JK akiweka saini kitabu cha Maombolezo leo Nyumbani kwa marehemu bibi Asha Adam Sapi Mkwawa wakati Rais Kikwete alipokwenda kutoa heshima zake za mwisho na kuwafariji ndugu wa Marehemu. Bibi Asha alikuwa mke wa Marehemu Adam Sapi Mkwawa aliyekuwa spika wa Zamani wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mwili wa Bibi Asha ulisafirishwa baadaye kwenda Iringa kwa Mazishi
JK akiwafariji ndugu na jamaa wa Marehemu bibi Asha Adam Sapi Mkwawa leo wakati Rais alipokwenda kuwapa pole kufuatia kifo cha mke huyo wa spika wa Zamani wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 9 mpaka sasa

  1. Inalilahi wainailahi rajiun. Poleni wote ndio wote tunaelekea njia moja. tuliokuwa Duniani tukumbuke Kusoma kuswali na Kuwaombea Dua waliopita. Abdu Pole kaka.

    ReplyDelete
  2. Mzee Wa Zeze, Columbus, OhioApril 28, 2009

    Poleni sana wafiwa wote mlioko Dar, Iringa( Kalenga), US na kwengineko.
    Mola aiweke pema roho ya marehemu Bi. Asha Mkwawa.

    ReplyDelete
  3. poleni sana watu wa iringa kokote mlipo mzee sapi aliliwakilisha vizuri sana bunge kwa kusimamia vema nidhamu ya wabunge na kuweza kuendeleza libeneke la maswali na majibu pamoja na mijadala mbalimbali kwa nidhamu ya hali ya juu bwana alitoa na bwana ametwaa jina la bwana lihimidiwe!!!!

    ReplyDelete
  4. heeeee bibi yangu umefariki??

    yani naona apa ktk blogu??

    ndugu zangu poleni sana,na mfike salama iringa-kalenga kwa mazishi ya mpendwa wetu

    inguluvi itange!!

    ndugu yenu

    ReplyDelete
  5. Pokeeni salaam za rambirambi wafiwa wote,hususan watoto wa marehemu na ndugu kwa karibu kabisa,polei wana wa Kalenga wote,wanyalukolo wote wa mkoa wa Iringa na popote ulimwenguni,kwa watanzania wote waishio mkoa wa Iringa,kwa ndugu watanzania wenzangu wote.Tuko nanyi katika wakati huu mgumu na wa majonzi makubwa.Lakini alochokiamua Mwenyezi Mungu hakuna mwenye uwezo wa kukitengua.Sote tulimpenda sana mama Asha Mkwawa,lakini yeye Muumba kampenda zaidi!Ailaze mahala pema peponi roho ya marehemu,amina!

    ReplyDelete
  6. Poleni sana majirani zangu. tupo pamoja kuomboleza msiba huu mzito. Safari njema ya Kalenga ya kumsindikiza mpendwa wetu ktk nyumba ya millele.

    ReplyDelete
  7. Inna lillah wainna ilaihi rajiun. Poleni sana ndugu zetu kwa msiba huu wa mama yetu mpendwa. Inshaallah Mwenyeezi Mungu Subhanahu Wataala atawapa subira katika wakati huu mgumu na Inshaallah atampa marehemu kauli thabit na kumweka pema, Aamin.
    Pole sana Eddie Sapi.

    ReplyDelete
  8. Tangaulia segito Asha, kamweleze Mwagito Mkwavi Sitta (samwel) ameharibu misingi yote aliyoweka.

    ReplyDelete
  9. Poleni sana wanafamilia. Mungu ailaze roho yake mahala pema peponi. Amen.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...