Ali Kiba akiwa kwenye studio za Redio Maarufu kupita zote kwa vijana nchini Uholanzi Funx Radio,ambapo nyimbo ya Ali Kiba Cinderella ilikuwa namba moja kwa kipindi kirefu sana mwaka jana wakihojiwa Live  kuhusu Historia ya Ali Kiba na Muziki wa Tanzania kwa ujumla. 

Ali Kiba na Lolilo (mwanamuziki Kutoka Burundi) wakifanya makamuzi ya kufa mtu
ali kiba akipongezwa kwa nguvu na mashabiki

ali kiba akimwaga lazi jukwaani

Ali Kiba na Lolilo (mwanamuziki Kutoka Burundi)wamewaacha mashabiki hoi katika mji wa Bergen-Norway. Pia wapenzi wanaambiwa wakae mkao wa kula kwani wakali hawa wamerecord single pamoja mjini Bergen ambayo itatoka hivi karibuni.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 13 mpaka sasa

  1. Hivi mkuu wa nanii hiii huwa huna kitu kingine cha maana cha kutuwekea zaidi ya Ali Kiba Ali Kiba ????????????????

    ReplyDelete
  2. alikuwa anaongea lugha gani redioni huyo????

    ReplyDelete
  3. I can see the promoters are answering our comments, nimefurahi sana kuona mmempeleka Ali Kiba redioni.

    This is what I would like to see African promoters based in the western world do when our musicians visit those countries.

    Sio mnawapeleka kwenye klabu za waafrika tuu, watatoka vipi kimataifa.

    Ali K 4 Real!!!!!

    ReplyDelete
  4. Anony wa juu hapo kisicho cha maana kwako kwa wengine ni cha maana. Ali Kiba Ali Kiba kwa wengine ni muhimu kama yalivyo mambo mengine kwako c unajuwa hii blog ni ya watu wengi wenye interest tofauti tofauti??/.

    Ushauri ni kwamba kama kuna kitu kinakuboa unakiruka c lazima ukiangalie kwani vipo vingi humu vya kuangalia.

    ReplyDelete
  5. anonymous wa April 09, 2009 11:09 AM
    inaelekea una chuki binafsi!Ali Kiba is the most successful bongo flava artist katika upande wa tour so hate him or love him the kid is making money and expanding his fan base habari ndiyo hiyo

    ReplyDelete
  6. We anon wa kwanza kwani umelazimishwa kusoma au kuja hapa?

    Ebo? This is Issa Michuzi's blog and he is free to put what he wants.

    Kama humpendi Ali Kiba kanywe vipande vya chupa. Kuna wengine tunapenda kumuona anavyowapagawisha wazee wa kupiga box.

    ReplyDelete
  7. kwani we hater wa kwanza hapo juu umelazimishwa au unalipwa kusoma habari za humu ??

    ReplyDelete
  8. wewe hater wakwanza juu nakuomba usiwe na chongo kwani hilo box unalo piga sio baya ukirudi bongo utakunywa maji japo siku mbili na kwenu wata furahi hivyo ukitaka nawe kutangazwa poa kwani hii sio blog ya michuzi,michuzi ni mtumishi wa jamii hivyo kula kitu ile iko roho inapenda
    Ali Kiba mwache kama alivyo dogo anajituma na ameisha safiri sehemu nyingi kuliko wewe hivyo usikonde myonge myongeni haki yake mpeni

    ReplyDelete
  9. Aise hizi show zenu za ulaya mnazoziita "makamuz" au "kutesa ughaibuni" saa nyingine zinatufanya tulioko huku bongo tushangae kama kuna haja ya wasanii kuaga huku home kuwa wanaenda kupiga show ulaya. Kama hiyo picha hapo chini its like alikuwa kwenye mgahawa, kwa hesabu yangu ya kimaimuna sidhani kama hao watu wanazidi 300. Huyo kiba akiitwa kwenye kumbi uchwara za bongo mfano freetime resort, TCC au Wailes anapata watu mara 3 zaidi ya hapo, hapo hatujaongelea wakipiga launching ya albums kama diamond jubilee ukumbi unatapika kabisa.

