kinachowaponza wachezaji wetu wa bongo. mchezaji anatakiwa kujifunza kila siku na kuwa na heshima kwa kocha wa timu. Rekebisheni tabia bado amjafika.

    ReplyDelete
  46. Michuzi mambo?Nadhani hawa wachezaji walikosea,haiwezekani kila blogger awaseme wamekosea nikiwemo na mimi.Watakuwa wamesoma wameelewa,wakaombe msamaha kwa kocha.MFANO MZURIM NI MGOSI(MUSSA HASSAN),KOCHA ALIZOEA KUMWANZISHA BENCHI WATU WANAPIGA KELELE LAKINI HATA SIKU MOJA HATUJAWAHI KUMSIKIA MGOSI AKILALAMIKA ZAIDI YA KUONGEZA BIDII KATIKA MAZOEZI HADI KUMSHAWISHI KOCHA KUMWANZISHA.TUMESIKIA MAFANIKO ALIYOYAFIKIA!KWANI NINI NYIE WENZENU MSIJIFUNZE.NAKUPONGEZA MGOSI-KEEP IT UP.ULIKUWA UNAONEKANA KABISA UNAPIGANIA NCHI ZAKO KWA JUHUDI BINAFSI WAKATI MWINGINE.WE NEED MGOSI TYPE OF PLAYERS.

    ReplyDelete
  47. Kocha Sir Alex Ferguson wa ManUTD ana eleweka wa wadau wote wa soka la Uingereza kwa kuwapiga 'Hair dryer' wachezaji wake wakati wa mapumziko ktk mechi au mazoezi.

    Kila mmoja anajua Hair Dryer inavyopiga kelele wakati wa kukausha nywele full blast.

    Wachezaji wa ManUTD, Uongozi na washabiki hawauingilii staili ya Sir Alex kulipuka kwa makelele ikiwa wachezaji wameshindwa kufikia kile walichokubaliana.

    Hivyo Boban, Chuji na wengine mkubali staili za Maximo maana ndio aliyepewa majukumu ya jinsi ya kukiongoza kikosi chake ktk soka. Soka ni sawa na 'vita' kwa kutumia mpira baina ya nchi na nchi au klabu na klabu. Hivyo ktk vita hakuna lelemama ni kutekeleza yale ya bosi au ukiweza mchezaji fanya 'ubunifu' kocha akubali kuwa ubunifu wako utaleta mafanikio ktk hiyo vita chini ya kiongozi wako.

    Bila hivyo huo ni utovu wa nidhamu na ukosefu wa 'professionalism'.

    ReplyDelete
  48. MJOMBA NI KAMA SIJAKUSOMA KIAINA FLANI KWANI YONDANI ALICHEZA MECHI GANI? NAHOFU HATA HAYO MAELEZO MENGINE.

    ReplyDelete
  49. LIFE WITHOUT PURPOSE
    LIFE WITHOUT VISION
    LIFE WITHOUT PLAN

    ayo ndo matokeo ya mtu/watu kutokua nayo ndo hizo claps wanazoongea ao vijana

    ReplyDelete
  50. honestly speaking, Tanzanian Players are so well behind from being so called professional players, if you dig deep down in the world football professional players history you ll see how behind Tanzanian players are (age wise,talent wise and personal effort wise), Maximo has done wonders to Tanzania's soccer(Bravo Maximo),i think the players should stop thinking of other things and concentrate on their job, i believe if you ve talent no matter where you are, you ll be seen, Kolo Toure came straight from Asec to Arsenal, so as many players,
    i think they should be thankful rite nw they play in a better ground(thank you BWM) n they get attention from the gvt(Viva JK)
    Wat these Players has done is so unacceptable in soccer, Coach is everything to the team, he knows you more than you know urselves, so stop behaving like cabs and start doing your job

    we need time, hardworking and discipline to become something in the world of soccer....wat we are doing rite now has been done for so many years in many countries, and we need more soccer academies to produce cream of soccer

    God bless Tanzania

    ReplyDelete
  51. Maximo hamna kitu.
    Tevez alikuwa na bifu na Fergusson juu usajili wa kudumu na liliwekwa kwenye vyombo vya habari.
    Gallas alikuwa captain wa ARSenal NA MAMBO YA SIRI YA DRESSING ROOM ALIYAWEKA KWENYE VYOMBO VYA HABARI.
    MAXIMO SIO KOCHA AONDOKE.ANA MAMBO YA AJABU UTAFIKIRI MTU NA MKE MWENZIE.
    KUNA MTU HAPO JUU KAWAPIGIA DEBE TFF KWENYE MCHAKATO WA KOCHA NADHANI NI MTU WA TFF WANAJIPIGIA DEBE. NI KWELI WALIFELI KUPATA KOCHA WA MAANA. HAWAKUPELEKA RIPOTI WA JK NDIO WAMESABABISHA TUMEPATA HUYU LOSER MAXIMO.MARA ANATAKA VIJANA BASI ACHUKUE TIMU YA VIJANA YA TINOKO.
    MDAU KISIJU.

    ReplyDelete
  52. Naona Ferguson...Ferguson....Ferguson...Ferguson..
    Je hakuna vigezo vingine?.... Vijana Malengo hawana wameridhika na Simba na Yanga...Timu zisizo na malengo...Nidhamu ni tatizo kubwa sana.....maandalizi ya vijana ni mabovu...Maximo ana kazi kubwa... vijana wanadhani/wanaamini mchezaji mpira mzuri lazima awe mvuta bangi. hamfiki popote zaidi ya Simba na Yanga.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...