mdau katuletea taswira hii ikumuonesha baba wa taifa mwalimu julius kambarage nyerere akipozi na watu wanaoonekana kuwa waarabu. bahati mbaya mdau hakusema hii ilikuwa lini na wapi na nini kilikuwa kinaendelea. wenye data tunaomba msaada tutani wa kuelimishana

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 14 mpaka sasa

  1. Michuzi,

    Hii inaonekana kama ni Mwalimu alikuwa Zanzibar na alivaa suti nyeusi nafikiri ni Abeid Karume.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 12, 2009

    Ushahidi wa taswira inaonyesha kwamba Picha hii ilipigwa kati ya mwaka 1960 na 1961 wakati Mwalimu akiwa Chief Minister wa Tanganyika, mahali ilikuwa ofisini kwake ushahidi hakuvaa koti, hivyo alikuwa mwenyeji wa mkutano na ofisi hii ilikuwa ni pale ilipo sasa Wizara ya mambo ya Nje, angalia ukutani bado ilikuwepo picha ya Malikia Elizabeth kwani uhuru kamili ilikuwa bado, hao wageni ni viongozi wa jamii ya ki Yemeni waliokuwa Tanganyika, wadau changieni!

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 12, 2009

    mwaka 1961

    mojawapo ya ofisi za serikali darisalama,akikutana na jumuiya ya kiarabu toka nchi gani"sikumbuki"
    ili kuwekana sawa ktk maswala ya kiimani tanganyika,nchi haitaongozwa na udini "secular state"

    asante

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 12, 2009

    hapana shaka yoyote sura ni za kizanzibari, mapozi ya kizanzibari na hata achitecture ni ya kizanzibari. Mtuma picha anaweza kuthibitisha hilo.

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 12, 2009

    Hii picha inaonyesha Nyerere alikuwa bado kijana sana,miaka ya 50 au 60 hivi, je kulikuwa tayari kuna coloured photos kweli?

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 12, 2009

    Seif Shariff HAmad naye hakukosekama kwenye hii picha (mwenye kaunda suti)

    ReplyDelete
  7. AnonymousJune 12, 2009

    Nadhani hawa ni baadhi waliopigania uhuru TZ na niwale waliomfungisha Swaumu/Mwezi wa Ramadhani julius

    ReplyDelete
  8. AnonymousJune 12, 2009

    Ndugu zake Osama

    ReplyDelete
  9. AnonymousJune 12, 2009

    hawa si waYEMEN kama yupo mmoja au wawili lakini wengi wao wazi wanaonekana ni waOMAN. pasipoti yao ni hiyo midevu na vilemba!
    inawezekana ni jumuia ya waarabu mchanganyiko walimtembelea mwalimu au jumuia ya waoman waliokuwa wakiishi mabara au toka zanzibar.

    ReplyDelete
  10. AnonymousJune 13, 2009

    Wapigania uhuru wa Jamii ya Watu Wa Oman kutoka kule Zanzibari na Dar Es Salaam katika moja ya ofisi za Sirikali mwaka 1961. Hakuna viongozi wowote wa TANu isipokuwa Nyerere mwenyewe. Kwenye kona kuna mtu mweusi (nikimaanisha sio mwaarabu) ni mmoja wa watu waliokuwa katika ofisi za Karume Zanzibar jina nimelisahau.

    Mzalendo wa TANU.

    ReplyDelete
  11. AnonymousJune 13, 2009

    hizo ni hekima na busara za mwalimu!!!

    Mdau canada.

    ReplyDelete
  12. AnonymousJune 13, 2009

    Ni kweli tulikuwa na maduka mengi ya 'Washihiri" hapo Dsm Mnazi Mmoja na Lumumba street mpaka miaka ya 1970 na pia walikuwa wazuri ktk biashara ya "mali kwa mali'', je ndugu zetu hawa "washihiri'' wamepotelea wapi wadau?
    Mdau
    Max
    'Mtoto wa Mjini'
    Sasa nipo New Wales, Australia

    ReplyDelete
  13. AnonymousJune 14, 2009

    aaa hii picha imetolewa kutoka blog ya forodhani[ muulizeni golden eye ndio anajua ni wapi hapo]

    ReplyDelete
  14. AnonymousJune 14, 2009

    michizu ama picha hii ilikuwa ni wengi waomani walikuwa wana harakati wa TANU. ilikuwa mwaka 1961.

    mmoja katika hao wazee walioko mbele ni mzazi wangu.

    mzee batashi ni marufu sana kwa baba wa MAREHEMU BABA WA TAIFA maana alicahngia hata pesa za kwenda UNO.

    hivyo hao na wakareketwa wa TANU siku hizo na baba yangu sikumbuki card number yake lakini ndio za mwanzo.

    pia BABA wa taifa aliwakaribisha na kuwaambia wasiwe na shaka yoyote juu yake yeye ni mtoto wao.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...