ubunifu na mapambo ya nguvu huonekana katika shoo za bongo kama haya ya kili music awards
bosi wa masoko wa tbl david minja (pili kulia) akiwa na meneja wa kilaji cha kilimanjaro lager oscar shelukindo (pili shoto) na wadau katika maandalizi ya kili music awards wikiendi iliyopita

pamoja na kuwa mwanamuziki mkongwe na kilimanjaro band wana njenje, keppy kyombile pia ni fundi mitambo mahiri wa sauti katika matamasha mbalimbali, akiwa mtaalamu wa makonso ya aina zote. aghalabu humkosi kwenye matamasha toka ya ziff na sauti za busara kule zenj na yote yafanyikayo dar.
mabingwa wa kushuti video na tv wa 2eyez  production wakiwa na vyombo vya kisasa vya kwao na vya digital art productions huwa makini na kazi zao
majukwaa hupambwa kwa ustadi na huvutia pia kwa mapambo na taa za kisasa
kila kitu kinatengenezwa hapahapa bongo
muziki wa nguvuna vikorombwezo kibao vya kisasa vipo bongokwa shoo ya aina yoyote ile. huu mzigo ambao uko full nondo ni wa prime time promotions ambayo pamoja na sauti pia wana jukwaa ka kisasa linaloweza kutumika hata na wacko jacko
juu na chini ni ukumbi wa diamond jubilee hall kabla ya hafla ya kili music awards

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 10 mpaka sasa

  1. Bongo kweli tambarare lakini BILA UMEME TUTAFIKA KWELI?????

    ReplyDelete
  2. mtoamaoni wa kwanza huna jema??bongo tambarareeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee

    ReplyDelete
  3. JUST ONE WORD-"FANTASTIC". ILA NA BARABARA NAZO NA MITAA IWE KAMA HIVI, LOL.

    ReplyDelete
  4. na parking ziwe hivi hivi

    security
    valet parking
    na sura za tabasamu kwa wahudumu wanaokaribisha watu

    ReplyDelete
  5. kuna watu wabeba mabox ulaya na marekani wanaboa, kila kitu cha bongo wanaponda. wanatia kinyaa, nyumbani ni nyumbani, hta ikiwa unakaa chini ya mti. East or West, home is best

    ReplyDelete
  6. Tusikasirike inatakiwa miundo mbinu kwanza na sio vinginevyo!

    ReplyDelete
  7. BONGO TAMBARARE TOKA ZAMANI . YATEGEMEA POSITION YAKO KIMAISHA KWA WAKATI HUSIKA .

    ReplyDelete
  8. duh! video mixer kwenye sherehe ahaaaa kumbe ndiyo maana video za kibongo ni vichekesho...!

    ReplyDelete
  9. SHELUKINDO UPO HABARI YA MIAKA MINGI?NAONA UPO TBL KWA MBELE,TULIKUWA WOTE AGUMBA COMPUTER MIAKA YA 200-2001.PALE JENGO LA USHIRIKA,TUPE NAMBA YAKO BASI TUKUSALIMIE RAFIKI.UKEREWE

    ReplyDelete
  10. We anonymous wa 11.06 a.m unayetaka namba ya Shelukindo, si umeshaambiwa ni yeye ni meneja wa Kilimanjaro Lager hapo TBL? Basi piga simu TBL umwulizie utampata ! Sio lazima aweke namba yake kwenye hii blog ya jamii !

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...