timu zote mbili siku ya mechi ya Bongo FC na Kilimanjaro mwaka jana huko Stockholm


Na Ripota wa Globu ya Jamii, Helsinki
Timu za Watanzania za FC BONGO ya Finland na KILIMANJARO ya Sweden zitachuana rasmi siku ya Jumamosi tarehe 27.6.2009 katika viwanja vya Finnair Stadium Helsinki Finland.

Timu hizo ambazo zilichuana kwa mara ya kwanza mwaka jana huko Stockholm na Kilimanjaro wakabahatika kuwafunga Fc Bongo mabao 4-3 kwa taaabu.

Inasemekana kuwa Fc Bongo walichukiwa sana na
uamuzi wa refa kuwapa bao la nne vijana wa kilimanjaro kwa mpira ambao ulikua ushatoka nje, pia baada ya mpira kuisha wakapewa pilau dume bila ya nyama kiasi hata wageni wengine walikwamwa na pilau kavu na kupata huduma ya kwanza.

Habari kutoka Helsinki zinasema kuwa Vijana wa Fc Bongo wanajinoa vibaya sana ili kulipizia kisasi watani wao hao wa jadi kutoka nchi ya jirani. Habari zaidi zinadatisha kwamba safari hii benchi lao la ufundi litaongezewa nguvu na kibabu kimoja kutoka Lamu, nchini Kenya, ambacho kinawasili usiku huu.

Kocha na Mlezi wa Fc Bongo Abdalla Ezza (hahaha sasa anaitwa Hiddink) ameahidi kuwapa fundisho kubwa la kandanda kwa wageni wake hao wa Kilimanjaro, anaamini kikosi kilichoenda stockholm mwaka jana kilikua hakijatimia kwani wachezaji wake (Key Players) wengi hakuweza kusafiri nao kwani walikua ndio kwanza wamerudi makazini kutoka kwenye likizo zao za summer na hawakuweza kupata ruhusa makazini.

Nao Kilimanjaro wakizidi kujiamini kuwa wataweza kuwanyamazisha wenyeji wao huko Helsinki. Ripota wa Stockholm ameshuhudia timu hiyo ikijifua kisawasaw na kocha wa timu anayochezea Mohamed Athumani Machupa.

Habari zaidi kuhusu mechi hiyo tembelea website ya kilimanjaro hapa
http://fckilimanjaro.snabber.se/

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Kiama chao kinawasubiri hao Kilimanjaro, Watakoma ubishi mwaka huu, na biriyani ya mbuzi tutawalisha.

    ReplyDelete
  2. Mmechi mbona mwezi wa sita na umeandika jumamosi hii?

    ReplyDelete
  3. Walete hao kilmanjaro tuwatoe hangover za botini

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...