    Mi nadhani mapromota wa nje mna kazi ya kutafuta wahudhuriaji wengi zaidi. Na msilenge watz na wakenya au waafrica wachache. Sio mbaya mkitangaza hata kwa ngozi nyeupe coz nna uhakika wapo wengi wanaopenda kuchek wasanii wetu wanafanya nini ila hawapati habari. Then hamishieni kwenye kumbi kubwa kidogo.
    Ni hayo tu.
    Jason

    ReplyDelete
  10. mi namuunga mkono huyo anaeitwa hater.
    mgema akisifiwa sana, basi mnazi huujaz maji. kwani hakuna wasanii wengine wanaozunguka huku na huko lakini kila kukicha kiba, kiba, kiba kiba. mwisho itakuwa KIBAKAAAAA

    ReplyDelete
  11. MICHUZI SIYO MTUMISHI WA JAMII. MICHUZI NI MTUMWA KWA HONGO INGAWA KILA MTU ANAISHI HIVYO LAKINI N'JOMBA HAPO TUUUU MACHI. INABOA HATA WE MWENYEWE KIBA UNA BORE. WEKA VITU HADHARANI SIYO KUFICHA MAONI YA WENGINE. KAMA NI YA JAMII BASI KILA NALO ROHONI NA KULITUMA HUKO KWA MPENDA HELA, LITOLEWE. AU NA SIYE TUTOE KITU KIDOGO NDIYO TUTAWEKWA KWENYE BLOG HII. WE MICHUZI UMEKATAA MESEJI ZANGU KIBAO UNATAKA NIKUKATIE KIDOGO ETI GARI YAKO INAHITAJI KIWESE. N'JOMBA NOOOMA HATA KAMA NDIYO KUKATIA LUPASO SIYO, NINGEKUPA TU LAKINI NDO HIVYO TENA POCHI BADO LIPO LUZI SIYO.
    NIMELONGA

    ReplyDelete
  12. Hujui unachosema nafikiri. Kama Wailesi au TCC anapata watu 300 basi zidisha na kiingilio cha shilingi za TZ uone anapata sh ngapi jumla. Then uangalie kwamba akipata watu 100 hapa Norway, France au UK, ukizidisha kwa Pound wanazolipa jumla utakuta ni sawa na kuingiza watu 1000 hapo TZ kimapato.
    Pia haji kwa show tu, anakuja kwa exposure na kuonana na wanamuziki wengine wa nje. Ndio maana mwaka jana mzima alikuwa nje ya nchi akizichanga na huwezi mlinganisha na yule aliyebaki hapo mwaka mzima.
    Ali kiba ana miziki michache sana lakini anafanya kazi ya ziada kuiuza kwa style ya kutoka nje ya nchi. Mpe hongera huyu mtoto kwa bidii ya kujituma na kutokuwa na majigambo baada ya kutoka stejini.

    ReplyDelete
  13. SASA HUYU KIBA ANAWAKILISHA NINI?
    MAANA WAJAMAIKA WANAWAKILISHA UTAMADUNI WA REGGAE NA RASTAFARISM, WAAMERIKA WANAWAKILISHA UTAMADUNI WA MUZIKI WA KIMAREKANI YAKIWEMO MAVAZI, NYWELE, N.K. SASA HUYU ALI KIBA YEYE ANAWAKILISHA UTAMADUNI WA TZ, AFRIKA AU WAPI, MAANA SIONI TOFAUTI BINA YAKE NA WAIMBAJI WA KIMAREKANI, MARAPA. SASA YEYE NI MWAKILISHI WA BONGO AU NI MTUMWA WA UKOLONI MAMBOLEO, MAANA NAONA ANAJITAHIDI KWA NGUVU ZOTE KUIGA MITINDO YAO, HAPO NUSRA HIYO SURUALI YAKE IMPOROMOKE.
    KWANGU MIMI HUKU NI KUKUBALI KUTAWALIWA KWA BEI RAHISI SANA.
    SIAMINI MHE. MICHU UNAWEZA KURUHUSU BLOG YETU YA JAMII IENDELEE KUFAGILIA UKOLONI MAOMBOLEO AMBAO UATUSHUSHIA THAMANI YETU NA KUDHARAU MILA ZETU.
    HAWA VIJANA WENGI WAO NI WACHACHE WA ELIMU, WACHUKULIWE WAKAPEWE SOMO KK NYANJA ZA SIASA NA HISTORIA, NA SISI WANAJAMII TULAANI VIKALI SHOMBO HILI.
    NYAMAFFF

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...