kiongozi wa msondo ngoma music band muhidin maalim gurumo akifafanua jambo kwa waandishi wa habari  kuhusu harambee iliyoanzishwa ya kila mljai wa safari lager kuchangia ili bendi hiyo ipate vyombo vipya. meneja wa safari lager, fimbo butala, yuko pembeni. jumla ya tshs. milioni 50 zinatarajiwa kukusanywa ili kuipatia bendi hii kongwe vyombo vipya.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. Kuna mtu atapigwa risasi....ngoja nikacheki wakwangu..Lol....mmenitisha..!!

    ReplyDelete
  2. Kila wakipiga musiki na kukusanya viingilio huwa wanasahau kuweka mbegu. Omba omba - utamaduni sasa.

    ReplyDelete
  3. mkulima kala mbegu........anaomba kwa jirani sasa.muziki mmpepiga miaka yote hiyo hamna hata akiba...ebooooo.

    ReplyDelete
  4. Ukienda kwenye shoo zao wanavyokutolea macho ulipe kiingilio, Utafikiri mjusi kabanwa na mlango,Wakitaka vyombo vipya wapolee, Nyooooooooo bin kudadeki.
    Mdau-Orlando,FL.

    ReplyDelete
  5. Wadau kumbukeni hii bendi kwa miaka mingi ya nyuma ilikuwa ni mali ya chama cha wafanyakazi kwa hiyo fedha zilizopatikana zilikuwa za mwenye bendi na wanamuziki walikuwa waajiliwa wakilipwa mshahara tu, hivi karibuni ndio wameanza kujitegemea na bendi kuwa mali ya wanamuziki kwa hiyo tusiwalaumu kwamba miaka yote walifanya nini. Ninawapongeza TBL kwa kuamua kuwasaidia msondo maana muziki wao ni bomba ila kwa umri wao hawawezi kukimbizana na bendi za vijana, ninashauri pia ingeanzishwa namna nyingine kwa ajili ya wanaopenda kuchangia bila kupitia kinywaji cha safari

    ReplyDelete
  6. nadhani hata mimi naunga mkono ushauri wa anony. hapo juu ili kuisaidia bendi yetu ni kweli wangeanzisha na njia nyingine ya mchango,kwa njia hii ya safari beer inatubana kidogo wengine.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...